Zaburi 111 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 111:1-10

Zaburi 111111 Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.

Sifa Za Bwana Kwa Matendo Ya Ajabu

1111:1 Za 34:1; 109:30; 115:18; 145:10; 9:1; 89:7; 1:5Msifuni Bwana.

Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote,

katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.

2111:2 Ay 36:24; Za 143:5; 64:9; Ufu 15:3Kazi za Bwana ni kuu,

wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.

3111:3 Za 112:3, 9; 119:142Kazi zake zimejaa fahari na utukufu,

haki yake hudumu daima.

4111:4 Kum 4:31; Za 86:15Amefanya maajabu yake yakumbukwe,

Bwana ni mwenye neema na huruma.

5111:5 Mwa 1:30; Za 37:25; 103:11; 105:8; Mt 6:26, 31-33; 1Nya 16:15Huwapa chakula wale wanaomcha,

hulikumbuka agano lake milele.

6111:6 Za 64:9; 66:3; 105:44Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake,

akiwapa nchi za mataifa mengine.

7111:7 Za 92:4; 19:7; 119:128Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki,

mausia yake yote ni ya kuaminika.

8111:8 Za 119:89, 152, 160; Isa 40:8; Mt 5:18Zinadumu milele na milele,

zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.

9111:9 Za 34:22; 103:4; 130:7; 30:4; 99:3; Lk 1:68; 1:49Aliwapa watu wake ukombozi,

aliamuru agano lake milele:

jina lake ni takatifu na la kuogopwa.

10111:10 Ay 23:15; Kum 4:6; Za 19:9; 119:98, 104, 130; 28:6; 89:52Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima,

wote wanaozifuata amri zake wana busara.

Sifa zake zadumu milele.