Yeremia 36 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 36:1-32

Yehoyakimu Achoma Kitabu Cha Yeremia

136:1 2Nya 36:5Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema: 236:2 Yer 25:3; Za 40:7; Hab 2:2; Kut 17:14; Eze 2:7; 25:3“Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa. 336:3 Eze 12:3; Amo 5:15; Isa 6:9; Yer 18:8; Mdo 3:19; Yn 3:8; Mk 14:8; Mdo 26:20; Mk 4:12; 2Fal 17:13Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”

436:4 Yer 32:12; Zek 5:1; Yer 45; 1; Eze 2:9; Yer 51:59Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu. 5Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana. 636:6 Kut 4:16; 2Nya 20:4Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao. 736:7 Yer 26:3; Kum 31:17; 29:18; Yer 37:20Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”

8Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu. 936:9 2Nya 20:3; Amu 20:26Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda. 1036:10 Yer 52:25; Mwa 23:10; Yer 26:10; 29:3; 26:24Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.

11Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu, 1236:12 Yer 26:22; 2Sam 8:17; Yer 38:4alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote. 13Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu, 14maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake. 15Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.”

Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu. 16Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.” 17Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”

1836:18 Isa 8:12; Mt 10:16-32; 1Pet 3:14-15Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”

1936:19 1Fal 17:3; Yer 26:16Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”

20Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu. 2136:21 2Fal 22:10Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme. 2236:22 Amo 3:15; Amu 3:20Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto. 2336:23 1Fal 22:8; 2Tim 4:3Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea. 2436:24 Hes 14:6; 2Fal 22:11; Isa 36:22; Mwa 37:29Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao. 2536:25 Mwa 37:26; Rum 8:34Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza. 2636:26 Mt 23:34; 1Fal 17:3; Za 11:1Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.

27Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema: 28“Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto. 2936:29 Isa 30:10; Amo 5:10; Yer 33:12Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?” 3036:30 Isa 14:19; Yer 22:19; 52:2; 8:2; 2Fal 24:6Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku. 3136:31 Kut 20:5; Mit 29:1; 1:24Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’ ”

3236:32 Kut 34:1; Yer 30:2; Kut 4:15; Rum 16:22Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.

New International Version

Jeremiah 36:1-32

Jehoiakim Burns Jeremiah’s Scroll

1In the fourth year of Jehoiakim son of Josiah king of Judah, this word came to Jeremiah from the Lord: 2“Take a scroll and write on it all the words I have spoken to you concerning Israel, Judah and all the other nations from the time I began speaking to you in the reign of Josiah till now. 3Perhaps when the people of Judah hear about every disaster I plan to inflict on them, they will each turn from their wicked ways; then I will forgive their wickedness and their sin.”

4So Jeremiah called Baruch son of Neriah, and while Jeremiah dictated all the words the Lord had spoken to him, Baruch wrote them on the scroll. 5Then Jeremiah told Baruch, “I am restricted; I am not allowed to go to the Lord’s temple. 6So you go to the house of the Lord on a day of fasting and read to the people from the scroll the words of the Lord that you wrote as I dictated. Read them to all the people of Judah who come in from their towns. 7Perhaps they will bring their petition before the Lord and will each turn from their wicked ways, for the anger and wrath pronounced against this people by the Lord are great.”

8Baruch son of Neriah did everything Jeremiah the prophet told him to do; at the Lord’s temple he read the words of the Lord from the scroll. 9In the ninth month of the fifth year of Jehoiakim son of Josiah king of Judah, a time of fasting before the Lord was proclaimed for all the people in Jerusalem and those who had come from the towns of Judah. 10From the room of Gemariah son of Shaphan the secretary, which was in the upper courtyard at the entrance of the New Gate of the temple, Baruch read to all the people at the Lord’s temple the words of Jeremiah from the scroll.

11When Micaiah son of Gemariah, the son of Shaphan, heard all the words of the Lord from the scroll, 12he went down to the secretary’s room in the royal palace, where all the officials were sitting: Elishama the secretary, Delaiah son of Shemaiah, Elnathan son of Akbor, Gemariah son of Shaphan, Zedekiah son of Hananiah, and all the other officials. 13After Micaiah told them everything he had heard Baruch read to the people from the scroll, 14all the officials sent Jehudi son of Nethaniah, the son of Shelemiah, the son of Cushi, to say to Baruch, “Bring the scroll from which you have read to the people and come.” So Baruch son of Neriah went to them with the scroll in his hand. 15They said to him, “Sit down, please, and read it to us.”

So Baruch read it to them. 16When they heard all these words, they looked at each other in fear and said to Baruch, “We must report all these words to the king.” 17Then they asked Baruch, “Tell us, how did you come to write all this? Did Jeremiah dictate it?”

18“Yes,” Baruch replied, “he dictated all these words to me, and I wrote them in ink on the scroll.”

19Then the officials said to Baruch, “You and Jeremiah, go and hide. Don’t let anyone know where you are.”

20After they put the scroll in the room of Elishama the secretary, they went to the king in the courtyard and reported everything to him. 21The king sent Jehudi to get the scroll, and Jehudi brought it from the room of Elishama the secretary and read it to the king and all the officials standing beside him. 22It was the ninth month and the king was sitting in the winter apartment, with a fire burning in the firepot in front of him. 23Whenever Jehudi had read three or four columns of the scroll, the king cut them off with a scribe’s knife and threw them into the firepot, until the entire scroll was burned in the fire. 24The king and all his attendants who heard all these words showed no fear, nor did they tear their clothes. 25Even though Elnathan, Delaiah and Gemariah urged the king not to burn the scroll, he would not listen to them. 26Instead, the king commanded Jerahmeel, a son of the king, Seraiah son of Azriel and Shelemiah son of Abdeel to arrest Baruch the scribe and Jeremiah the prophet. But the Lord had hidden them.

27After the king burned the scroll containing the words that Baruch had written at Jeremiah’s dictation, the word of the Lord came to Jeremiah: 28“Take another scroll and write on it all the words that were on the first scroll, which Jehoiakim king of Judah burned up. 29Also tell Jehoiakim king of Judah, ‘This is what the Lord says: You burned that scroll and said, “Why did you write on it that the king of Babylon would certainly come and destroy this land and wipe from it both man and beast?” 30Therefore this is what the Lord says about Jehoiakim king of Judah: He will have no one to sit on the throne of David; his body will be thrown out and exposed to the heat by day and the frost by night. 31I will punish him and his children and his attendants for their wickedness; I will bring on them and those living in Jerusalem and the people of Judah every disaster I pronounced against them, because they have not listened.’ ”

32So Jeremiah took another scroll and gave it to the scribe Baruch son of Neriah, and as Jeremiah dictated, Baruch wrote on it all the words of the scroll that Jehoiakim king of Judah had burned in the fire. And many similar words were added to them.