Yeremia 38 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 38:1-28

Yeremia Atupwa Kwenye Kisima

138:1 Yer 37:3; Mdo 4:2; 1Nya 9:12Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema, 238:2 Yer 34:17; 11:21; 45:5; 21:9; 38:19; Mt 24:7-8“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’ 338:3 Yer 21:10; 32:3Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’ ”

438:4 Yer 36:12; 11:21; 26:11; Za 37:12-40; Amo 7:10; 1Sam 17:32Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”

538:5 Yer 26:14; 1Sam 15:24Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”

638:6 Yer 37:21; Mao 3:53; Mk 9:42; Yos 2:15; Mwa 37:24; Ay 30:9Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.

738:7 Yer 39:16; Isa 56:3-5; Mdo 8:27; Ay 29:7Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini, 8Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia, 938:9 Yer 37:21; Mwa 37:20“Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”

10Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”

11Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. 12Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo, 1338:13 Yer 37:21; 2Kor 6:4-5nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.

Sedekia Amhoji Yeremia Tena

1438:14 1Sam 3:17; Za 82:4; Yer 37:3Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”

15Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”

1638:16 Yer 37:17; Hes 16:22; Isa 42:5; 57:16; Ebr 12:9Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”

1738:17 2Fal 24:12; Yer 21:8-10; 27:8Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi. 1838:18 Yer 34:3; 37:8; 24:8; 32:4Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’ ”

1938:19 Isa 51:12; Yn 12:42; Yer 52:15; 1Sam 31:4; Yer 39:9Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”

2038:20 Yer 11:4; Isa 55:3; 2Kor 5:20; Kum 5:33; Yer 40:9Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama. 21Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia: 2238:22 Yer 6:12; Ay 19:14; Yer 13:21; Ay 30:19; Za 69:14Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia:

“ ‘Walikupotosha na kukushinda,

wale rafiki zako uliowaamini.

Miguu yako imezama matopeni;

rafiki zako wamekuacha.’

2338:23 2Fal 25:6; Yer 24:8; 41:10; 32:4; Eze 17:15; Yer 21:10; 37:8“Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”

2438:24 Yer 37:17-21Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa. 25Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’ 2638:26 Yer 37:15, 20; 39:14; 1Sam 16:2basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’ ”

27Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.

28Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.

New International Version

Jeremiah 38:1-28

Jeremiah Thrown Into a Cistern

1Shephatiah son of Mattan, Gedaliah son of Pashhur, Jehukal38:1 Hebrew Jukal, a variant of Jehukal son of Shelemiah, and Pashhur son of Malkijah heard what Jeremiah was telling all the people when he said, 2“This is what the Lord says: ‘Whoever stays in this city will die by the sword, famine or plague, but whoever goes over to the Babylonians38:2 Or Chaldeans; also in verses 18, 19 and 23 will live. They will escape with their lives; they will live.’ 3And this is what the Lord says: ‘This city will certainly be given into the hands of the army of the king of Babylon, who will capture it.’ ”

4Then the officials said to the king, “This man should be put to death. He is discouraging the soldiers who are left in this city, as well as all the people, by the things he is saying to them. This man is not seeking the good of these people but their ruin.”

5“He is in your hands,” King Zedekiah answered. “The king can do nothing to oppose you.”

6So they took Jeremiah and put him into the cistern of Malkijah, the king’s son, which was in the courtyard of the guard. They lowered Jeremiah by ropes into the cistern; it had no water in it, only mud, and Jeremiah sank down into the mud.

7But Ebed-Melek, a Cushite,38:7 Probably from the upper Nile region an official38:7 Or a eunuch in the royal palace, heard that they had put Jeremiah into the cistern. While the king was sitting in the Benjamin Gate, 8Ebed-Melek went out of the palace and said to him, 9“My lord the king, these men have acted wickedly in all they have done to Jeremiah the prophet. They have thrown him into a cistern, where he will starve to death when there is no longer any bread in the city.”

10Then the king commanded Ebed-Melek the Cushite, “Take thirty men from here with you and lift Jeremiah the prophet out of the cistern before he dies.”

11So Ebed-Melek took the men with him and went to a room under the treasury in the palace. He took some old rags and worn-out clothes from there and let them down with ropes to Jeremiah in the cistern. 12Ebed-Melek the Cushite said to Jeremiah, “Put these old rags and worn-out clothes under your arms to pad the ropes.” Jeremiah did so, 13and they pulled him up with the ropes and lifted him out of the cistern. And Jeremiah remained in the courtyard of the guard.

Zedekiah Questions Jeremiah Again

14Then King Zedekiah sent for Jeremiah the prophet and had him brought to the third entrance to the temple of the Lord. “I am going to ask you something,” the king said to Jeremiah. “Do not hide anything from me.”

15Jeremiah said to Zedekiah, “If I give you an answer, will you not kill me? Even if I did give you counsel, you would not listen to me.”

16But King Zedekiah swore this oath secretly to Jeremiah: “As surely as the Lord lives, who has given us breath, I will neither kill you nor hand you over to those who want to kill you.”

17Then Jeremiah said to Zedekiah, “This is what the Lord God Almighty, the God of Israel, says: ‘If you surrender to the officers of the king of Babylon, your life will be spared and this city will not be burned down; you and your family will live. 18But if you will not surrender to the officers of the king of Babylon, this city will be given into the hands of the Babylonians and they will burn it down; you yourself will not escape from them.’ ”

19King Zedekiah said to Jeremiah, “I am afraid of the Jews who have gone over to the Babylonians, for the Babylonians may hand me over to them and they will mistreat me.”

20“They will not hand you over,” Jeremiah replied. “Obey the Lord by doing what I tell you. Then it will go well with you, and your life will be spared. 21But if you refuse to surrender, this is what the Lord has revealed to me: 22All the women left in the palace of the king of Judah will be brought out to the officials of the king of Babylon. Those women will say to you:

“ ‘They misled you and overcame you—

those trusted friends of yours.

Your feet are sunk in the mud;

your friends have deserted you.’

23“All your wives and children will be brought out to the Babylonians. You yourself will not escape from their hands but will be captured by the king of Babylon; and this city will38:23 Or and you will cause this city to be burned down.”

24Then Zedekiah said to Jeremiah, “Do not let anyone know about this conversation, or you may die. 25If the officials hear that I talked with you, and they come to you and say, ‘Tell us what you said to the king and what the king said to you; do not hide it from us or we will kill you,’ 26then tell them, ‘I was pleading with the king not to send me back to Jonathan’s house to die there.’ ”

27All the officials did come to Jeremiah and question him, and he told them everything the king had ordered him to say. So they said no more to him, for no one had heard his conversation with the king.

28And Jeremiah remained in the courtyard of the guard until the day Jerusalem was captured.

The Fall of Jerusalem

This is how Jerusalem was taken: