Yeremia 7 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 7:1-34

Dini Za Uongo Hazina Maana

1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 27:2 Yer 17:19; 19:2-3“Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu:

“ ‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana. 37:3 Yer 26:13; 35:13; 18:11Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa. 47:4 Yer 28:15; Mik 3:11; Ay 15:31Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!” 57:5 Kut 22:22; Law 25:17; Isa 1:17; Yer 26:13Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake, 67:6 2Fal 21:16; Kum 8:19; Yer 22:3; Kut 20:3; Yer 5:28; Eze 22:7; Yer 2:34kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe, 77:7 Kum 4:40; Yos 1:16ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele. 8Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.

97:9 Yer 11:13-17; Kut 20:3; Hos 2:13; Kut 20:13-15; Law 19:12; Zek 8:17; Yer 32:29“ ‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua, 107:10 2Fal 21:4-5; Eze 23:38-39; Yer 23:11; 32:34; Eze 33:25kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza? 117:11 Isa 56:7; Mt 21:13; Mk 11:17; Mwa 31:50; Amu 11:10; Hes 11:29; Lk 19:40; Yer 42:5Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.

127:12 1Sam 4:10; Yos 18:1; Za 78:60-64; 1Sam 2:32; Kut 40:2; Yos 18:10; Dan 9:18“ ‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli. 137:13 2Nya 36:15; Isa 65:12; Yer 35:17; Za 71:17; Isa 48:17; Yer 32:33; Mit 1:24Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu. 14Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu. 157:15 Mwa 4:14; Kut 33; 15; 2Fal 17:20; Za 78:67; Yer 23:39Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’

167:16 Kut 32:10; Kum 9:14; Hes 23:19“Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza. 17Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 187:18 Yer 44:17; 19:13; Kum 31:17; 1Fal 14:9; Isa 57:6Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha. 197:19 Ay 7:20; 1Kor 10:22; Yer 22:22; Kum 32:21; Yer 44:3; 9:19Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?

207:20 Ay 40:11; Mao 2:3-5; Isa 30:15; Yer 42:18; 6:11-12; Mao 4:11; Eze 20:47-48“ ‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.

217:21 Isa 1:11; Amo 5:21-22; 1Sam 2:12-17; Hos 8:13; Yer 6:20; 7:22; Isa 43:23; 1Sam 15:22“ ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe! 22Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu, 237:23 Kut 15:26; 19:5; Law 26:12; Kum 5:33; 1Yn 3:23; Isa 51:16; 1Fal 8:36; 7:24; Za 81:11-12; Kum 29:19; Yer 34:14; 6:10; 11:8; 17:23; 3:17; 2:19lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa. 24Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele. 257:25 Neh 9:30; Yer 25:4; 2Nya 36:15; Isa 20:3; Hes 11:29; Yer 35:15Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii. 267:26 Za 81:11; Kut 32:9; Mdo 7:51; Yer 16:12; Lk 11:27Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’

277:27 Eze 2:7; Zek 7:13; Eze 3:7; Isa 65:12“Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu. 28Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao. 297:29 Isa 15:2; Hos 11:8; Mik 5:3; Law 21:5; Ay 1:20; Yer 4:8; 6:30; 12:7Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.

Bonde La Machinjo

307:30 Yer 2:7; 32:34; Eze 7:20-22; Law 20:3“ ‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi. 317:31 2Fal 23:10; Law 18:21; Za 106:38; Eze 20:31; Mik 6:7; Yos 15:8; 2Nya 33:6Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu. 327:32 Yer 19:6; 19:11Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi. 337:33 Kum 28:26; Eze 29:5; Mwa 15:11; Yer 6:11; 14:16Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza. 347:34 Hos 2:11; Isa 24:8; Eze 26:13; Ufu 18:23; Zek 7:14; Mt 23:38; Isa 24:7-12Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.

New International Version

Jeremiah 7:1-34

False Religion Worthless

1This is the word that came to Jeremiah from the Lord: 2“Stand at the gate of the Lord’s house and there proclaim this message:

“ ‘Hear the word of the Lord, all you people of Judah who come through these gates to worship the Lord. 3This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: Reform your ways and your actions, and I will let you live in this place. 4Do not trust in deceptive words and say, “This is the temple of the Lord, the temple of the Lord, the temple of the Lord!” 5If you really change your ways and your actions and deal with each other justly, 6if you do not oppress the foreigner, the fatherless or the widow and do not shed innocent blood in this place, and if you do not follow other gods to your own harm, 7then I will let you live in this place, in the land I gave your ancestors for ever and ever. 8But look, you are trusting in deceptive words that are worthless.

9“ ‘Will you steal and murder, commit adultery and perjury,7:9 Or and swear by false gods burn incense to Baal and follow other gods you have not known, 10and then come and stand before me in this house, which bears my Name, and say, “We are safe”—safe to do all these detestable things? 11Has this house, which bears my Name, become a den of robbers to you? But I have been watching! declares the Lord.

12“ ‘Go now to the place in Shiloh where I first made a dwelling for my Name, and see what I did to it because of the wickedness of my people Israel. 13While you were doing all these things, declares the Lord, I spoke to you again and again, but you did not listen; I called you, but you did not answer. 14Therefore, what I did to Shiloh I will now do to the house that bears my Name, the temple you trust in, the place I gave to you and your ancestors. 15I will thrust you from my presence, just as I did all your fellow Israelites, the people of Ephraim.’

16“So do not pray for this people nor offer any plea or petition for them; do not plead with me, for I will not listen to you. 17Do you not see what they are doing in the towns of Judah and in the streets of Jerusalem? 18The children gather wood, the fathers light the fire, and the women knead the dough and make cakes to offer to the Queen of Heaven. They pour out drink offerings to other gods to arouse my anger. 19But am I the one they are provoking? declares the Lord. Are they not rather harming themselves, to their own shame?

20“ ‘Therefore this is what the Sovereign Lord says: My anger and my wrath will be poured out on this place—on man and beast, on the trees of the field and on the crops of your land—and it will burn and not be quenched.

21“ ‘This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: Go ahead, add your burnt offerings to your other sacrifices and eat the meat yourselves! 22For when I brought your ancestors out of Egypt and spoke to them, I did not just give them commands about burnt offerings and sacrifices, 23but I gave them this command: Obey me, and I will be your God and you will be my people. Walk in obedience to all I command you, that it may go well with you. 24But they did not listen or pay attention; instead, they followed the stubborn inclinations of their evil hearts. They went backward and not forward. 25From the time your ancestors left Egypt until now, day after day, again and again I sent you my servants the prophets. 26But they did not listen to me or pay attention. They were stiff-necked and did more evil than their ancestors.’

27“When you tell them all this, they will not listen to you; when you call to them, they will not answer. 28Therefore say to them, ‘This is the nation that has not obeyed the Lord its God or responded to correction. Truth has perished; it has vanished from their lips.

29“ ‘Cut off your hair and throw it away; take up a lament on the barren heights, for the Lord has rejected and abandoned this generation that is under his wrath.

The Valley of Slaughter

30“ ‘The people of Judah have done evil in my eyes, declares the Lord. They have set up their detestable idols in the house that bears my Name and have defiled it. 31They have built the high places of Topheth in the Valley of Ben Hinnom to burn their sons and daughters in the fire—something I did not command, nor did it enter my mind. 32So beware, the days are coming, declares the Lord, when people will no longer call it Topheth or the Valley of Ben Hinnom, but the Valley of Slaughter, for they will bury the dead in Topheth until there is no more room. 33Then the carcasses of this people will become food for the birds and the wild animals, and there will be no one to frighten them away. 34I will bring an end to the sounds of joy and gladness and to the voices of bride and bridegroom in the towns of Judah and the streets of Jerusalem, for the land will become desolate.