Yohana 13 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 13:1-38

Yesu Awanawisha Wanafunzi Wake Miguu

113:1 Yn 11:55; 12:33; 16:28Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.

213:2 Lk 22:3Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu. 313:3 Mt 28:18; Yn 8:42; 17:8Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu, 413:4 Mt 11:29; 20:29; Lk 12:37hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni. 513:5 Lk 7:44Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.

613:6 1Pet 5:5Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”

713:7 Yn 13:12Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”

813:8 Yn 3:5; 1Kor 6:11; Efe 5:26; Tit 3:5; Ebr 10:22Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.”

Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.”

9Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”

1013:10 Yn 15:3Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.” 1113:11 Mt 10:4Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.

12Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia? 1313:13 Mt 26:18; Yn 11:28; Mdo 10:36Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo. 1413:14 1Pet 5:5Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi. 1513:15 Mt 11:29; 1Tim 4:12Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi. 1613:16 Mt 10:24; Lk 6:40Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma. 1713:17 Lk 11:28; 1:25Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.

1813:18 Za 41:9; Mt 26:23“Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’

1913:19 Yn 14:29; 16:4; 4:26; 8:24“Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye. 2013:20 Mt 10:40; Lk 10:16Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”

Yesu Anatabiri Kusalitiwa Kwake

(Mathayo 26:20-25; Marko 14:17-21; Luka 22:21-23)

2113:21 Yn 12:27; Mt 26:21Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”

22Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani. 2313:23 Yn 20:2; 21:7, 20Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu. 24Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”

2513:25 Mt 26:22; Yn 21:20Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”

2613:26 Mt 10:4Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni. 2713:27 Lk 22:3Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia.

Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.” 28Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo. 2913:29 Yn 12:6Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote. 3013:30 Lk 22:53Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.

Yesu Atabiri Petro Kumkana

(Mathayo 26:31-35; Marko 14:27-31; Luka 22:31-34)

3113:31 Yn 7:39; 12:23; 17:4; 1Pet 4:11Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake. 3213:32 Yn 17:1Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.

3313:33 Yn 7:33, 34“Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.

3413:34 1Yn 2:7-11; 3:11; Law 19:18; 1The 4:9; Efe 5:2; 1Yn 4:10, 11; 2:14“Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane. 3513:35 Yn 3:14; 4:20Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”

3613:36 Yn 16:5; 14:2; 21:18, 19; 2Pet 1:4Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?”

Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”

3713:37 Mt 26:33, 34, 35; Mk 14:29, 30, 31; Lk 22:33, 34Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”

3813:38 Yn 18:27Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”

Священное Писание

Иохан 13:1-38

Иса Масих омывает ноги ученикам

1Приближался праздник Освобождения. Иса знал, что настал час Ему покинуть этот мир и вернуться к Отцу. Полюбив Своих, находящихся в этом мире, Он полюбил их до конца.

2Во время ужина, когда дьявол уже побудил Иуду Искариота, сына Шимона, предать Ису, 3Иса, зная, что Отец отдал всё в руки Его и что Он пришёл от Всевышнего и теперь возвращается к Всевышнему, 4встал из-за стола, снял с Себя верхнюю одежду и опоясался полотенцем. 5Потом Он налил воды в таз и начал мыть Своим ученикам ноги и вытирать их полотенцем, которым был опоясан. 6Когда Он подошёл к Шимону Петиру, тот сказал Ему:

– Повелитель, Тебе ли мыть мне ноги?!

7Иса сказал ему:

– Сейчас ты не понимаешь, что Я делаю, но позже поймёшь.

8– Ты никогда не вымоешь моих ног! – возразил Петир.

Иса ответил:

– Если Я не омою тебя, то у тебя нет со Мной ничего общего.

9Шимон Петир ответил:

– Тогда, Повелитель, омой мне не только ноги, но и руки и голову!

10Иса ответил:

– Омытого нет нужды мыть, разве только ноги, так как всё его тело чисто. Вы ведь чисты, хотя и не все.

11Он знал, кто предаст Его, и поэтому сказал, что не все чисты.

12Окончив мыть ученикам ноги, Иса снова оделся и, возвратившись, возлёг на Своём месте за столом.

– Вы понимаете, что Я сделал для вас? – спросил Он их. – 13Вот вы называете Меня Учителем и Повелителем, и правильно, потому что Я и есть Учитель и Повелитель. 14Поэтому если Я, ваш Повелитель и Учитель, омыл вам ноги, то вы тоже должны мыть ноги друг другу. 15Я показал вам пример, чтобы и вы делали то же, что Я сделал вам. 16Говорю вам истину: раб не больше своего господина, и посланный не больше пославшего его. 17Если вы это знаете и так поступаете, то вы благословенны.

18– Я не говорю о всех вас. Тех, кого Я избрал, Я знаю, но слова Писания: «Тот, кто ест Мой хлеб, пошёл против Меня»13:18 Заб. 40:10. – должны исполниться. 19Говорю вам обо всём заранее, чтобы, когда это произойдёт, вы поверили, что Я и есть Тот, за Кого Себя выдаю13:19 Букв.: «Я есть». Часто в Писании, когда Всевышний говорил о Себе, Он употреблял это же самое выражение (см., напр., Исх. 3:14; Втор. 32:39; Ис. 41:4; 43:10-13 и сноски на эти стихи). Здесь виден явный намёк Исы на то, Кем Он в действительности является.. 20Говорю вам истину: кто принимает посланного Мною, тот принимает и Меня, и кто принимает Меня, тот принимает и Пославшего Меня.

Последний ужин с учениками

(Мат. 26:20-25; Мк. 14:17-21; Лк. 22:21-23)

21Сказав это, Иса произнёс в большом волнении:

– Говорю вам истину: один из вас предаст Меня.

22Ученики стали растерянно переглядываться между собой, недоумевая, кого Он имеет в виду. 23Один из учеников, которого Иса любил13:23 То есть Иохан, один из двенадцати посланников Исы и автор этой книги (см. 21:20-24)., возлежал у стола рядом с Ним. 24Шимон Петир показал ему жестом:

– Спроси, кого Он имеет в виду?

25Откинувшись назад к Исе, ученик спросил:

– Повелитель, кто это?

26Иса ответил:

– Тот, кому Я подам этот кусок хлеба, обмакнув его в блюдо.

И обмакнув кусок, Иса протянул его Иуде Искариоту, сыну Шимона. 27Как только Иуда взял хлеб, в него вошёл сатана.

– Делай быстро то, что собираешься делать, – сказал ему Иса.

28Никто из возлежавших за столом не понял, зачем Иса сказал ему это. 29Иуда отвечал за ящик с общими деньгами, и некоторые подумали, что Иса попросил его купить необходимое к празднику или же раздать часть денег бедным. 30Взяв хлеб, Иуда сразу же вышел. Была ночь.

Повеление о любви

31Когда Иуда вышел, Иса сказал:

– Теперь Ниспосланный как Человек прославлен, а в Нём прославлен Всевышний. 32Если Всевышний прославлен в Нём, то Всевышний прославит в Себе и Его и сделает это незамедлительно. 33Дети Мои, недолго Мне ещё быть с вами. Вы будете искать Меня, и как Я говорил предводителям иудеев, так говорю и вам: туда, куда Я иду, вы не можете прийти.

34Я даю вам новое повеление: любите друг друга. Как Я вас полюбил, так и вы любите друг друга. 35Все узнают, что вы Мои ученики, если вы будете любить друг друга!

Предсказание об отречении Петира

(Мат. 26:33-35; Мк. 14:29-31; Лк. 22:33-34)

36Шимон Петир спросил Его:

– Повелитель, куда Ты идёшь?

Иса ответил:

– Туда, куда Я иду, ты сейчас со Мной пойти не сможешь, но позже ты пойдёшь.

37Петир спросил:

– Повелитель, почему я не могу идти за Тобой сейчас? Да я готов даже жизнь отдать за Тебя!

38Иса тогда сказал:

– Ты жизнь свою за Меня отдашь? Говорю тебе истину: не успеет и петух пропеть, как ты трижды отречёшься от Меня.