Yeremia 27 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 27:1-22

Yuda Kumtumikia Nebukadneza

127:1 2Nya 36:11; Yer 28:1Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 227:2 Law 26:13; Yer 28:10-13; 1Fal 22:11Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Tengeneza nira, ujivike shingoni mwako, uifunge kwa kamba za ngozi. 327:3 Yer 25:17, 21; Mwa 10:15; Yer 25:21-22Kisha utume ujumbe kwa wafalme wa Edomu, Moabu, Amoni, Tiro na Sidoni kupitia wajumbe ambao wamekuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda. 4Wape ujumbe kwa ajili ya mabwana zao na uwaambie: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Waambieni hivi mabwana zenu: 527:5 Kum 9:29; Za 115:16; Dan 4:17; Mwa 1:25Kwa uwezo wangu mkuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa nimeumba dunia na watu wake na wanyama walioko ndani yake, nami humpa yeyote inipendezavyo. 627:6 Yer 25:9; 21:7; Eze 29:18-20; Dan 2:37-38; Yer 28:14Sasa nitazitia nchi zenu zote mkononi mwa mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, na nitawafanya hata wanyama wa mwituni wamtumikie. 727:7 Dan 5:18, 28; Yer 25:12; 2Nya 36:20; Yer 51:47; 25:14Mataifa yote yatamtumikia yeye, pamoja na mwanawe na mwana wa mwanawe, hadi wakati wa nchi yake utakapowadia, kisha mataifa mengi na wafalme wenye nguvu nyingi watamshinda.

8“ ‘ “Lakini kama kukiwa na taifa lolote au ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babeli, ama kuinamisha shingo yake chini ya nira yake, nitaliadhibu taifa hilo kwa upanga, njaa na tauni, asema Bwana, mpaka nitakapoliangamiza taifa hilo kwa mkono wake. 927:9 Kum 18:11; Efe 5:6; Mit 19:27; Eze 13:1-23; Mwa 30:27; Isa 44:25; Kut 7:11; Yer 6:14Kwa hiyo msiwasikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota ndoto wenu, watabiri na wachawi wanaowaambia ninyi: Hamtamtumikia mfalme wa Babeli. 1027:10 Yer 23:25; Mk 13:5; 2Fal 23:27Wanawatabiria uongo ambao utawafanya ninyi mhamishwe mbali kutoka nchi yenu. Nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia. 1127:11 Yer 21:9; Kum 6:2Lakini ikiwa taifa lolote litainama na kuweka shingo lake katika nira ya mfalme wa Babeli na kumtumikia, nitaliacha taifa hilo katika nchi yake yenyewe ili wailime na kuishi humo, asema Bwana.” ’ ”

1227:12 Yer 17:4; 21:9Nilitoa ujumbe huo huo kwa Sedekia mfalme wa Yuda. Nilisema, “Ingiza shingo yako katika nira ya mfalme wa Babeli, umtumikie yeye na watu wake, nawe utaishi. 1327:13 Eze 18:31; Mit 8:36; Yer 14:12Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga, njaa na tauni, ambazo Bwana ameonya juu ya taifa lolote ambalo halitamtumikia mfalme wa Babeli? 1427:14 Yer 14:14; Mt 7:15; Yer 23:16-21Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia kwamba, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babeli,’ kwa sababu wanawatabiria uongo. 1527:15 Yer 23:21-29; 9; 44:16; 6:15; Mt 15:12-14‘Sikuwatuma hao,’ asema Bwana. ‘Wanatabiri uongo kwa jina langu. Kwa hiyo, nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia, ninyi pamoja na manabii wanaowatabiria.’ ”

1627:16 1Fal 7:48-50; Yer 28:3; Dan 1:2; 2Fal 24:13Kisha nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: Msiwasikilize manabii wanaosema, ‘Hivi karibuni sana vyombo vya nyumba ya Bwana vitarudishwa kutoka Babeli.’ Wanawatabiria ninyi uongo. 1727:17 Yer 23:16; 42:11Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babeli, nanyi mtaishi. Kwa nini mji huu uwe magofu? 1827:18 Hes 21:7; 1Sam 7:8; Ay 42; 8; Yak 5:16Kama wao ni manabii na wanalo neno la Bwana, basi na wamsihi Bwana Mwenye Nguvu Zote ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Bwana na katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visipelekwe Babeli. 1927:19 1Fal 7:23-26; 2Fal 25:13; Yer 52:17-23Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote kuhusu zile nguzo, ile Bahari, vile vishikizo viwezavyo kuhamishika, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika mji huu, 2027:20 Kum 28:36; 2Nya 36:10; Yer 22:24; Mt 1:11ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli hakuvichukua wakati alipomchukua Yekonia27:20 Yekonia au Konia ni jina jingine la Yehoyakini. mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda kwenda uhamishoni huko Babeli kutoka Yerusalemu, pamoja na wakuu wote wa Yuda na Yerusalemu. 21Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu vitu ambavyo vimebaki ndani ya nyumba ya Bwana, na ndani ya jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, na katika Yerusalemu: 2227:22 2Fal 20:17; 2Nya 25:13; 36:21; Yer 24:6; Ezr 7:19‘Vitachukuliwa kupelekwa Babeli, nako huko vitabaki mpaka siku nitakayovijilia,’ asema Bwana. ‘Kisha nitavirudisha na kuvirejesha mahali hapa.’ ”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

耶利米書 27:1-22

耶利米負軛的比喻

1約西亞的兒子猶大約雅敬執政初期,耶和華的話傳給了耶利米2耶和華對我說:「你要用皮帶和木頭做個軛,套在自己頸上。 3然後請那些到耶路撒冷朝見猶大西底迦的使者傳話給他們的主人以東王、摩押王、亞捫王、泰爾王和西頓王, 4說,『以色列的上帝——萬軍之耶和華說, 5我伸出大能的臂膀創造了大地、地上的人類和動物,我想把大地賜給誰就賜給誰。 6現在,我要把你們的國家交給我的僕人巴比倫尼布甲尼撒,連田野的走獸也要歸他管轄。 7各國都要臣服於他和他的子孫,直到他的國家滅亡。那時,許多國家和強大的君王必奴役他。 8如果哪一邦或哪一國不肯臣服於巴比倫尼布甲尼撒,不肯負巴比倫王的軛,我必用刀劍、饑荒和瘟疫懲罰他們,直到我藉巴比倫王的手毀滅他們。這是耶和華說的。 9你們不可聽信你們的先知、占卜者、解夢者、巫師和術士的話,他們說你們不會臣服於巴比倫王。 10他們的預言是騙人的,只會使你們遠離家園。我會趕走你們,使你們滅亡。 11但如果哪一國肯負巴比倫王的軛,臣服於他,我必使那國的人們留在本國耕種居住。這是耶和華說的。』」

12我同樣對猶大西底迦說:「你們要負巴比倫王的軛,臣服於他和他的人民,就可存活。 13你和你的人民何必死於刀劍、饑荒和瘟疫呢?耶和華要降這些災難給不肯臣服於巴比倫王的國家。 14不要聽信那些先知騙人的預言,他們說你們不會臣服於巴比倫王。 15耶和華並沒有派他們,他們卻奉祂的名說假預言。如果你們聽信他們的話,耶和華必把你們和向你們說預言的先知趕走,使你們一同滅亡。」 16我也對祭司和全體民眾說:「耶和華說,『你們不要聽信假先知騙人的預言,他們說耶和華殿裡的器皿很快就要從巴比倫運回來了。 17你們不可聽信他們的話。你們要臣服於巴比倫王,以便存活。何必使這城淪為廢墟呢? 18如果他們真的是先知,有耶和華給他們的信息,就讓他們求萬軍之耶和華不要使聖殿中、猶大王宮內和耶路撒冷剩餘的器皿被擄到巴比倫去。』 19-20巴比倫尼布甲尼撒約雅敬的兒子猶大耶哥尼雅,以及猶大耶路撒冷的貴族從耶路撒冷擄到巴比倫去的時候,沒有帶走耶和華殿的銅柱、銅海、銅底座及其他器皿。 21關於耶和華殿中、猶大王宮內和耶路撒冷剩下的物件,以色列的上帝——萬軍之耶和華說: 22『它們必被擄到巴比倫,留在那裡,一直到我眷顧以色列人的日子,那時我必把它們帶回原處。這是耶和華說的。』」