Yeremia 4 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 4:1-31

14:1 Yoe 2:12; Ezr 8:5; 2Fal 7:13; 21:4; Kum 4:30; Hos 12:6; Yer 16:18; 35:15“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli,

nirudie mimi,”

asema Bwana.

“Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu

na usiendelee kutangatanga,

24:2 Kum 10:20; Hes 14:21; Gal 3:8; Hos 4:15; Mwa 12:2; Isa 19:18; 65:16; Yer 12:16ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa,

‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’

ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye

na katika yeye watajitukuza.”

34:3 Hos 10:12; Mk 4:18Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu:

“Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu,

wala msipande katikati ya miiba.

44:4 Law 26:41; Rum 2:28-29; Sef 2:2; Amo 5:6; Ay 41:21; Kut 32:22; Yer 8:14; Yos 10:20; Yer 5:20; Hes 10:2-7; Ay 39:24Jitahirini katika Bwana,

tahirini mioyo yenu,

enyi wanaume wa Yuda

na watu wa Yerusalemu,

la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu

na kuwaka kama moto

kwa sababu ya uovu mliotenda,

ikiwaka pasipo wa kuizima.

Maafa Kutoka Kaskazini

5“Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema:

‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’

Piga kelele na kusema:

‘Kusanyikeni pamoja!

Tukimbilie katika miji yenye maboma!’

64:6 Yer 1:13-15; Isa 14:31; Za 74:4; Isa 31:9; Yer 50:2; 11:11; 18:11Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni!

Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa!

Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini,

maangamizi ya kutisha.”

74:7 Dan 7:4; Eze 12:20; Yer 2:15; Isa 6:11; Yer 25:38; Hos 5:14; Nah 2:12; Yer 6:26Simba ametoka nje ya pango lake,

mharabu wa mataifa amejipanga.

Ametoka mahali pake

ili aangamize nchi yenu.

Miji yenu itakuwa magofu

pasipo mtu wa kuishi humo.

84:8 1Fal 21:27; Yer 30:24; Isa 22:12; 3:24; Yer 6:26; Eze 7:18; Yer 7:29; 9:20Hivyo vaeni nguo za magunia,

ombolezeni na kulia kwa huzuni,

kwa kuwa hasira kali ya Bwana

haijaondolewa kwetu.

9“Katika siku ile,” asema Bwana

“mfalme na maafisa watakata tamaa,

makuhani watafadhaika,

na manabii watashangazwa mno.”

104:10 Eze 14:9; Kut 5:23; 2The 2:11; Isa 63:17; Yer 6:14; 8:11; Eze 13:10; Mik 3:5Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”

114:11 Mwa 41:6; Hos 13:15; Eze 17:10; Law 26:33; Ay 1:19Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa, 124:12 Isa 64:6; Yer 1:16upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”

134:13 Isa 5:28; 2Sam 22:10; Eze 26:10; Kum 28:49; Mao 4:19; Isa 66:15Tazama! Anakuja kama mawingu,

magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli,

farasi wake wana mbio kuliko tai.

Ole wetu! Tunaangamia!

144:14 Rut 3; 3; Yak 4:8; Za 51:2; Isa 45:22; Za 6:3Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe.

Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?

154:15 Yer 8:16; Mwa 30:6; Yer 31:6Sauti inatangaza kutoka Dani,

ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.

16“Waambie mataifa jambo hili,

piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu:

‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali,

likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.

174:17 2Fal 25:1-4; 1Sam 12:15; Yer 5:23Wamemzunguka kama watu walindao shamba,

kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’ ”

asema Bwana.

184:18 Za 107:17; Ay 20:6-11; Yer 2:17-19; Isa 1:28; Yer 5:25“Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe

yameleta haya juu yako.

Hii ndiyo adhabu yako.

Tazama jinsi ilivyo chungu!

Tazama jinsi inavyochoma moyo!”

194:19 Isa 16:11; Mao 1:20; Hes 10:9; Yer 20:9; Sef 1:16; Isa 22:4; Yer 6:24Ee mtima wangu, mtima wangu!

Ninagaagaa kwa maumivu.

Ee maumivu makuu ya moyo wangu!

Moyo wangu umefadhaika ndani yangu,

siwezi kunyamaza.

Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta,

nimesikia kelele ya vita.

204:20 Kum 31:17; Za 42:7; Hes 24:5; Mao 2:4; Yer 10:20Maafa baada ya maafa,

nchi yote imekuwa magofu.

Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa,

makazi yangu kwa muda mfupi.

214:21 Hes 2:2; Isa 18:3; Yos 6:20; Hos 5:8Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita

na kusikia sauti za tarumbeta?

224:22 1Kor 14:20; Yer 5:21; 13:23; Za 36:3; Rum 16:19; Yer 5:21; 10:8; Za 14:4“Watu wangu ni wapumbavu,

hawanijui mimi.

Ni watoto wasio na akili,

hawana ufahamu.

Ni hodari kutenda mabaya,

hawajui kutenda yaliyo mema.”

234:23 Ay 9:7; 30:26; Isa 5:30; 59:9; Mao 3:2Niliitazama dunia,

nayo haikuwa na umbo tena ni tupu;

niliziangalia mbingu,

mianga ilikuwa imetoweka.

244:24 Eze 38:20; Ay 9:6; Isa 5:25; Kut 19:18Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka,

vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.

254:25 Hos 4:3; Sef 1:3; Yer 7:20Nilitazama, wala watu hawakuwepo;

kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.

26Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa,

miji yake yote ilikuwa magofu

mbele za Bwana,

mbele ya hasira yake kali.

274:27 Amo 9:8; Yer 5:10; 12:12; Eze 20:17; Yer 46:28Hivi ndivyo Bwana asemavyo:

“Nchi yote itaharibiwa,

ingawa sitaiangamiza kabisa.

284:28 Yer 14:2; Hos 4:3; Hes 23:19; Isa 5:30; Yer 30:24; 23:20; 12:4-11Kwa hiyo dunia itaomboleza

na mbingu zilizo juu zitakuwa giza,

kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma,

nimeamua na wala sitageuka.”

294:29 Yer 8:16; Isa 6:12; 2Fal 25:4; Yer 6:23; 1Sam 26:20; Kut 33:22Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde

kila mji unakimbia.

Baadhi wanakimbilia vichakani,

baadhi wanapanda juu ya miamba.

Miji yote imeachwa,

hakuna aishiye ndani yake.

304:30 Isa 10:3-4; Eze 16:11; 23:40; 2Fal 9:30; Ay 19:14; Eze 23:9; Za 35:4Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa?

Kwa nini unajivika vazi jekundu

na kuvaa vito vya dhahabu?

Kwa nini unapaka macho yako rangi?

Unajipamba bure.

Wapenzi wako wanakudharau,

wanautafuta uhai wako.

314:31 Mwa 3:16; Mik 4:10; Isa 42:14; Mao 1:17; Yer 6:24; 13:21; 22:23; Za 9:14; Isa 42:14; Kum 32:25; Mao 2:21Nasikia kilio kama cha mwanamke

katika utungu wa kuzaa,

kilio cha uchungu kama cha anayemzaa

mtoto wake wa kwanza:

kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua,

akiinua mikono yake, akisema,

“Ole wangu! Ninazimia;

maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

耶利米书 4:1-31

1耶和华说:“以色列啊,

如果你回转,

回转归向我,

从我眼前除掉可憎的神像,

不再离开我;

2如果你本着诚实、正直、公义,

凭永活的耶和华起誓,

你必成为万国的祝福,

得到他们的尊敬4:2 “你必成为万国的祝福,得到他们的尊敬”或译“万国必得到耶和华的祝福,并以祂为荣”。。”

3耶和华对犹大人和耶路撒冷人说:

“要开垦你们的荒地,

不要在荆棘中撒种。

4犹大人和耶路撒冷的居民啊,

你们要自行割礼,

除掉心中的污垢,归向耶和华。

不然,我必因你们的恶行而发烈怒,如火燃烧,

无人能够扑灭。

5“你们要在犹大传讲,在耶路撒冷宣告,

‘要在全国吹响号角。’

高声呼喊,

‘要集合起来,

我们要逃进坚城。’

6你们要向锡安举起旗帜,

赶快逃亡,不要迟延,

因为我要从北方降下灾祸,

大肆毁灭。”

7毁灭列国者已出动,

如狮子冲出巢穴,

要使你们的土地荒凉,

城邑沦为废墟,无人居住。

8为此,你们要腰束麻布,

嚎啕大哭,

因为耶和华向我们发的烈怒还没有止息。

9耶和华说:“到那天,君王必吓坏,官长必丧胆,祭司和先知必惊骇。” 10我说:“唉!主耶和华啊,你完全欺骗了这群百姓和耶路撒冷人,因为你说,‘你们会安享太平。’其实剑锋已抵着他们的咽喉了。”

11那时,耶和华必对这群百姓和耶路撒冷人说:“一阵热风从荒野光秃的山头吹向我的子民,不是为扬场、吹净糠秕。 12那是我发出的一阵强风。现在我要宣告我对他们的审判。”

13看啊,仇敌必如云涌来,

他的战车快如旋风,

他的战马比飞鹰还快。

我们有祸了!

我们灭亡了!

14耶路撒冷啊,

要洗去你内心的邪恶,

这样你才能得救。

你心怀恶念要到何时呢?

15传来消息,

以法莲山区报出恶讯。

16耶和华说:“你们去通知列国,

耶路撒冷宣告,

‘围攻的人从远方来,

犹大的城邑高声喊杀,

17像看守田园一样包围耶路撒冷

因为耶路撒冷背叛了我。’

这是耶和华说的。

18你的所作所为给你招致这灾祸,

你是罪有应得,你会痛彻心肺!”

19我的心啊,我的心啊!

我伤心欲绝,烦躁不安。

我无法保持缄默,

因为我听见了号角声和战争的呐喊。

20恶讯频传,山河破碎,

我的帐篷忽然倒塌,

幔子顷刻破裂。

21我还要看这旌旗、

听这号声到何时呢?

22耶和华说:“我的子民愚顽,

不认识我,

是蒙昧无知的儿女,

善于行恶,不知行善。”

23我俯瞰大地,

只见一片空虚混沌;

我观看天空,毫无亮光。

24我眺望群山,只见大山在颤抖,

小山在摇晃。

25我四下观看,只见杳无人烟,

飞鸟绝迹。

26我四下观看,只见良田变荒野,

城邑都在耶和华的烈怒下沦为废墟。

27耶和华说:“遍地将要荒凉,

然而我不会彻底毁灭大地。

28因此,地要悲哀,

天要昏暗,

因为我言出必行,

我心意已决,绝不反悔。”

29各城的人听到骑兵和弓箭手的呐喊,

都纷纷逃命。

有的跑入丛林,有的爬进岩洞。

各城荒弃,无人居住。

30你这荒凉的城啊!

你在做什么?

纵然你穿上红袍,

戴上金饰,

描眉画眼,

又有什么用呢?

你的情人藐视你,

要杀害你。

31我听见好像妇人分娩时的喊叫声,

好像妇人生头胎时的痛苦呻吟。

那是少女锡安的喊叫声,

她在喘息,伸出双手说:

“噢!我有祸了,

我要死在杀戮者手上了。”