Yeremia 37 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 37:1-21

Yeremia Gerezani

137:1 2Fal 14:17; 1Nya 3:16; Eze 17:13; 2Nya 36:10; 24:8, 12; Yer 22:24Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini37:1 Yehoyakini ni jina jingine la Yekonia au Konia. mwana wa Yehoyakimu. 237:2 2Fal 24:19; 2Nya 36:12-14; Mit 29:12Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.

337:3 2Fal 25:18; Yer 52:24; Hes 21:7; 1Sam 12:19; Yer 38:14; Kut 8:28; 1Fal 13:6Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”

437:4 Yer 32:2Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani. 537:5 Mwa 15; 18; Yer 34:21; 31:1; Isa 30:5; 2Fal 24:7; Eze 17:15Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.

6Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema: 737:7 Mwa 25:22; 2Fal 22:18; 18:21; Yer 2:12; 36; Mao 4:17“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri. 837:8 Yer 21:10; 39; 8; Mit 21:30; Yer 38:3, 8Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’

937:9 Yer 29:8; Mk 13:5“Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha! 1037:10 Law 26:36-38; Isa 30:17; Yer 21:4-5, 10Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”

11Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao, 1237:12 Yer 32:9Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko. 1337:13 Yer 20:2; 21:9Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”

1437:14 Isa 58:6; Yer 40:4Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa. 1537:15 Yer 20:2; 38:26; Ebr 11:36; Mdo 5:40; 12:6; 1Fal 22:27Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.

16Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu. 1737:17 Yer 15:11; 38:16; 21:7; Mwa 25:22Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?”

Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”

1837:18 1Sam 16:18; Yn 10:32; Mdo 25:8Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani? 1937:19 Yer 14:13; Eze 13:2Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’ 20Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”

2137:21 Law 26:26; 2Kor 4; 6; Isa 33:16; 2Fal 25:3; Yer 52:6; 39:13-14Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.

New International Version

Jeremiah 37:1-21

Jeremiah in Prison

1Zedekiah son of Josiah was made king of Judah by Nebuchadnezzar king of Babylon; he reigned in place of Jehoiachin37:1 Hebrew Koniah, a variant of Jehoiachin son of Jehoiakim. 2Neither he nor his attendants nor the people of the land paid any attention to the words the Lord had spoken through Jeremiah the prophet.

3King Zedekiah, however, sent Jehukal son of Shelemiah with the priest Zephaniah son of Maaseiah to Jeremiah the prophet with this message: “Please pray to the Lord our God for us.”

4Now Jeremiah was free to come and go among the people, for he had not yet been put in prison. 5Pharaoh’s army had marched out of Egypt, and when the Babylonians37:5 Or Chaldeans; also in verses 8, 9, 13 and 14 who were besieging Jerusalem heard the report about them, they withdrew from Jerusalem.

6Then the word of the Lord came to Jeremiah the prophet: 7“This is what the Lord, the God of Israel, says: Tell the king of Judah, who sent you to inquire of me, ‘Pharaoh’s army, which has marched out to support you, will go back to its own land, to Egypt. 8Then the Babylonians will return and attack this city; they will capture it and burn it down.’

9“This is what the Lord says: Do not deceive yourselves, thinking, ‘The Babylonians will surely leave us.’ They will not! 10Even if you were to defeat the entire Babylonian37:10 Or Chaldean; also in verse 11 army that is attacking you and only wounded men were left in their tents, they would come out and burn this city down.”

11After the Babylonian army had withdrawn from Jerusalem because of Pharaoh’s army, 12Jeremiah started to leave the city to go to the territory of Benjamin to get his share of the property among the people there. 13But when he reached the Benjamin Gate, the captain of the guard, whose name was Irijah son of Shelemiah, the son of Hananiah, arrested him and said, “You are deserting to the Babylonians!”

14“That’s not true!” Jeremiah said. “I am not deserting to the Babylonians.” But Irijah would not listen to him; instead, he arrested Jeremiah and brought him to the officials. 15They were angry with Jeremiah and had him beaten and imprisoned in the house of Jonathan the secretary, which they had made into a prison.

16Jeremiah was put into a vaulted cell in a dungeon, where he remained a long time. 17Then King Zedekiah sent for him and had him brought to the palace, where he asked him privately, “Is there any word from the Lord?”

“Yes,” Jeremiah replied, “you will be delivered into the hands of the king of Babylon.”

18Then Jeremiah said to King Zedekiah, “What crime have I committed against you or your attendants or this people, that you have put me in prison? 19Where are your prophets who prophesied to you, ‘The king of Babylon will not attack you or this land’? 20But now, my lord the king, please listen. Let me bring my petition before you: Do not send me back to the house of Jonathan the secretary, or I will die there.”

21King Zedekiah then gave orders for Jeremiah to be placed in the courtyard of the guard and given a loaf of bread from the street of the bakers each day until all the bread in the city was gone. So Jeremiah remained in the courtyard of the guard.