Yeremia 30 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 30:1-24

Kurudishwa Kwa Israeli

1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 230:2 Isa 30:8; Yer 36:2“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe. 330:3 Yer 29:14; 16:15; Amo 9:14; Yer 24:6Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”

4Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda: 530:5 Yer 6:25“Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Vilio vya woga vinasikika:

hofu kuu, wala si amani.

630:6 Yer 4:31; Isa 29:22Ulizeni na mkaone:

Je, mwanaume aweza kuzaa watoto?

Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu

ameweka mikono yake tumboni

kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa,

kila uso ukigeuka rangi kabisa?

730:7 Isa 2:12; Amo 5:18; Yoe 2:11; Isa 22:5; Sef 1:15; Yer 23:3Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha!

Hakutakuwa na nyingine mfano wake.

Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo,

lakini ataokolewa kutoka hiyo.

830:8 Isa 9:4; Yer 25:14; Eze 34:27; Yer 27:7; Za 107:14“ ‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote,

‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao

na kuvipasua vifungo vyao;

wageni hawatawafanya tena watumwa.

930:9 Isa 55:3-4; 1Sam 13:14; Hos 1:11; 3:5; Yer 33:15; Eze 34:23-24Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao

na Daudi mfalme wao,

nitakayemwinua kwa ajili yao.

1030:10 Isa 41:10-13; 43:5; Yer 29:14; Isa 35:9; Yer 17:25; Isa 29:22; Eze 34:25-28“ ‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

usifadhaike, ee Israeli,’

asema Bwana.

‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali,

wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao.

Yakobo atakuwa tena na amani na usalama,

wala hakuna atakayemtia hofu.

1130:11 Law 26:44; Yer 4:27; 10:24; Hos 11:9; Amo 9:8; Yer 5:18; Isa 29:22; Eze 34:25-28Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’

asema Bwana.

‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote

ambamo miongoni mwao nimewatawanya,

sitawaangamiza ninyi kabisa.

Nitawaadhibu, lakini kwa haki.

Sitawaacha kabisa bila adhabu.’

1230:12 Yer 8:22; 15:18; Ay 6:4; Yer 10:19“Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Kidonda chako hakina dawa,

jeraha lako haliponyeki.

1330:13 Nah 3:19; Amu 6:31; Yer 14:19; 8:22; 46:11Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako,

hakuna dawa ya kidonda chako,

wewe hutapona.

1430:14 Yer 22:20; Ay 13:24; 30:21; Yer 25:7; Mao 1:2Wale walioungana nawe wote wamekusahau,

hawajali chochote kukuhusu wewe.

Nimekupiga kama vile adui angelifanya,

na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya,

kwa sababu hatia yako ni kubwa mno

na dhambi zako ni nyingi sana.

1530:15 Yer 10:19; Mit 1:31Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako,

yale maumivu yako yasiyoponyeka?

Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi

nimekufanyia mambo haya.

1630:16 Kum 23:22; Yoe 3:4-8; Isa 29:8; Yer 10:25; Isa 14:2; Yer 49:2; 50:10“ ‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa;

adui zako wote watakwenda uhamishoni.

Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara;

wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.

1730:17 Isa 6:12; Yer 33:24; Kut 15:26; Za 142:4Lakini nitakurudishia afya yako

na kuyaponya majeraha yako,’

asema Bwana,

‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa,

Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’

1830:18 Kum 30:3; Yer 32:44; Za 103:13; Eze 39:25; 36:10; Yer 31:23; Hes 24:5“Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo,

na kuhurumia maskani yake.

Mji utajengwa tena juu ya magofu yake,

nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.

1930:19 Neh 8:12; Mwa 15:5; Isa 51:3, 11; 60:9; Yer 31:4; Isa 35:10; 44:23; Zek 2:4Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao

na sauti ya furaha.

Nitaiongeza idadi yao

wala hawatapungua,

nitawapa heshima

na hawatadharauliwa.

2030:20 Isa 54:13-14; Zek 8:5; Yer 31:17; Kut 23:22Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa

siku za zamani,

nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu;

nitawaadhibu wale wote wawaoneao.

2130:21 Yer 23:5-6; Hes 16:5; Kum 17:15Mmoja wao atakuwa kiongozi wao;

mtawala wao atainuka miongoni mwao.

Nitamleta karibu nami,

naye atanikaribia mimi,

kwa maana ni nani yule atakayejitolea

kuwa karibu nami?’

asema Bwana.

2230:22 Isa 19:25; Hos 2:23; Law 26:12‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu,

nami nitakuwa Mungu wenu.’ ”

2330:23 Yer 23:19; 25:32Tazama, tufani ya Bwana

italipuka kwa ghadhabu,

upepo wa kisulisuli uendao kasi

utashuka juu ya vichwa vya waovu.

2430:24 Yer 4:8; Mao 1:12; Yer 4:28; 23:19-20Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma

mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake.

Siku zijazo

mtayaelewa haya.

Het Boek

Jeremia 30:1-24

1Het woord, dat door Jahweh tot Jeremias werd gericht: 2Zo spreekt Jahweh, Israëls God! Schrijf alle woorden, die Ik tot u ga spreken, op in een boek. 3Want zie, de dagen zullen komen, is de godsspraak van Jahweh, dat Ik een einde zal maken aan de ballingschap van Israël en Juda, mijn volk, zegt Jahweh; dat Ik ze terugbreng naar het land, dat Ik hun vaderen heb geschonken, en dat ze het in bezit zullen nemen. 4Dit zijn de woorden, die Jahweh over Israël en Juda heeft gesproken: 5Zo spreekt Jahweh! Een angstgeschrei wordt gehoord, Benauwende schrik! 6Vraagt en ziet, Of mannen soms baren? Waarom dan zie ik iederen man Met de handen op de heupen als een barende vrouw? Waarom zijn alle gezichten vertrokken, Doodsbleek geworden? 7Wee, hoe geweldig die dag; Zo is er geen ander! Een angsttijd voor Jakob: Maar hij zal er uit worden gered! 8Op die dag: spreekt Jahweh der heirscharen, Breek Ik het juk van hun nek, En scheur hun banden vaneen. Niet langer zullen vreemden ze knechten; 9Maar Jahweh zullen ze dienen, hun God, En David, hun koning, dien Ik hun zal verwekken. 10Jakob, mijn dienaar, wees niet bang, Spreekt Jahweh; Israël, ge behoeft niet te vrezen; Want Ik ga u verlossen uit verre gewesten, Uw kroost uit het land hunner ballingschap! Jakob keert terug, en vindt weer zijn rust, Onbekommerd, door niemand verschrikt. 11Want Ik ben met u, om u te redden, spreekt Jahweh! Ja, Ik ga alle volken vernielen, Waaronder Ik u heb verstrooid. Maar u zal Ik nimmer vernielen, Ik tuchtig u enkel, zoals ge verdient; 12Neen, Ik laat u niet ongestraft! Zo spreekt Jahweh: Uw plaag is ontzettend, En schrijnend uw wonde; 13Niemand wil uw zweren verbinden, Geneesmiddelen helpen u niet. 14Al uw minnaars zijn u vergeten, En bekommeren zich niet meer om u. Want Ik heb u als een vijand onbarmhartig geslagen, Om uw grote schuld, en uw talloze zonden. 15Wat krijt ge dan zo om uw wonden, En uw ontzettende plaag? Om uw grote schuld, en uw talloze zonden Heb Ik u dit berokkend! 16Waarachtig, die u verslinden, Worden allen verslonden; En al uw verdrukkers Zullen in ballingschap gaan; Uw plunderaars worden geplunderd, Uw rovers zal Ik beroven! 17Dan sluit Ik uw wonde, En genees uw kwalen, Is de godsspraak van Jahweh; Omdat men u Verstoteling noemt: Dit is Sion, om wien zich niemand bekommert! Zo spreekt Jahweh! 18Zie, Ik maak de tenten van Jakob gelukkig, En ontferm Mij over zijn stulpen; De stad wordt herbouwd op haar heuvel, De burcht troont weer op zijn oude plaats;, 19Er stijgen jubelzangen uit op, En vrolijke kreten. Ik vermeerder ze weer: zij verminderen niet; Ik herstel ze in ere: men veracht ze niet meer; 20Zijn zonen zullen weer worden als vroeger, Zijn gemeente zal voor mijn aangezicht staan; Al zijn verdrukkers zal Ik bestraffen, Hij wordt weer sterker dan zij! 21Zijn vorst staat uit zijn midden op; Ik laat hem komen: hij mag Mij naderen; Wie anders zou zijn leven wagen, Om Mij te naderen, spreekt Jahweh! 22Zo zult gij mijn volk, En Ik zal uw God zijn! 23Zie, de storm van Jahweh komt, De gramschap barst los als een wervelwind, Op het hoofd van de bozen stort zij zich uit. 24De toorn van Jahweh legt zich niet neer, Eer Hij zijn plannen heeft ten uitvoer gebracht: Ten leste zult ge het zelf ondervinden!