Yeremia 47 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 47:1-7

Ujumbe Kuhusu Wafilisti

147:1 Zek 9:5-7; Sef 2:4-5; Amo 1:6; Mwa 10:14-19Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:

247:2 Isa 8:7; 14:31; 15:3Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini,

yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana.

Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake,

miji na wale waishio ndani yake.

Watu watapiga kelele;

wote waishio katika nchi wataomboleza

347:3 Yer 46:9; Eze 23:24; Yer 50:43; Eze 7:17; 21:7kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio,

kwa sauti ya magari ya adui

na mngurumo wa magurudumu yake.

Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao,

mikono yao italegea.

447:4 Isa 23:1; Amo 1:9-10; Mwa 10:14-15; Yer 25:22; Yoe 3:4; Kum 2:23; Za 9:2-4Kwa maana siku imewadia

kuwaangamiza Wafilisti wote

na kuwakatilia mbali walionusurika wote

ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni.

Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti,

mabaki toka pwani za Kaftori.47:4 Kaftori ndio Krete.

547:5 Yer 41:5; Mik 1:16; Yer 25:20; Law 19:28Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza,

Ashkeloni atanyamazishwa.

Enyi mabaki kwenye tambarare,

mtajikatakata wenyewe mpaka lini?

647:6 Isa 34:5; Yer 12:12; Eze 21:3; Yer 48:10; 50:35“Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana,

utaendelea mpaka lini ndipo upumzike?

Rudi ndani ya ala yako;

acha na utulie.’

747:7 Eze 25:15-17Lakini upanga utatuliaje

wakati Bwana ameuamuru,

wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni

pamoja na pwani yake?”