Zaburi 11
Kumtumaini Bwana
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
111:1 Za 7:1; 50:11; Mwa 14:10Kwa Bwana ninakimbilia,
unawezaje basi kuniambia:
“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
211:2 Za 7:10, 13; 10:8; 58:7; 2Sam 22:35; Ay 33:3Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,
huweka mishale kwenye uzi wake,
wakiwa gizani ili kuwapiga
wale wanyofu wa moyo.
311:3 Za 18:15; 82:5; Isa 24:18Wakati misingi imeharibiwa,
mwenye haki anaweza kufanya nini?”
411:4 1Fal 8:48; Za 18:6; 27:4; 33:18; 66:7; Yon 2:7; Mik 1:2; Hab 2:20; Ufu 4:2; Mt 5:34; 23:22; Mit 15:3; Efe 5:13; Ebr 4:13Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu;
Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.
Huwaangalia wana wa watu,
macho yake yanawajaribu.
511:5 Ay 5:17; 23:10; 28:28; Za 94:12; 5:5; 45:7; Isa 1:14; Kum 7:13Bwana huwajaribu wenye haki,
lakini waovu na wanaopenda jeuri,
nafsi yake huwachukia.
611:6 Ufu 9:17; Ay 1:19; Mwa 9:24; 41:6Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali
na kiberiti kinachowaka,
upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
711:7 2Nya 12:6; Ezr 9:15; Za 9:8; 33:5; 99:4; 17:15; 140:13; 2Tim 4:8; Yer 9:24; Isa 28:17; 30:18; 56:1; 61:8; Ay 1:1; Lk 23:50Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki,
yeye hupenda haki.
Wanyofu watauona uso wake.