Yoshua 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Yoshua 6:1-27

Yeriko Yatekwa Na Kuangamizwa

16:1 Yos 24:11Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.

26:2 Kum 7:24; Yos 8:1; Amu 11:21; 2Sam 5:19; Neh 9:24; Dan 5:18-19Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita. 3Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita. 46:4 Kut 19:13; Law 25:9; Hes 10:8; Amu 7:16Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo. 56:5 Kut 19:13; 1Sam 6:15; Ezr 3:11; 10:12; Za 42:4; 95:1; Isa 8:9; 42:13Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”

6Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.” 76:7 Kut 14:15; Hes 10:35; 1Sam 4:3; 7:1Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”

86:8 Yos 4:13Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata. 96:9 Hes 2:31; Isa 52:12, 13; Hes 10:25; Isa 42:11-13Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa. 106:10 1Sam 4:5; Ezr 3:11Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!” 11Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.

126:12 Kum 31:25Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana. 136:13 1Nya 15:26; Gal 6:9Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia. 14Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.

156:15 1Fal 18:44; 2Fal 4:35; 5:14Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba. 166:16 Amu 7:20; 2Nya 14:14Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu! 176:17 Law 27:28; Kum 20:17; Isa 13:5; 24:1; 34:2-5; Mal 4:6; Yos 2:14; Mwa 13:3; 1Sam 15:6; Mt 10:41; 25:40; Ebr 6:10; 11:31; Yak 2:25Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma. 186:18 Yos 7:1, 12, 25, 26; 1Nya 2:7; Kum 7:26; 13:17; Isa 52:11; Rum 12:9; 2Kor 6:17; Efe 5:11; 1The 5:2; 1Fal 18:17, 18Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu. 196:19 Hes 31:22Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”

206:20 Law 25:9; Amu 6:34; 7:22; 1Fal 1:41; Isa 18:3; Yer 4:21; 42:14; Amo 2:2; Ebr 11:30Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji. 216:21 Kum 20:16; 1Sam 15:3, 8; 1Fal 20:42; Yer 48:18; Ufu 18:21Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.

226:22 Mwa 42:9; Yos 2:4; Hes 21:32; Yos 2:14; Ebr 11:30-31Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.” 236:23 Yos 2:13Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.

246:24 Hes 31:10; Kum 13:16Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana. 256:25 Amu 1:25; Yos 2:1; 2:1, 6; Ebr 11:31Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.

266:26 1Sam 14:24; Hes 5:21; 1Fal 16:34Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko:

“Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume

ataiweka misingi yake;

kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho

atayaweka malango yake.”

276:27 Mwa 39:2; Hes 14:43; Yos 9:1; 1Nya 14:17; Amu 1:9; 2Sam 7:9; Rum 8:31; 1Sam 2:30Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

約書亞記 6:1-27

耶利哥城塌陷

1因為害怕以色列人,耶利哥城門緊閉,無人出入。 2耶和華對約書亞說:「看啊,我已經把耶利哥及其王和英勇的戰士都交在你手中了。 3所有軍隊要每天繞城一圈,連續六天, 4讓七個祭司拿著七個羊角號走在約櫃前面。到了第七天,你們要繞城七圈,祭司要吹響號角。 5當你們聽到號角長鳴時,所有人都要高聲吶喊,城牆就會坍塌,眾人便可以直衝上去。」 6的兒子約書亞便召來祭司,對他們說:「你們抬起約櫃,派七位祭司拿著七個羊角號走在耶和華的約櫃前面。」 7他又對民眾說:「你們要前去繞著城牆走,軍隊要走在耶和華的約櫃前面。」

8約書亞吩咐完畢,七個祭司便在耶和華面前拿著羊角號邊走邊吹,耶和華的約櫃就跟在他們後面, 9軍隊走在吹號的祭司前面,殿後軍隊跟在約櫃後面。祭司一路上吹著號角。 10約書亞吩咐民眾:「我哪天叫你們吶喊,你們再吶喊。在此之前,不許作聲,一句話也不許說。」 11這樣,約書亞讓人抬著耶和華的約櫃繞城一圈,然後眾人各自回營過夜。

12第二天,約書亞一早起來,祭司又抬起耶和華的約櫃。 13七個祭司拿著七個羊角號走在耶和華的約櫃前面,一邊走一邊吹號。軍隊走在祭司前面,殿後軍隊跟在耶和華的約櫃後面,伴隨著持續不斷的號角聲。 14這一天他們又繞城一圈,然後各自回營。六天都是這樣。

15第七天黎明時分,他們起來照樣繞城,只是這一天他們繞城七次。 16繞到第七次,祭司吹響了號角,約書亞吩咐民眾說:「吶喊吧!因為耶和華已經將這城交給你們了。 17要把這座城和城裡所有的東西毀滅,作為獻給耶和華之物。只有妓女喇合和她家中所有的人可以活命,因為她曾把我們派去的探子隱藏起來。 18你們要小心,不可私拿任何應當毀滅的東西,免得你們自取滅亡,並使以色列全營遭受滅頂之災。 19所有金銀和銅鐵器皿都是耶和華的聖物,要放進耶和華的庫房。」 20於是,民眾吶喊,號角響起,當民眾伴隨著號角聲高聲吶喊時,城牆坍塌了。民眾便一擁而上,佔領了耶利哥城, 21用刀殺了城裡所有的男女老少、牛羊和驢。

22約書亞對那兩個探子說:「你們到那個妓女家裡,照著你們向她起過的誓,把她和她的家人都帶出來。」 23於是,那兩個年輕探子便進去,把喇合和她的父母、兄弟及所有的親人都帶出來,安置在以色列人的營外。 24以色列人燒毀全城和城內的一切,只把金銀和銅鐵器皿放在耶和華的庫房裡。 25約書亞因為妓女喇合把兩個派到耶利哥的探子隱藏起來,就饒了她和她一家人的性命。他們至今仍住在以色列人當中。

26之後,約書亞起誓說:

「重建耶利哥城的人必定在耶和華面前受咒詛,

他立地基的時候必死長子,

建城門的時候必喪幼子。」

27耶和華與約書亞同在,他的聲名傳遍整個地方。