Yeremia 50 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 50:1-46

Ujumbe Kuhusu Babeli

150:1 Isa 13:1; Za 137:8; Mwa 10:10Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:

250:2 Kum 30:4; Yer 4:16; 51:31, 47; Isa 21:9; Za 20:5; Isa 13:2; Yer 46:6; Law 26:30“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa,

twekeni bendera na mkahubiri;

msiache kitu chochote, bali semeni,

‘Babeli utatekwa;

Beli ataaibishwa,

Merodaki atajazwa na hofu kuu.

Sanamu zake zitaaibishwa

na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’

350:3 Isa 14:22-23; Yer 9:11; Sef 1:3; Isa 13:17; 41:25; Yer 25:26Taifa kutoka kaskazini litamshambulia,

na kuifanya nchi yake ukiwa.

Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,

watu na wanyama wataikimbia.

450:4 Eze 37:22; Ezr 3:12; Yer 31:9; Isa 9:13; Hos 3:5; Yer 3:18“Katika siku hizo, wakati huo,”

asema Bwana,

“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda

wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.

550:5 1Sam 29:1; Yer 33:7; Kum 29:14; Ebr 8:6-10; Isa 11:16; Yer 31:21; 32:40Wataiuliza njia iendayo Sayuni

na kuelekeza nyuso zao huko.

Watakuja na kuambatana na Bwana

katika agano la milele

ambalo halitasahaulika.

650:6 Isa 53:6; Mt 10:6; Yer 3:6; Eze 34:6; Za 119:176; Mt 9:36; Yer 10:21; Za 95:10“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;

wachungaji wao wamewapotosha

na kuwasababisha kuzurura

juu ya milima.

Walitangatanga juu ya mlima na kilima,

na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.

750:7 Yer 2:3; 14:8; Za 22:4; Yer 5:17; 10:25; Eze 35:12Yeyote aliyewakuta aliwala;

adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia,

kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi,

Bwana, aliye tumaini la baba zao.’

850:8 Isa 48:20; Ufu 18:4; Yer 51:6“Kimbieni kutoka Babeli;

ondokeni katika nchi ya Wakaldayo

tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.

950:9 Isa 13:17; Yer 25:14; Isa 41:25; Yer 25:26Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli

muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini.

Watashika nafasi zao dhidi yake,

naye kutokea kaskazini atatekwa.

Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari,

ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.

10Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara;

wote wamtekao nyara watapata za kutosha,”

asema Bwana.

1150:11 Isa 47:6; Yer 31:18“Kwa sababu hushangilia na kufurahi,

wewe utekaye urithi wangu,

kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka,

na kulia kama farasi dume,

1250:12 Yer 51:47; 25:12; 51:26mama yako ataaibika mno,

yeye aliyekuzaa atatahayari.

Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote,

atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.

1350:13 Eze 27:36; Hab 2:6; Kum 29:22; Yer 49:17; 9:11; 48:9; 51:62; 18:16Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu,

lakini ataachwa ukiwa kabisa.

Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki

kwa sababu ya majeraha yake yote.

14“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli,

enyi nyote mvutao upinde.

Mpigeni! Msibakize mshale wowote,

kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.

1550:15 Yer 51:14; 2Nya 30:8; Yer 51:44-58; 2Fal 25:4; Yer 51:6; Ufu 18:6; Isa 10:3; Hab 2:7-8Piga kelele dhidi yake kila upande!

Anajisalimisha, minara yake inaanguka,

kuta zake zimebomoka.

Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana,

mlipizeni kisasi;

mtendeeni kama alivyowatendea wengine.

1650:16 Yer 25:38; Isa 13:14; Yer 51:9Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli,

pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna.

Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu

kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja na akimbilie

kwenye nchi yake mwenyewe.

1750:17 2Fal 24:1; Yer 2:15; Kum 4:27; 2Fal 17:6; 24:10-17; 1Pet 2:25; Yer 2:15; Hes 24:8“Israeli ni kundi lililotawanyika

ambalo simba wamelifukuzia mbali.

Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru,

wa mwisho kuponda mifupa yake

alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”

1850:18 Isa 10:12; Eze 31:3; Sef 2:13Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake

kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.

1950:19 Yer 31:10; Eze 34:13; Yer 33:12; Isa 65:10; Mik 7:14; Zek 10:10Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe

naye atalisha huko Karmeli na Bashani;

njaa yake itashibishwa

juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.

2050:20 Za 103:12; Zek 3:4-9; Isa 33:24; Yer 31:34; Rum 9:27; Isa 10:20-22; Eze 36:16Katika siku hizo, wakati huo,”

asema Bwana,

“uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli,

lakini halitakuwepo,

kwa ajili ya dhambi za Yuda,

lakini haitapatikana hata moja,

kwa kuwa nitawasamehe

mabaki nitakaowaacha.

2150:21 Eze 23:23; Isa 10:6“Shambulieni nchi ya Merathaimu

na wale waishio huko Pekodi.

Wafuatieni, waueni

na kuwaangamiza kabisa,”

asema Bwana.

“Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.

2250:22 Yer 4:19-21; 51:54Kelele ya vita iko ndani ya nchi,

kelele ya maangamizi makuu!

2350:23 Isa 14:16; Yer 51:20; Isa 10:5Tazama jinsi nyundo ya dunia yote

ilivyovunjika na kuharibika!

Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa

miongoni mwa mataifa!

2450:24 Yer 51:12; Dan 5:30-31; Yer 51:31; Ay 9:4Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli,

nawe ukakamatwa kabla haujafahamu;

ulipatikana na ukakamatwa

kwa sababu ulimpinga Bwana.

2550:25 Isa 13:5Bwana amefungua ghala lake la silaha

na kuzitoa silaha za ghadhabu yake,

kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote

anayo kazi ya kufanya

katika nchi ya Wakaldayo.

2650:26 Isa 14:22-23; Yer 51:11; Rut 3:7Njooni dhidi yake kutoka mbali.

Zifungueni ghala zake za nafaka;

mlundikeni kama lundo la nafaka.

Mwangamizeni kabisa

na msimwachie mabaki yoyote.

2750:27 Za 68:30; Yer 48:15; Ay 18:20; Yer 25:34Waueni mafahali wake wachanga wote;

waacheni washuke machinjoni!

Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia,

wakati wao wa kuadhibiwa.

2850:28 Isa 48:20; Yer 51:10; 2Fal 24:13; Yer 52:13Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli

wakitangaza katika Sayuni

jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

2950:29 Ay 21:19; Ufu 18:6; Oba 1:15; Dan 5:23; Isa 14:13-14; Mao 3:24; Isa 13:18; Kum 32:41“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli,

wote wale wavutao upinde.

Pigeni kambi kumzunguka kabisa,

asitoroke mtu yeyote.

Mlipizeni kwa matendo yake;

mtendeeni kama alivyotenda.

Kwa kuwa alimdharau Bwana,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

3050:30 Isa 13:18; Yer 49:26; 51:4Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote watanyamazishwa siku ile,”

asema Bwana.

3150:31 Yer 21:13; Ufu 18:7-8“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

“kwa kuwa siku yako imewadia,

yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.

3250:32 Yer 21:14; 49:27; Amo 5:2; Za 20:8; 119:21Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka,

wala hakuna yeyote atakayemuinua;

nitawasha moto katika miji yake,

utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

3350:33 Isa 58:6; 14:17Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Watu wa Israeli wameonewa,

nao watu wa Yuda pia.

Wote waliowateka wamewashikilia sana,

wanakataa kuwaachia waende.

3450:34 Yer 31:35; 51:19; Za 119:154; Mao 3:58; Kut 6:6; Ay 19:25; Isa 49:25Lakini Mkombozi wao ana nguvu;

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

Atatetea kwa nguvu shauri lao

ili alete raha katika nchi yao,

lakini ataleta msukosuko

kwa wale waishio Babeli.

3550:35 Yer 47:6; Dan 5:7; Isa 37:13; 45:1“Upanga dhidi ya Wakaldayo!”

asema Bwana,

“dhidi ya wale waishio Babeli

na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!

36Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo!

Watakuwa wapumbavu.

Upanga dhidi ya mashujaa wake!

Watajazwa na hofu kuu

3750:37 Yer 25:20; 2Fal 19:23; Isa 19:16; Yer 51:21; Nah 3:13; Isa 45:3Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita

pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake!

Wao watakuwa kama wanawake.

Upanga dhidi ya hazina zake!

Hizo zitatekwa nyara.

3850:38 Isa 11:15; Yer 51:36; Ufu 16:12Ukame juu ya maji yake!

Nayo yatakauka.

Kwa kuwa ni nchi ya sanamu,

wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.

3950:39 Isa 34:13-15; Ufu 18:2; Isa 13:19-22; Za 74:14; Yer 51:37“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo,

nao bundi watakaa humo.

Kamwe haitakaliwa tena

wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

4050:40 Mwa 19:24; Mt 10:15; 2Pet 2:6; Yer 51:62Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora

pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,”

asema Bwana,

“vivyo hivyo hakuna mtu yeyote

atakayeishi humo.

Naam, hakuna mtu yeyote

atakayekaa humo.

4150:41 Isa 41:25; Yer 6:22; Isa 13:14; Yer 51:22-28; Ufu 17:16; Isa 23:17“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini;

taifa kubwa na wafalme wengi

wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.

4250:42 Isa 13:18; 5:30; 47:1; Yer 6:23; Ay 30:21Wamejifunga pinde na mikuki;

ni wakatili na wasio na huruma.

Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao;

wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita

ili kukushambulia, ee Binti Babeli.

4350:43 Yer 47:3; 6:22-24Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu,

nayo mikono yake imelegea.

Uchungu umemshika,

maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4450:44 Hes 16:5; Ay 41:10; Isa 46:9; Yer 12:5; 49:19Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho mengi,

ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula.

Ni nani aliye mteule,

nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi,

na ni nani awezaye kunipinga?

Tena ni mchungaji yupi

awezaye kusimama kinyume nami?”

4550:45 Isa 24:14; Mdo 4:28; Isa 48:14; Yer 51:11Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli,

kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali.

Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.

4650:46 Ay 24:12; Ufu 18:9-10; Amu 5:4; Yer 49:21Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka;

kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.