Yoshua 18 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yoshua 18:1-28

Mgawanyo Wa Nchi Iliyobaki

118:1 Yos 19:51; 21:2; Amu 18:31; 21:12; 1Sam 1:3; 3:21; 4:3; 1Fal 14:2; Za 78:60; Yer 7:12; 26:6; 41:5; Kut 27:21; 40:2; Mdo 7:45Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao, 2lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.

318:3 Amu 18:9; Sef 3:16; Mt 20:6; Yn 6:27; Flp 3:13-14Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa? 418:4 Mik 2:5Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia. 518:5 Yos 15:1; 16:1-4Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini. 618:6 Law 16:8; Yos 14:2Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu. 718:7 Yos 13:33; 13:8Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”

8Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.” 9Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo. 1018:10 Hes 34:13; Yer 7:12; Hes 33:54; Yos 19:51; Mit 16:33Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.

Mgawo Kwa Benyamini

11Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.

1218:12 Yos 8:15; 7:2Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni. 1318:13 Mwa 28:19; Yos 12:9; Hes 32:3; Yos 16:5; Amu 1:23; Hes 18:20; Kum 10:9; Eze 44:28Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.

1418:14 Yos 10:10; 9:17; 1Nya 13:6Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.

1518:15 Yos 15:9Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa. 1618:16 Yos 17:15; 15:7-8; 2Fal 23:10; 2Nya 28:3; 33:6; Isa 30:33; Yer 19:2; Yos 15:8Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli. 1718:17 Yos 22:10; 15:6-7Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 1818:18 Yos 15:6; 11:2; 16:1Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba. 1918:19 Yos 15:6; Mwa 14:3Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.

2018:20 1Sam 9:1; Yos 21:4, 17Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki.

Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.

2118:21 Yos 6:26; 1Fal 16:34; Lk 10:30Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo:

Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi, 2218:22 Yos 15:6; 2Nya 13:4; Yos 16:1Beth-Araba, Semaraimu, Betheli, 2318:23 Kum 2:23; Amu 6:11, 24; 8:27, 32; 9:6; 1Sam 13:17Avimu, Para na Ofra, 2418:24 Yos 21:17; 1Sam 13:3, 16; 14:5; 1Fal 15:22; 2Fal 23:8; Isa 10:29; Amu 19:12-16; Ezr 2:26Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

2518:25 Yos 10:40; Amu 4:5; 19:13; 1Sam 2:11; 7:17; 25:1; Neh 11:33; 1Fal 15:17, 21; Neh 7:29Gibeoni, Rama na Beerothi, 2618:26 Yer 11:3; Yos 9:17; Ezr 2:25; Neh 7:29Mispa, Kefira, Moza, 27Rekemu, Irpeeli, Tarala, 2818:28 2Sam 21:14; Yos 15:8; 10:1; 15:57; 9:17; Eze 48:23; Mwa 46:21; Mdo 17:26Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake.

Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.

New International Version

Joshua 18:1-28

Division of the Rest of the Land

1The whole assembly of the Israelites gathered at Shiloh and set up the tent of meeting there. The country was brought under their control, 2but there were still seven Israelite tribes who had not yet received their inheritance.

3So Joshua said to the Israelites: “How long will you wait before you begin to take possession of the land that the Lord, the God of your ancestors, has given you? 4Appoint three men from each tribe. I will send them out to make a survey of the land and to write a description of it, according to the inheritance of each. Then they will return to me. 5You are to divide the land into seven parts. Judah is to remain in its territory on the south and the tribes of Joseph in their territory on the north. 6After you have written descriptions of the seven parts of the land, bring them here to me and I will cast lots for you in the presence of the Lord our God. 7The Levites, however, do not get a portion among you, because the priestly service of the Lord is their inheritance. And Gad, Reuben and the half-tribe of Manasseh have already received their inheritance on the east side of the Jordan. Moses the servant of the Lord gave it to them.”

8As the men started on their way to map out the land, Joshua instructed them, “Go and make a survey of the land and write a description of it. Then return to me, and I will cast lots for you here at Shiloh in the presence of the Lord.” 9So the men left and went through the land. They wrote its description on a scroll, town by town, in seven parts, and returned to Joshua in the camp at Shiloh. 10Joshua then cast lots for them in Shiloh in the presence of the Lord, and there he distributed the land to the Israelites according to their tribal divisions.

Allotment for Benjamin

11The first lot came up for the tribe of Benjamin according to its clans. Their allotted territory lay between the tribes of Judah and Joseph:

12On the north side their boundary began at the Jordan, passed the northern slope of Jericho and headed west into the hill country, coming out at the wilderness of Beth Aven. 13From there it crossed to the south slope of Luz (that is, Bethel) and went down to Ataroth Addar on the hill south of Lower Beth Horon.

14From the hill facing Beth Horon on the south the boundary turned south along the western side and came out at Kiriath Baal (that is, Kiriath Jearim), a town of the people of Judah. This was the western side.

15The southern side began at the outskirts of Kiriath Jearim on the west, and the boundary came out at the spring of the waters of Nephtoah. 16The boundary went down to the foot of the hill facing the Valley of Ben Hinnom, north of the Valley of Rephaim. It continued down the Hinnom Valley along the southern slope of the Jebusite city and so to En Rogel. 17It then curved north, went to En Shemesh, continued to Geliloth, which faces the Pass of Adummim, and ran down to the Stone of Bohan son of Reuben. 18It continued to the northern slope of Beth Arabah18:18 Septuagint; Hebrew slope facing the Arabah and on down into the Arabah. 19It then went to the northern slope of Beth Hoglah and came out at the northern bay of the Dead Sea, at the mouth of the Jordan in the south. This was the southern boundary.

20The Jordan formed the boundary on the eastern side.

These were the boundaries that marked out the inheritance of the clans of Benjamin on all sides.

21The tribe of Benjamin, according to its clans, had the following towns:

Jericho, Beth Hoglah, Emek Keziz, 22Beth Arabah, Zemaraim, Bethel, 23Avvim, Parah, Ophrah, 24Kephar Ammoni, Ophni and Geba—twelve towns and their villages.

25Gibeon, Ramah, Beeroth, 26Mizpah, Kephirah, Mozah, 27Rekem, Irpeel, Taralah, 28Zelah, Haeleph, the Jebusite city (that is, Jerusalem), Gibeah and Kiriath—fourteen towns and their villages.

This was the inheritance of Benjamin for its clans.