Yeremia 41 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 41:1-18

141:1 Yer 40:8; Lk 22:21; Za 41:9Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko, 241:2 Za 41:9; Yer 40:5; 2Sam 3:27; Rum 3:15; Yos 11:10; Ebr 11:37; 2Sam 20:9-10; Yer 40:8Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi. 3Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.

4Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo, 541:5 Law 19:27; Yer 48:37; Mwa 12:6; 1Fal 16:24; 3:2; Isa 15:2; Yer 47:5; Hes 16:40; Amu 9:1-57; Mk 14:63watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana. 641:6 2Sam 5:16; Ufu 20:10; Hos 7:11; Za 5:9Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.” 741:7 Mwa 27:24; 2Fal 10:14Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima. 841:8 Isa 45:3Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine. 941:9 1Fal 15:22; 2Nya 16:6; Amu 6:2; Yos 10:16-18Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.

1041:10 Yer 40:7, 12-14; Neh 2:10, 19Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.

1141:11 Yer 40:8-13Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya, 1241:12 2Sam 2:13; Yn 9:7; Kut 14:14; Yn 18:36; Yos 9:3waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni. 13Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi. 14Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea. 1541:15 Yos 21:30; Mit 28; 17; 1Sam 30:17Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.

Kukimbilia Misri

1641:16 Yer 42:1; 43:2-4; Eze 7:16; 14:22; Sef 2:9Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni. 1741:17 2Sam 19:37; Yer 42:14; Mwa 35:19; Mik 5:2Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri 1841:18 Hes 14:9; Lk 12:4-5; Yer 40:5; Isa 5:12; Yer 42:16; 2Fal 25:22ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.

New International Version

Jeremiah 41:1-18

1In the seventh month Ishmael son of Nethaniah, the son of Elishama, who was of royal blood and had been one of the king’s officers, came with ten men to Gedaliah son of Ahikam at Mizpah. While they were eating together there, 2Ishmael son of Nethaniah and the ten men who were with him got up and struck down Gedaliah son of Ahikam, the son of Shaphan, with the sword, killing the one whom the king of Babylon had appointed as governor over the land. 3Ishmael also killed all the men of Judah who were with Gedaliah at Mizpah, as well as the Babylonian41:3 Or Chaldean soldiers who were there.

4The day after Gedaliah’s assassination, before anyone knew about it, 5eighty men who had shaved off their beards, torn their clothes and cut themselves came from Shechem, Shiloh and Samaria, bringing grain offerings and incense with them to the house of the Lord. 6Ishmael son of Nethaniah went out from Mizpah to meet them, weeping as he went. When he met them, he said, “Come to Gedaliah son of Ahikam.” 7When they went into the city, Ishmael son of Nethaniah and the men who were with him slaughtered them and threw them into a cistern. 8But ten of them said to Ishmael, “Don’t kill us! We have wheat and barley, olive oil and honey, hidden in a field.” So he let them alone and did not kill them with the others. 9Now the cistern where he threw all the bodies of the men he had killed along with Gedaliah was the one King Asa had made as part of his defense against Baasha king of Israel. Ishmael son of Nethaniah filled it with the dead.

10Ishmael made captives of all the rest of the people who were in Mizpah—the king’s daughters along with all the others who were left there, over whom Nebuzaradan commander of the imperial guard had appointed Gedaliah son of Ahikam. Ishmael son of Nethaniah took them captive and set out to cross over to the Ammonites.

11When Johanan son of Kareah and all the army officers who were with him heard about all the crimes Ishmael son of Nethaniah had committed, 12they took all their men and went to fight Ishmael son of Nethaniah. They caught up with him near the great pool in Gibeon. 13When all the people Ishmael had with him saw Johanan son of Kareah and the army officers who were with him, they were glad. 14All the people Ishmael had taken captive at Mizpah turned and went over to Johanan son of Kareah. 15But Ishmael son of Nethaniah and eight of his men escaped from Johanan and fled to the Ammonites.

Flight to Egypt

16Then Johanan son of Kareah and all the army officers who were with him led away all the people of Mizpah who had survived, whom Johanan had recovered from Ishmael son of Nethaniah after Ishmael had assassinated Gedaliah son of Ahikam—the soldiers, women, children and court officials he had recovered from Gibeon. 17And they went on, stopping at Geruth Kimham near Bethlehem on their way to Egypt 18to escape the Babylonians.41:18 Or Chaldeans They were afraid of them because Ishmael son of Nethaniah had killed Gedaliah son of Ahikam, whom the king of Babylon had appointed as governor over the land.