Yoeli 3 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoeli 3:1-21

Mataifa Yahukumiwa

13:1 Kum 30:3; Yer 16:15; 40:5; Eze 3:20; 38:8“Katika siku hizo na wakati huo,

nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,

23:2 Zek 14:2; Isa 13:9; 2Nya 20:26; Isa 66:16; Yer 2:35; Sef 3:8; Mwa 11:4; Law 26:33nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta

katika Bonde la Yehoshafati3:2 Yehoshafati maana yake Bwana huhukumu.

Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao

kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli,

kwa kuwa waliwatawanya watu wangu

miongoni mwa mataifa

na kuigawa nchi yangu.

33:3 Oba 1:11; Amo 2:6; Ay 6:27; Eze 24:6Wanawapigia kura watu wangu

na kuwauza wavulana ili kupata makahaba;

waliwauza wasichana

ili wapate kunywa mvinyo.

43:4 Mwa 10:15; Mt 11:21; Yak 2:13; Lk 18:7; Amo 1:6-9; Isa 14:29-31; 34:8; Za 87:4; Eze 25:15-17“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda. 53:5 1Fal 15:18; 2Nya 21:16-17Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu. 63:6 Eze 27:13; Zek 9:13Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.

73:7 Isa 43:5-6; 66:6; Yer 23:8“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya. 83:8 Eze 23:42; Isa 14:2; 60:14; Mwa 10:7; Yer 30:16; 2Nya 9:1Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.

93:9 Isa 8:9; Yer 46:4Tangazeni hili miongoni mwa mataifa:

Jiandaeni kwa vita!

Amsha askari!

Wanaume wote wapiganaji

wasogee karibu na kushambulia.

103:10 Zek 12:8; Isa 2:4; Mik 4:3; Hes 25:7Majembe yenu yafueni yawe panga

na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki.

Aliye dhaifu na aseme,

“Mimi nina nguvu!”

113:11 Eze 38:15-16; Sef 3:8; Isa 13:3Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote,

kusanyikeni huko.

Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!

123:12 Za 96:13; 82:1; 2Nya 20:26; Isa 2:4“Mataifa na yaamshwe;

na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati,

kwa kuwa nitaketi mahali pale

kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.

133:13 Isa 17:5; Ufu 14:15-20; Amu 6:11; Mt 13:39; Mk 4:29; Yer 51:33; Hos 6:11Tia mundu,

kwa kuwa mavuno yamekomaa.

Njooni, mkanyage zabibu,

kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa

na mapipa yanafurika:

kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”

143:14 Isa 2:4; 13:4; 34:2-8; Sef 1:7; Yoe 1:15; Eze 36:5Umati mkubwa, umati mkubwa

katika bonde la uamuzi!

Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu

katika bonde la uamuzi.

15Jua na mwezi vitatiwa giza,

na nyota hazitatoa mwanga wake tena.

163:16 Amu 5:4; Isa 14:16; 25:4; 42:13; 2Sam 22:3; Zek 9:12; Eze 38:19Bwana atanguruma kutoka Sayuni

na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu;

dunia na mbingu vitatikisika.

Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake,

ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.

Baraka Kwa Watu Wa Mungu

173:17 Yoe 2:27; Za 74:2; Isa 4:3; 35:8; Ufu 21:27; Nah 1:15; Kut 6:7; Yer 31:40; Eze 44:9“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu,

nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.

Yerusalemu utakuwa mtakatifu;

kamwe wageni hawatavamia tena.

183:18 Kut 3:8; Eze 47:1; Zek 13:1; Wim 5:1; Isa 25:6; 30:25; 35:6; 44:3; Ufu 22:1-2; Hes 25:1; Yoe 2:24“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya,

na vilima vitatiririka maziwa;

mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji.

Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana

na kunywesha Bonde la Shitimu.3:18 Au: Bonde la Migunga.

193:19 Yer 51:35; Oba 1:10; Isa 11:14; 34:11Lakini Misri itakuwa ukiwa,

Edomu itakuwa jangwa tupu,

kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda,

ambao katika nchi yao

walimwaga damu isiyo na hatia.

203:20 Ezr 9:12; Amo 9:15Yuda itakaliwa na watu milele

na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.

213:21 Eze 36:25; 48:35; Isa 1:15; 59:20; Za 74:2; Zek 8:3Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe,

nitasamehe.”

Bwana anakaa Sayuni!

Het Boek

Joel 3:1-21

1Want zie, in die dagen en in die tijd, Waarin Ik het lot van Juda, En het lot van Jerusalem ten beste zal keren, 2Drijf Ik alle heidenen te hoop; In het Dal van Josafat zal Ik ze voeren, En daar oordeel over hen houden! Omdat ze mijn volk, en Israël mijn erfdeel, Onder de heidenen hebben verstrooid; Mijn land onder elkander verdeeld, 3En over mijn volk het lot geworpen; Den knaap hebben verruild voor een deerne, Het meisje verkocht voor wijn, om te brassen. 4Wat wilt ge van Mij, Tyrus en Sidon, En gij allen, Filistijnse gewesten? Wilt ge vergelding aan Mij oefenen, Of u wreken op Mij? Bliksemsnel stort Ik uw wraak Op uw eigen hoofd terug! 5Ge hebt mijn zilver geroofd en mijn goud, Mijn kostbaarste schatten naar uw paleizen gesleept; 6De zonen van Juda en Jerusalem Aan de Grieken verkocht, Om ze weg te voeren Ver van hun land. 7Zie, Ik roep ze op van de plaats, waarheen gij ze verkocht, Maar uw gedrag stort Ik terug op uw eigen hoofd: 8Aan de kinderen van Juda verkoop Ik uw zonen en dochters; Zij zullen ze weer aan de Sjabeërs verkopen Voor een ver verwijderd volk: Waarachtig, Jahweh heeft het gezegd! 9Kondigt het onder de heidenen af: Maakt u gereed voor de heilige strijd; Werft sterke mannen aan! Oorlogsmannen, treedt aan; rukt allen vooruit; 10Smeedt uw ploegen om tot zwaarden, Uw sikkels tot lansen! Zelfs de zwakke moet zeggen: Ik ben een held! 11Vooruit, gij allen, u gehaast, Omliggende volken, Sluit de rangen aaneen: Jahweh, breng daar uw strijders bijeen! 12Op heidenen; op naar het Dal van Josafat; Want daar zit Ik ten oordeel over alle omliggende volken! 13Slaat de sikkel erin, want de oogst is rijp, Gaat treden, want de perskuip is vol; De bakken vloeien over, Want hun boosheid is groot! 14Drommen, drommen in het Dal der Beslissing; Want Jahweh’s dag is nabij in het Dal der Beslissing! 15Zon en maan verduisteren, De sterren trekken haar glans terug; 16Jahweh buldert uit Sion, dondert uit Jerusalem: Hemel en aarde beven ervan! Maar voor zijn volk is Jahweh een toevlucht, Een burcht voor Israëls zonen. 17Dan zult ge weten, dat Ik, Jahweh, uw God ben, Dat Ik woon op de Sion, mijn heilige berg; Dan zal Jerusalem heilig wezen, Geen vreemdeling komt er meer in! 18Op die dag druipen de bergen van wijn, Vloeien de heuvelen van melk, En al de beken van Juda Stromen over van water. Een bron zal uit het huis van Jahweh ontspringen, En zelfs het Sjittim-dal besproeien! 19Egypte zal een steppe worden, Edom een dorre woestijn; Omdat ze Juda’s kinderen hebben mishandeld, Onschuldig bloed in hun land hebben vergoten. 20Maar Juda zal in eeuwigheid blijven bestaan, Jerusalem van geslacht tot geslacht; 21hun bloed laat Ik niet ongewroken: Ik, Jahweh, blijf wonen op Sion!