Yona 1 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yona 1:1-17

Yona Anamkimbia Bwana

11:1 Mt 16:4; 12:39-41; 2Fal 14:25; Lk 11:29-32Neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amitai: 21:2 Mwa 10:11; 18:20; Yon 3:3; Nah 2:8; Mt 12:41; Ezr 9:6; Yak 5:4“Nenda katika mji mkubwa wa Ninawi ukahubiri juu yake, kwa sababu uovu wake umekuja juu mbele zangu.”

31:3 Za 139:7; Yos 19:46; Mdo 9:36-43; Mwa 4:16; 10:4; Kut 4:13; Isa 23:1; Yer 20:9Lakini Yona alimkimbia Bwana na kuelekea Tarshishi. Alishuka mpaka Yafa, ambapo alikuta meli iliyokuwa imepangwa kuelekea bandari ile. Baada ya kulipa nauli, akapanda melini na kuelekea Tarshishi ili kumkimbia Bwana. 41:4 Za 107:23-26Ndipo Bwana akatuma upepo mkali baharini, nayo dhoruba kali sana ikavuma hata meli ikawa hatarini kuvunjika. 51:5 Mdo 27:18-19Mabaharia wote waliogopa na kila mmoja akamlilia mungu wake mwenyewe. Nao wakatupa mizigo baharini ili meli ipungue uzito.

Lakini Yona alikuwa ameteremkia chumba cha ndani ya meli, mahali ambapo alilala na kupatwa na usingizi mzito. 61:6 Yon 3:8; Mt 8:25; Za 78:34; 107:28Nahodha akamwendea na kusema, “Wewe unawezaje kulala? Amka ukamwite mungu wako! Huenda akatuangalia, tusiangamie.”

71:7 Yos 7:10-18; Hes 32:23; Mit 16:33; Mdo 1:26; 1Sam 10:20; 14:43Kisha mabaharia wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tupige kura tumtafute anayehusika na maafa haya.” Wakapiga kura, kura ikamwangukia Yona.

81:8 Yos 7:19Kwa hiyo walimuuliza, “Tuambie, ni nani anayehusika kwa kutuletea tatizo hili lote? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Nchi yako ni ipi? Wewe ni kutoka taifa lipi?”

91:9 Dan 2:18; Mdo 17:24; Za 146:6; 96:9; Neh 9:6Akajibu, “Mimi ni Mwebrania, nami namwabudu Bwana, Mungu wa Mbinguni, aliyeumba bahari na nchi kavu.”

10Hili liliwaogopesha nao wakamuuliza,

“Umefanya nini?” (Walijua alikuwa anamkimbia Bwana, kwa sababu alishawaambia hivyo.)

11Bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Kwa hiyo walimuuliza, “Tukutendee nini ili kufanya bahari itulie kwa ajili yetu?”

121:12 Mhu 9:18; 2Sam 24:17; 1Nya 21:17Akawajibu, “Niinueni mnitupe baharini, nayo itakuwa shwari. Ninajua mawimbi haya makubwa yamewatokea kwa ajili ya kosa langu.”

131:13 Mit 21:30Badala yake, wale watu walijitahidi kupiga makasia wawezavyo ili wapate kurudi pwani. Lakini hawakuweza, kwa kuwa bahari ilizidi kuchafuka kuliko mwanzo. 141:14 Kum 21:8; Za 115:3; Dan 4:35Ndipo wakamlilia Bwana, “Ee Bwana, tafadhali usituue kwa kuondoa uhai wa mtu huyu. Usituhesabie hatia kwa kuutoa uhai wa mtu asiyekuwa na hatia, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umefanya kama ilivyokupendeza.” 151:15 Za 107:29; Lk 8:24Kisha walimchukua Yona, wakamtupa baharini nayo bahari iliyokuwa imechafuka ikatulia. 161:16 Mk 4:41; Hes 30:2; Za 66:13-14Katika jambo hili watu wakamwogopa Bwana sana, wakamtolea Bwana dhabihu na kumwekea nadhiri.

171:17 Mt 12:40; 16:4; Lk 11:30; Yn 4:6-7Lakini Bwana akamwandaa nyangumi1:17 Yaani samaki mkubwa sana. kummeza Yona, naye Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu, usiku na mchana.

New International Version

Jonah 1:1-17

Jonah Flees From the Lord

1The word of the Lord came to Jonah son of Amittai: 2“Go to the great city of Nineveh and preach against it, because its wickedness has come up before me.”

3But Jonah ran away from the Lord and headed for Tarshish. He went down to Joppa, where he found a ship bound for that port. After paying the fare, he went aboard and sailed for Tarshish to flee from the Lord.

4Then the Lord sent a great wind on the sea, and such a violent storm arose that the ship threatened to break up. 5All the sailors were afraid and each cried out to his own god. And they threw the cargo into the sea to lighten the ship.

But Jonah had gone below deck, where he lay down and fell into a deep sleep. 6The captain went to him and said, “How can you sleep? Get up and call on your god! Maybe he will take notice of us so that we will not perish.”

7Then the sailors said to each other, “Come, let us cast lots to find out who is responsible for this calamity.” They cast lots and the lot fell on Jonah. 8So they asked him, “Tell us, who is responsible for making all this trouble for us? What kind of work do you do? Where do you come from? What is your country? From what people are you?”

9He answered, “I am a Hebrew and I worship the Lord, the God of heaven, who made the sea and the dry land.”

10This terrified them and they asked, “What have you done?” (They knew he was running away from the Lord, because he had already told them so.)

11The sea was getting rougher and rougher. So they asked him, “What should we do to you to make the sea calm down for us?”

12“Pick me up and throw me into the sea,” he replied, “and it will become calm. I know that it is my fault that this great storm has come upon you.”

13Instead, the men did their best to row back to land. But they could not, for the sea grew even wilder than before. 14Then they cried out to the Lord, “Please, Lord, do not let us die for taking this man’s life. Do not hold us accountable for killing an innocent man, for you, Lord, have done as you pleased.” 15Then they took Jonah and threw him overboard, and the raging sea grew calm. 16At this the men greatly feared the Lord, and they offered a sacrifice to the Lord and made vows to him.

Jonah’s Prayer

17Now the Lord provided a huge fish to swallow Jonah, and Jonah was in the belly of the fish three days and three nights.