Yeremia 34 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 34:1-22

Onyo Kwa Sedekia

134:1 Yer 27:7; 2Fal 25:1; Yer 39:1; Dan 2:37Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 234:2 2Nya 36:11; Yer 32:29; 37:8“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto. 334:3 Yer 32:4; 21:7; 2Fal 25:7Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.

434:4 Yer 52:11“ ‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga, 534:5 2Nya 16:14utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’ ”

6Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu, 734:7 Yos 10:3-10; 2Nya 11:9; 2Fal 18:13wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.

Uhuru Kwa Watumwa

834:8 2Fal 11:17; Kut 21:2; Neh 5:5-8; Law 25:39-41Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa. 934:9 Law 25:39-46; Kum 15:12-18; Neh 5:11Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa. 10Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru. 11Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.

12Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 1334:13 Kut 24:8; Kum 15:15“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema, 1434:14 Kut 21:2; Law 25:39; Kum 15:12; 2Fal 17:14; Yer 7:26‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali. 1534:15 Yer 7:10-11; 32:34; Neh 10:29Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu. 1634:16 Eze 3:20; 18:24; Kut 20:7; Law 19:12Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.

1734:17 Mt 7:2; Gal 6:7; Yer 15:4; Kum 28:25, 64; Yer 21:7; 14:12; 29:18; 24:9“Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia. 1834:18 Mwa 15:10; Rum 2:8; Yer 11:10Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama. 1934:19 Yer 26:10; Sef 3:3-4Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama, 2034:20 Eze 16:27; 23:28; Yer 11:21; 7:33; 21:7; Kum 28:25, 64nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.

2134:21 Yer 32:4; 52:24-27; 37:5; 39:6; 2Fal 25:21“Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu. 2234:22 Yer 39:1-2; 37:8; 38:18; Neh 2:17; Mik 7:13; Eze 23:47Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

耶利米書 34:1-22

給西底迦的警告

1巴比倫尼布甲尼撒率領他的軍隊和他統治的各邦國攻打耶路撒冷及其周圍城邑時,耶和華對耶利米說: 2「以色列的上帝耶和華這樣說,『你去告訴猶大西底迦以色列的上帝耶和華說:看啊,我要把這城交在巴比倫王的手中,他要將城付之一炬。 3你必逃不出巴比倫王的手心,你必被抓,落入他手中。你必和巴比倫王面對面、眼對眼地說話,然後被帶到巴比倫4猶大西底迦啊!你要聽耶和華關於你的話。耶和華說:你必不會死在刀劍之下, 5你必安然去世。人們必為你燒香,像為你的先王燒香一樣,他們必為你哀悼說,唉,我主啊!』這是我耶和華說的。」

6耶利米先知就在耶路撒冷把這番話告訴了猶大西底迦7那時,巴比倫王的軍隊正攻打耶路撒冷以及猶大僅存的兩座堅城拉吉亞西加

8耶和華的話傳給耶利米之前,西底迦王與耶路撒冷的居民立約,宣佈釋放自己的奴隸。 9各人都要釋放自己的希伯來男女奴隸,誰都不應使自己的希伯來同胞做奴隸。 10所有立約的首領和人民都答應守約,不再奴役他們。他們按約釋放了自己的男女奴隸。 11但事後他們卻反悔,抓回先前釋放的男女奴隸,再次奴役他們。 12那時,耶和華對耶利米說: 13以色列的上帝耶和華這樣說,『我曾帶領你們的祖先離開埃及,使他們不再受奴役,那時我與他們立約說, 14如果你們的希伯來同胞賣身做你們的奴隸,服侍你們六年後,到第七年你們要給他們自由。34·14 申命記15·12你們的祖先卻掩耳不聽。 15不久前,你們回心轉意,做我視為正的事,釋放自己的同胞,並且在我的殿中當著我的面立了約。 16然而,你們卻反悔,各自抓回先前釋放的男女奴隸,再次奴役他們,褻瀆了我的名。 17因此耶和華說,既然你們不聽我的話,不給自己的同胞自由,看啊,我必給你們自由,使你們自由地死於刀劍、瘟疫和饑荒,使你們的遭遇令天下萬國驚懼。這是耶和華說的。 18-19猶大耶路撒冷的官員、宮廷侍臣、祭司和全體百姓曾把牛犢劈成兩半,從中間走過跟我立約,後來卻又違背跟我立的約,不守在我面前所立之約的規定,所以我必使他們的下場像他們劈開的牛犢一樣。 20我要把他們交在想殺他們的敵人手中,他們的屍體要成為飛禽走獸的食物。 21我要把猶大西底迦及其官員交在想殺他們的敵人手中,交在剛撤軍的巴比倫王手中。 22看啊,我要吩咐他們回來攻佔這城,將它付之一炬,我要使猶大的城邑荒無人煙。這是耶和華說的。』」