Yohana 16 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Yohana 16:1-33

116:1 Yn 15:18-27; Mt 11:16“Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani. 216:2 Yn 12:42; Isa 66:5; Ufu 6:9Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu. 316:3 Yn 17:25; 1Yn 3:1Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi. 416:4 Yn 14:29Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.

Kazi Ya Roho Mtakatifu

516:5 Yn 16:10, 17, 28; 7:33; 13:36; 14:5“Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’ 616:6 Yn 6:22; 14:1Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni. 716:7 Yn 14:16, 26; 15:26Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu. 816:8 1Kor 14:24; Ebr 4:12Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu. 916:9 Yn 15:22Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi, 1016:10 Rum 1:17; 1Pet 3:18kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena, 1116:11 Yn 12:31kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.

1216:12 1Kor 3:2“Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa. 1316:13 Yn 14:17; Za 25:5Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo. 14Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi. 1516:15 Yn 17:10Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.

1616:16 Yn 7:33; 16:22; 14:18-24“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”

Huzuni Itageuka Kuwa Furaha

1716:17 Yn 16:16; 16:5Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?” 18Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”

19Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? 2016:20 Mk 16:10; Yn 20:20Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha. 2116:21 Mik 4:9; 1The 5:3Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni. 2216:22 Isa 60:14; Lk 24:41, 52; Yn 14:1, 27; Mdo 2:46; 13:52; 1Pet 1:8Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye. 2316:23 Mt 7:7; Yn 15:16Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa. 2416:24 Yn 3:29; 15:11Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.

Amani Kwa Wanafunzi

2516:25 Yn 10:6“Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba. 2616:26 Yn 16:23, 24Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu, 2716:27 Yn 14:21, 23kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu. 2816:28 Yn 5:10, 17; 13:3Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”

2916:29 Yn 16:25Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo. 3016:30 1Fal 17:24; Yn 16:27; 13:3; 2:25Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”

31Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini? 3216:32 Yn 16:2, 25; Mt 26:31; 26:56; Yn 8:16, 29Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami. 3316:33 Yn 14:27; 15:18-21; 1Yn 5:4; Ufu 21:7Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”