Yoeli 2 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Yoeli 2:1-32

Jeshi La Nzige

12:1 Hos 10:2, 7; Kut 15:17; Oba 1:15; Sef 1:14-16; Eze 12:23Pigeni tarumbeta katika Sayuni;

pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu.

Wote waishio katika nchi na watetemeke,

kwa kuwa siku ya Bwana inakuja. Iko karibu,

22:2 Ay 9:7; Isa 8:22; 13:10; Amo 5:18; Kut 10:14; Dan 9:12; Mt 24:21; Eze 34:12siku ya giza na huzuni,

siku ya mawingu na utusitusi.

Kama mapambazuko yasambaavyo

toka upande huu wa milima

hata upande mwingine

jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja.

Jambo kama hili halijakuwepo tangu zamani

wala halitakuwepo tena kamwe

kwa vizazi vijavyo.

32:3 Za 97:3; 105:34-35; Kut 10:12-15; Isa 14:17; Zek 7:14; Isa 1:31Mbele yao moto unateketeza,

nyuma yao miali ya moto

inawaka kwa nguvu.

Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni,

nyuma yao ni jangwa lisilofaa:

hakuna kitu kinachowaepuka.

4Wanaonekana kama farasi;

wanakwenda mbio

kama askari wapanda farasi.

52:5 Ufu 9:9; Isa 5:24; 30:30Wanatoa sauti kama magari ya vita,

wanaporukaruka juu ya vilele vya milima,

kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua,

kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.

62:6 Yer 8:21; Isa 13Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu;

kila uso unabadilika rangi.

72:7 Isa 5:27; Mit 30:27; Ay 16:14Wanashambulia kama wapiganaji wa vita;

wanapanda kuta kama askari.

Wote wanatembea katika safu,

hawapotoshi safu zao.

8Hakuna anayemsukuma mwenzake;

kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja.

Wanapita katika vizuizi

bila kuharibu safu zao.

92:9 Yer 9:21; Kut 10:6Wanaenda kasi kuingia mjini;

wanakimbia ukutani.

Wanaingia ndani ya nyumba;

kwa kuingilia madirishani kama wevi.

102:10 Isa 5:30; 13:10; Za 18:7; 102:26; Ufu 9:2; Ay 9:7; Eze 38:19Mbele yao dunia inatikisika,

anga linatetemeka,

jua na mwezi vinatiwa giza,

na nyota hazitoi mwanga wake tena.

112:11 Isa 2:12; Hes 24:23; Ufu 6:17; 18:8; Sef 2:11; Eze 30:3; Yoe 1:15; Yer 50:34; Mal 3:2; Za 29:3Bwana anatoa mshindo wa ngurumo

mbele ya jeshi lake;

majeshi yake hayana idadi,

ni wenye nguvu nyingi

wale ambao hutii agizo lake.

Siku ya Bwana ni kuu,

ni ya kutisha.

Ni nani anayeweza kuistahimili?

Rarueni Mioyo Yenu

122:12 Kum 4:30; Hos 12:6; Eze 33:11; 1Sam 7:3“Hata sasa,” asema Bwana,

“nirudieni kwa mioyo yenu yote,

kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”

132:13 Za 34:18; 51:17; 86:5; Mwa 37:29; Hes 14:6; Kut 34:6; Yon 4:2; Isa 57:15; 2Fal 22:19; Mt 5:3-4; Ay 1:20Rarueni mioyo yenu

na siyo mavazi yenu.

Mrudieni Bwana, Mungu wenu,

kwa maana yeye ndiye mwenye neema

na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo,

huona huruma, hujizuia kuleta maafa.

142:14 Yer 26:3; 31:14; Yn 3:9; Sef 2:3; Isa 65:8; Zek 8:13; Yos 14:12; Amo 5:15; Hag 2:19; Mal 3:10Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma

na kuacha baraka nyuma yake:

sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji

kwa ajili ya Bwana Mungu wenu.

152:15 2Nya 20:3; Hes 10:2-3; Yer 36:9Pigeni tarumbeta katika Sayuni,

tangazeni saumu takatifu,

liiteni kusanyiko takatifu.

162:16 Kut 19:10; 2Nya 20:13; 1Kor 7:5; Za 19Wakusanyeni watu,

wekeni wakfu kusanyiko;

waleteni pamoja wazee,

wakusanyeni watoto,

wale wanyonyao maziwa.

Bwana arusi na atoke chumbani mwake

na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.

172:17 Eze 8:16; Mt 23:35; Kum 9:26-29; Ay 17:6; Za 42:3; Kut 32:11; Isa 37:20; Yoe 1:13; Isa 22:12Makuhani, ambao wanahudumu mbele za Bwana,

na walie katikati ya ukumbi

wa Hekalu na madhabahu.

Waseme, “Wahurumie watu wako, Ee Bwana.

Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa,

neno la dhihaka kati ya mataifa.

Kwa nini wasemezane miongoni mwao,

‘Yuko wapi Mungu wao?’ ”

Jibu La Bwana

182:18 Isa 26:11; 42:13; Zek 8:2; 1:14; Kum 32:36; Za 103:13; 72:13Kisha Bwana atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake

na kuwa na huruma juu ya watu wake.

192:19 Yer 31:12; Eze 34:29; Za 4:7; Law 26:5Bwana atawajibu:

“Ninawapelekea nafaka,

mvinyo mpya na mafuta,

vya kuwatosha ninyi

hadi mridhike kabisa;

kamwe sitawafanya tena

kitu cha kudharauliwa na mataifa.

202:20 Yer 1:14-15; Zek 14:8; Kum 11:24; Kut 10:19; Isa 34:3“Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi,

nikilisukuma ndani ya jangwa,

askari wa safu za mbele wakienda

ndani ya bahari ya mashariki

na wale wa safu za nyuma

katika bahari ya magharibi.

Uvundo wake utapaa juu;

harufu yake itapanda juu.”

Hakika ametenda mambo makubwa.

212:21 Sef 3:16-17; Isa 25:1; 29:22; 54:4; 1Yn 4:18Usiogope, ee nchi;

furahi na kushangilia.

Hakika Bwana ametenda mambo makubwa.

222:22 Yoe 1:18-20; Zek 8:12; Za 65:12; Hes 16:14; 1Fal 4:25Msiogope, enyi wanyama pori,

kwa kuwa mbuga za malisho yenu

zinarudia ubichi.

Miti nayo inazaa matunda,

mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.

232:23 Hab 3:18; Yak 5:7; Za 28:7; 33:21; Law 26:4Furahini, enyi watu wa Sayuni,

shangilieni katika Bwana Mungu wenu,

kwa kuwa amewapa mvua za vuli

kwa kipimo cha haki.

Anawapelekea mvua nyingi,

mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.

242:24 Law 26:10; Mal 3:10; Mit 3:10; Amo 9:13; Yoe 3:18Sakafu za kupuria zitajaa nafaka,

mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.

252:25 Kut 14:10; Amo 4:9“Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige:

parare, madumadu na tunutu,

jeshi langu kubwa ambalo

nililituma katikati yenu.

262:26 Law 23:40; 26:5; Isa 25:1; 29:22; 62:9; Za 126:3; Mik 6:14Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe,

na mtalisifu jina la Bwana Mungu wenu,

ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu;

kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.

272:27 Kut 6:2; Isa 44:8; 45:5; 54:4; Yoe 3:17; Law 26:11; Sef 3:11Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli

kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu,

na kwamba hakuna mwingine;

kamwe watu wangu hawataaibika tena.

Siku Ya Bwana

282:28 Yn 7:38; 11:2; Eze 39:29; Mdo 21:9; Hes 11:17; Gal 3:14; 1Sam 19:20“Hata itakuwa, baada ya hayo,

nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili.

Wana wenu na binti zenu watatabiri,

wazee wenu wataota ndoto,

na vijana wenu wataona maono.

292:29 1Kor 12:13; Gal 3:28; Eze 36:27Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake,

katika siku zile nitamimina Roho wangu.

302:30 Lk 21:11; Mk 13:24-25Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu

na duniani:

damu, moto na mawimbi ya moshi.

312:31 Isa 22:5; Mt 24:29; Isa 13:9-10; Mal 3:2; Yer 4:23; Yoe 1:15Jua litageuzwa kuwa giza

na mwezi kuwa mwekundu kama damu,

kabla ya kuja siku ya Bwana

ile kuu na ya kutisha.

322:32 Rum 9:27; 10:13; Oba 1:17; Mik 4:7; 7:18; Isa 11:11; 46:13; Za 106:8; 50:12; Yer 33:3; Mwa 4:26; Mdo 2:21, 39Na kila mtu atakayeliitia

jina la Bwana ataokolewa.

Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu

kutakuwepo wokovu,

kama Bwana alivyosema,

miongoni mwa walionusurika

ambao Bwana awaita.