Yeremia 48 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 48:1-47

Ujumbe Kuhusu Moabu

148:1 Hes 32:37; Yos 13:19; Mwa 19:37; Kum 23:6Kuhusu Moabu:

Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa.

Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa;

Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.

248:2 Hes 21:25; Isa 16:14; Yos 23:16Moabu haitasifiwa tena;

huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake:

‘Njooni na tuangamize taifa lile.’

Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa;

upanga utakufuatia.

3Sikiliza kilio kutoka Horonaimu,

kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.

4Moabu utavunjwa,

wadogo wake watapiga kelele.

548:5 Isa 15:5Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi,

wakilia kwa uchungu wanapotembea,

kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu,

kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.

648:6 Yer 17:6; Mwa 19:17Kimbieni! Okoeni maisha yenu,

kuweni kama kichaka jangwani.

748:7 Hes 21:29; Isa 46:1-2; Yer 49:3; 9:23; Za 49:6; Mk 11:28; Amo 2:3Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu,

ninyi pia mtachukuliwa mateka,

naye Kemoshi48:7 Kemoshi alikuwa mungu wa Wamoabu. atakwenda uhamishoni,

pamoja na makuhani wake na maafisa wake.

848:8 Kut 12:23; Yer 4:7; Yos 13:9Mharabu atakuja dhidi ya kila mji,

wala hakuna mji utakaookoka.

Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa,

kwa sababu Bwana amesema.

948:9 Amu 9:45; Yer 51:29Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu,

kwa kuwa ataangamizwa;

miji yake itakuwa ukiwa,

pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.

1048:10 Yer 47:6; 1Fal 20:42; 1Sam 15:3, 11; 2Fal 13:15-19“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila!

Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!

1148:11 Zek 1:15; Sef 1:12“Moabu amestarehe tangu ujana wake,

kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake,

haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine,

hajaenda uhamishoni.

Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo,

nayo harufu yake haijabadilika.

12Lakini siku zinakuja,”

asema Bwana,

“nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia,

nao watamimina;

wataacha magudulia yake yakiwa matupu

na kuvunja mitungi yake.

1348:13 Hos 10:6; Amu 11:24; Yos 7:2Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi,

kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu

walipotegemea mungu wa Betheli.48:13 Betheli ina maana ya Nyumba ya Mungu; lakini pia ni mahali ambapo Mfalme Yeroboamu alisimamisha moja ya sanamu za ndama ili kuabudiwa; nyingine aliiweka huko Dani (1Fal 12:29-33).

1448:14 Mhu 9:11; Za 33:16“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa,

watu jasiri katika vita’?

1548:15 Yer 50:27; 51:40, 57; 46:18; Isa 9:17Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa,

vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,”

asema Mfalme, ambaye jina lake

ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

16“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia,

janga kubwa litamjia kwa haraka.

1748:17 Za 110:2; 2Fal 3:4-5Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka,

ninyi nyote mnaojua sifa zake,

semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu,

tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’

1848:18 Isa 47:1; Hes 21:30; Yos 13:9“Shuka kutoka fahari yako

na uketi katika ardhi iliyokauka,

enyi wenyeji wa Binti wa Diboni,

kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako,

na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.

1948:19 Hes 32:34; Kum 2:36Simama kando ya barabara na utazame,

wewe unayeishi Aroeri.

Muulize mwanaume anayekimbia

na mwanamke anayetoroka,

waulize, ‘Kumetokea nini?’

2048:20 Isa 16:7; Hes 21:13Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa.

Lieni kwa huzuni na kupiga kelele!

Tangazeni kando ya Arnoni

kwamba Moabu ameangamizwa.

2148:21 Hes 21:23; Isa 15:4; Yos 13:18; 15:51; 13:9, 21Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu:

katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,

2248:22 Hes 21:30; Yos 13:9, 17; Hes 32:38katika Diboni, Nebo

na Beth-Diblathaimu,

2348:23 Hes 32:38; Yos 13:17-19katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli

na Beth-Meoni,

2448:24 Amo 2:2; Yer 49:13; Isa 15:1katika Keriothi na Bosra;

kwa miji yote ya Moabu,

iliyoko mbali na karibu.

2548:25 Za 75:10; Eze 30:21; Za 37:17Pembe48:25 Pembe hapa ni ishara ya nguvu. ya Moabu imekatwa,

mkono wake umevunjwa,”

asema Bwana.

2648:26 Yer 25:16, 27; 51:39; Isa 28:8; 1Sam 17:26“Mlevye,

kwa kuwa amemdharau Bwana.

Moabu na agaegae katika matapishi yake,

yeye na awe kitu cha dhihaka.

2748:27 Mit 24:17; Yer 2:26; Ay 16:4; Za 44:14; Mik 7:8-10; Kum 7:8-10; Sef 2:8Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa?

Je, alikamatwa miongoni mwa wezi,

kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau

kila mara unapozungumza juu yake?

2848:28 Za 55:6-7; Wim 1:15; Amu 6:2; Wim 2:14; Mwa 8; 8Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba,

enyi mnaoishi Moabu.

Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake

kwenye mdomo wa pango.

2948:29 Law 26:19; Isa 16:6; Ay 40:12; Mit 10:5; 16:18“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno,

kiburi chake na ufidhuli wake,

na kujivuna kwa moyo wake.

30Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,”

asema Bwana,

“nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.

3148:31 Isa 15:5-6; 2Fal 3:25Kwa hiyo namlilia Moabu,

kwa ajili ya Moabu yote ninalia,

ninaomboleza kwa ajili

ya watu wa Kir-Haresethi.

3248:32 Hes 32:3; 21:13; Isa 16:8-9; Yos 13:25Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo,

enyi mizabibu ya Sibma.

Matawi yako yameenea hadi baharini;

yamefika hadi bahari ya Yazeri.

Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva

na mizabibu yako iliyoiva.

3348:33 Isa 16:10; 24:7; Amo 5:17; Yoe 1:12Shangwe na furaha vimetoweka

kutoka bustani na mashamba ya Moabu.

Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo;

hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe.

Ingawa kuna kelele,

sio kelele za shangwe.

3448:34 Isa 15:4-6; Hes 32:3; 21:23; Mwa 13:10; Yos 13:26; Hes 21:25“Sauti ya kilio chao inapanda

kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi,

kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya,

kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.

3548:35 Isa 15:2; 16:12; Yer 11:13Nitakomesha wale wote katika Moabu

watoao sadaka mahali pa juu,

na kufukiza uvumba kwa miungu yao,”

asema Bwana.

3648:36 Isa 16:11; 15:7; Mit 11:4; 2Fal 3:25“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi;

unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

Utajiri waliojipatia umetoweka.

3748:37 Isa 15:2; Eze 29:18; Isa 3:24; Amo 8:10; Eze 27:31; 2Sam 10:4Kila kichwa kimenyolewa

na kila mwenye ndevu zimekatwa;

kila mkono umekatwa

na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.

3848:38 Yer 22:28; Isa 15:3Juu ya mapaa yote katika Moabu

na katika viwanja

hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo,

kwa kuwa nimemvunja Moabu

kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,”

asema Bwana.

39“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika!

Jinsi wanavyolia kwa huzuni!

Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu!

Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa,

kitu cha kutisha kwa wale wote

wanaomzunguka.”

4048:40 Kum 28:29; Hab 1:8; Isa 8:8; Yer 49:22Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama! Tai anashuka chini,

akitanda mabawa yake juu ya Moabu.

4148:41 Isa 21:3; Mik 4:9; Amo 2:16; Isa 15:1Miji itatekwa na ngome zake

zitatwaliwa.

Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu

itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4248:42 Za 83:4; Isa 16:14; Mit 16:18Moabu ataangamizwa kama taifa

kwa sababu amemdharau Bwana.

4348:43 Isa 24:17, 18; Yer 49:5Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea,

enyi watu wa Moabu,”

asema Bwana.

4448:44 1Fal 19:17; Ay 20:24; Yer 11:23; 23:12; Isa 24:18“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu

ataanguka ndani ya shimo,

yeyote atakayepanda kutoka shimoni,

atanaswa katika mtego,

kwa sababu nitaletea Moabu

mwaka wa adhabu yake,”

asema Bwana.

4548:45 Hes 21:21, 26-28; Yos 12:2; Hes 24:17“Katika kivuli cha Heshboni,

wakimbizi wamesimama pasipo msaada,

kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni,

mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni;

unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu,

mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.

4648:46 Hes 21:29; Amu 11:24Ole wako, ee Moabu!

Watu wa Kemoshi wameangamizwa;

wana wako wamepelekwa uhamishoni

na binti zako wamechukuliwa mateka.

4748:47 Za 14:7; Dan 11:41; Yer 49:6; Isa 11:1; Yer 12:15; Eze 16:53“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu,

katika siku zijazo,”

asema Bwana.

Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.

New International Version

Jeremiah 48:1-47

A Message About Moab

1Concerning Moab:

This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says:

“Woe to Nebo, for it will be ruined.

Kiriathaim will be disgraced and captured;

the stronghold48:1 Or captured; / Misgab will be disgraced and shattered.

2Moab will be praised no more;

in Heshbon48:2 The Hebrew for Heshbon sounds like the Hebrew for plot. people will plot her downfall:

‘Come, let us put an end to that nation.’

You, the people of Madmen,48:2 The name of the Moabite town Madmen sounds like the Hebrew for be silenced. will also be silenced;

the sword will pursue you.

3Cries of anguish arise from Horonaim,

cries of great havoc and destruction.

4Moab will be broken;

her little ones will cry out.48:4 Hebrew; Septuagint / proclaim it to Zoar

5They go up the hill to Luhith,

weeping bitterly as they go;

on the road down to Horonaim

anguished cries over the destruction are heard.

6Flee! Run for your lives;

become like a bush48:6 Or like Aroer in the desert.

7Since you trust in your deeds and riches,

you too will be taken captive,

and Chemosh will go into exile,

together with his priests and officials.

8The destroyer will come against every town,

and not a town will escape.

The valley will be ruined

and the plateau destroyed,

because the Lord has spoken.

9Put salt on Moab,

for she will be laid waste48:9 Or Give wings to Moab, / for she will fly away;

her towns will become desolate,

with no one to live in them.

10“A curse on anyone who is lax in doing the Lord’s work!

A curse on anyone who keeps their sword from bloodshed!

11“Moab has been at rest from youth,

like wine left on its dregs,

not poured from one jar to another—

she has not gone into exile.

So she tastes as she did,

and her aroma is unchanged.

12But days are coming,”

declares the Lord,

“when I will send men who pour from pitchers,

and they will pour her out;

they will empty her pitchers

and smash her jars.

13Then Moab will be ashamed of Chemosh,

as Israel was ashamed

when they trusted in Bethel.

14“How can you say, ‘We are warriors,

men valiant in battle’?

15Moab will be destroyed and her towns invaded;

her finest young men will go down in the slaughter,”

declares the King, whose name is the Lord Almighty.

16“The fall of Moab is at hand;

her calamity will come quickly.

17Mourn for her, all who live around her,

all who know her fame;

say, ‘How broken is the mighty scepter,

how broken the glorious staff!’

18“Come down from your glory

and sit on the parched ground,

you inhabitants of Daughter Dibon,

for the one who destroys Moab

will come up against you

and ruin your fortified cities.

19Stand by the road and watch,

you who live in Aroer.

Ask the man fleeing and the woman escaping,

ask them, ‘What has happened?’

20Moab is disgraced, for she is shattered.

Wail and cry out!

Announce by the Arnon

that Moab is destroyed.

21Judgment has come to the plateau—

to Holon, Jahzah and Mephaath,

22to Dibon, Nebo and Beth Diblathaim,

23to Kiriathaim, Beth Gamul and Beth Meon,

24to Kerioth and Bozrah—

to all the towns of Moab, far and near.

25Moab’s horn48:25 Horn here symbolizes strength. is cut off;

her arm is broken,”

declares the Lord.

26“Make her drunk,

for she has defied the Lord.

Let Moab wallow in her vomit;

let her be an object of ridicule.

27Was not Israel the object of your ridicule?

Was she caught among thieves,

that you shake your head in scorn

whenever you speak of her?

28Abandon your towns and dwell among the rocks,

you who live in Moab.

Be like a dove that makes its nest

at the mouth of a cave.

29“We have heard of Moab’s pride—

how great is her arrogance!—

of her insolence, her pride, her conceit

and the haughtiness of her heart.

30I know her insolence but it is futile,”

declares the Lord,

“and her boasts accomplish nothing.

31Therefore I wail over Moab,

for all Moab I cry out,

I moan for the people of Kir Hareseth.

32I weep for you, as Jazer weeps,

you vines of Sibmah.

Your branches spread as far as the sea48:32 Probably the Dead Sea;

they reached as far as48:32 Two Hebrew manuscripts and Septuagint; most Hebrew manuscripts as far as the Sea of Jazer.

The destroyer has fallen

on your ripened fruit and grapes.

33Joy and gladness are gone

from the orchards and fields of Moab.

I have stopped the flow of wine from the presses;

no one treads them with shouts of joy.

Although there are shouts,

they are not shouts of joy.

34“The sound of their cry rises

from Heshbon to Elealeh and Jahaz,

from Zoar as far as Horonaim and Eglath Shelishiyah,

for even the waters of Nimrim are dried up.

35In Moab I will put an end

to those who make offerings on the high places

and burn incense to their gods,”

declares the Lord.

36“So my heart laments for Moab like the music of a pipe;

it laments like a pipe for the people of Kir Hareseth.

The wealth they acquired is gone.

37Every head is shaved

and every beard cut off;

every hand is slashed

and every waist is covered with sackcloth.

38On all the roofs in Moab

and in the public squares

there is nothing but mourning,

for I have broken Moab

like a jar that no one wants,”

declares the Lord.

39“How shattered she is! How they wail!

How Moab turns her back in shame!

Moab has become an object of ridicule,

an object of horror to all those around her.”

40This is what the Lord says:

“Look! An eagle is swooping down,

spreading its wings over Moab.

41Kerioth48:41 Or The cities will be captured

and the strongholds taken.

In that day the hearts of Moab’s warriors

will be like the heart of a woman in labor.

42Moab will be destroyed as a nation

because she defied the Lord.

43Terror and pit and snare await you,

you people of Moab,”

declares the Lord.

44“Whoever flees from the terror

will fall into a pit,

whoever climbs out of the pit

will be caught in a snare;

for I will bring on Moab

the year of her punishment,”

declares the Lord.

45“In the shadow of Heshbon

the fugitives stand helpless,

for a fire has gone out from Heshbon,

a blaze from the midst of Sihon;

it burns the foreheads of Moab,

the skulls of the noisy boasters.

46Woe to you, Moab!

The people of Chemosh are destroyed;

your sons are taken into exile

and your daughters into captivity.

47“Yet I will restore the fortunes of Moab

in days to come,”

declares the Lord.

Here ends the judgment on Moab.