Yohana 16 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yohana 16:1-33

116:1 Yn 15:18-27; Mt 11:16“Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani. 216:2 Yn 12:42; Isa 66:5; Ufu 6:9Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu. 316:3 Yn 17:25; 1Yn 3:1Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi. 416:4 Yn 14:29Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.

Kazi Ya Roho Mtakatifu

516:5 Yn 16:10, 17, 28; 7:33; 13:36; 14:5“Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’ 616:6 Yn 6:22; 14:1Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni. 716:7 Yn 14:16, 26; 15:26Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu. 816:8 1Kor 14:24; Ebr 4:12Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu. 916:9 Yn 15:22Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi, 1016:10 Rum 1:17; 1Pet 3:18kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena, 1116:11 Yn 12:31kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.

1216:12 1Kor 3:2“Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa. 1316:13 Yn 14:17; Za 25:5Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo. 14Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi. 1516:15 Yn 17:10Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.

1616:16 Yn 7:33; 16:22; 14:18-24“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”

Huzuni Itageuka Kuwa Furaha

1716:17 Yn 16:16; 16:5Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?” 18Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”

19Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? 2016:20 Mk 16:10; Yn 20:20Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha. 2116:21 Mik 4:9; 1The 5:3Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni. 2216:22 Isa 60:14; Lk 24:41, 52; Yn 14:1, 27; Mdo 2:46; 13:52; 1Pet 1:8Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye. 2316:23 Mt 7:7; Yn 15:16Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa. 2416:24 Yn 3:29; 15:11Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.

Amani Kwa Wanafunzi

2516:25 Yn 10:6“Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba. 2616:26 Yn 16:23, 24Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu, 2716:27 Yn 14:21, 23kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu. 2816:28 Yn 5:10, 17; 13:3Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”

2916:29 Yn 16:25Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo. 3016:30 1Fal 17:24; Yn 16:27; 13:3; 2:25Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”

31Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini? 3216:32 Yn 16:2, 25; Mt 26:31; 26:56; Yn 8:16, 29Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami. 3316:33 Yn 14:27; 15:18-21; 1Yn 5:4; Ufu 21:7Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”

New International Version

John 16:1-33

1“All this I have told you so that you will not fall away. 2They will put you out of the synagogue; in fact, the time is coming when anyone who kills you will think they are offering a service to God. 3They will do such things because they have not known the Father or me. 4I have told you this, so that when their time comes you will remember that I warned you about them. I did not tell you this from the beginning because I was with you, 5but now I am going to him who sent me. None of you asks me, ‘Where are you going?’ 6Rather, you are filled with grief because I have said these things. 7But very truly I tell you, it is for your good that I am going away. Unless I go away, the Advocate will not come to you; but if I go, I will send him to you. 8When he comes, he will prove the world to be in the wrong about sin and righteousness and judgment: 9about sin, because people do not believe in me; 10about righteousness, because I am going to the Father, where you can see me no longer; 11and about judgment, because the prince of this world now stands condemned.

12“I have much more to say to you, more than you can now bear. 13But when he, the Spirit of truth, comes, he will guide you into all the truth. He will not speak on his own; he will speak only what he hears, and he will tell you what is yet to come. 14He will glorify me because it is from me that he will receive what he will make known to you. 15All that belongs to the Father is mine. That is why I said the Spirit will receive from me what he will make known to you.”

The Disciples’ Grief Will Turn to Joy

16Jesus went on to say, “In a little while you will see me no more, and then after a little while you will see me.”

17At this, some of his disciples said to one another, “What does he mean by saying, ‘In a little while you will see me no more, and then after a little while you will see me,’ and ‘Because I am going to the Father’?” 18They kept asking, “What does he mean by ‘a little while’? We don’t understand what he is saying.”

19Jesus saw that they wanted to ask him about this, so he said to them, “Are you asking one another what I meant when I said, ‘In a little while you will see me no more, and then after a little while you will see me’? 20Very truly I tell you, you will weep and mourn while the world rejoices. You will grieve, but your grief will turn to joy. 21A woman giving birth to a child has pain because her time has come; but when her baby is born she forgets the anguish because of her joy that a child is born into the world. 22So with you: Now is your time of grief, but I will see you again and you will rejoice, and no one will take away your joy. 23In that day you will no longer ask me anything. Very truly I tell you, my Father will give you whatever you ask in my name. 24Until now you have not asked for anything in my name. Ask and you will receive, and your joy will be complete.

25“Though I have been speaking figuratively, a time is coming when I will no longer use this kind of language but will tell you plainly about my Father. 26In that day you will ask in my name. I am not saying that I will ask the Father on your behalf. 27No, the Father himself loves you because you have loved me and have believed that I came from God. 28I came from the Father and entered the world; now I am leaving the world and going back to the Father.”

29Then Jesus’ disciples said, “Now you are speaking clearly and without figures of speech. 30Now we can see that you know all things and that you do not even need to have anyone ask you questions. This makes us believe that you came from God.”

31“Do you now believe?” Jesus replied. 32“A time is coming and in fact has come when you will be scattered, each to your own home. You will leave me all alone. Yet I am not alone, for my Father is with me.

33“I have told you these things, so that in me you may have peace. In this world you will have trouble. But take heart! I have overcome the world.”