Yeremia 26 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 26:1-24

Yeremia Atishiwa Kuuawa

126:1 2Fal 23:36Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Bwana: 226:2 Yer 19:14; Kut 23:14; Mdo 20:27; Kum 12:5; Yer 17:19; Mt 28:20; Kum 4:2“Hili ndilo Bwana asemalo: Simama katika ua wa nyumba ya Bwana na useme na watu wote wa miji ya Yuda wanaokuja kuabudu katika nyumba ya Bwana. Waambie kila kitu nitakachokuamuru, usipunguze neno. 326:3 Kum 30:2; Isa 55:7; Yer 18:8; 2Nya 33:12-13; Yer 35:15; 36:7Huenda watasikiliza, na kila mmoja akageuka kutoka njia yake mbaya. Kisha nitawahurumia na kuacha kuwaletea maafa niliyokuwa ninapanga kwa sababu ya maovu waliyofanya. 426:4 Law 26:14; Yer 25:3; 1Fal 9:6; Yer 11:8Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ikiwa hamtanisikiliza na kuifuata sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu, 526:5 Mit 1:24; Isa 65:12; Yer 7:13; 25:4; 44:5nanyi ikiwa hamtayasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao nimewatuma kwenu tena na tena (ijapokuwa hamkuwasikiliza), 626:6 Yos 18:1; Amu 18:31; Kum 28:25; 2Fal 22:19ndipo nitaifanya nyumba hii kama Shilo na mji huu kuwa kitu cha kulaaniwa na mataifa yote ya dunia.’ ”

7Makuhani, manabii na watu wote wakamsikia Yeremia akiyasema maneno haya ndani ya nyumba ya Bwana. 826:8 Mdo 6:12; 21:27; Law 24:15-16; Neh 9:26; Yer 11:21Lakini mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu kila kitu Bwana alichomwamuru kukisema, basi makuhani, manabii na watu wote walimkamata wakisema, “Ni lazima ufe! 926:9 Law 26:32; Yer 9:11; Mdo 21:32Kwa nini unatoa unabii katika jina la Bwana kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa na kuachwa tupu?” Nao watu wote wakamkusanyikia na kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Bwana.

1026:10 Yer 34:19; Eze 22:27; Mwa 23:10Maafisa wa Yuda waliposikia kuhusu mambo haya, wakapanda kutoka jumba la kifalme, wakaenda katika nyumba ya Bwana na kushika nafasi zao kwenye ingilio la Lango Jipya la nyumba ya Bwana. 1126:11 Yer 38:4; Kum 18:20; Mdo 6:11; Kum 18:20Kisha makuhani na manabii wakawaambia maafisa pamoja na watu wote, “Mtu huyu anastahili ahukumiwe kifo kwa sababu ametoa unabii mbaya dhidi ya mji huu. Mmesikia kwa masikio yenu wenyewe!”

1226:12 Yer 1:18; Isa 6:8; Mdo 5:29; Amo 7:15; Mdo 4:18-20Kisha Yeremia akawaambia maafisa wote na watu wote: “Bwana amenituma kutoa unabii dhidi ya nyumba hii na mji huu mambo yote mliyoyasikia. 1326:13 Yoe 2:12; Yer 7:5; 35:15; 11:4; 18:8Sasa tengenezeni njia zenu na matendo yenu, na kumtii Bwana Mungu wenu. Ndipo Bwana atawahurumia na kuacha kuleta maafa aliyokuwa ameyatamka dhidi yenu. 1426:14 Yos 9:15; Yer 38:5Lakini kwa habari yangu mimi, niko mikononi mwenu, nifanyieni lolote mnaloona kuwa ni jema na la haki. 1526:15 Kum 19:10; Yer 1:17Hata hivyo, jueni kwa hakika, ikiwa mtaniua, mtakuwa mmejipatia dhambi kwa damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe, na juu ya mji huu na wote wanaoishi ndani yake, kwa maana ni kweli Bwana amenituma kwenu ili niseme maneno haya yote masikioni mwenu.”

1626:16 Mdo 23:9; 5:34-39; 23:29Kisha maafisa na watu wote wakawaambia makuhani na manabii, “Mtu huyu asihukumiwe kifo! Amesema nasi katika jina la Bwana, Mungu wetu.”

17Baadhi ya wazee wa nchi wakasogea mbele, wakaliambia kusanyiko lote la watu, 1826:18 Isa 2:3; 2Fal 25:9; Neh 4:2; Mik 1:4; Zek 8:3; Yer 17:3; 9:11“Mika Mmoreshethi alitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“ ‘Sayuni italimwa kama shamba,

Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto,

na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu

kilichofunikwa na vichaka.’

1926:19 1Nya 3:13; Kut 32:14; Isa 37:14-20; 2Sam 24:16; Hab 2:10; 2Nya 32:24-26Je, Hezekia mfalme wa Yuda au mtu mwingine yeyote katika Yuda alimhukumu Mika kufa? Je, Hezekia hakumcha Bwana na kuhitaji msaada wake? Je, Bwana hakuwahurumia na akaacha kuleta maafa aliyokuwa ametamka dhidi yao? Tunakaribia sana kujiletea maangamizo ya kutisha sisi wenyewe!”

2026:20 Yos 9:17(Wakati huu, Uria mwana wa Shemaya kutoka mji wa Kiriath-Yearimu alikuwa mtu mwingine aliyetoa unabii kwa jina la Bwana. Alitoa unabii juu ya mambo yaliyofanana na haya dhidi ya mji huu na nchi hii kama alivyofanya Yeremia. 2126:21 Mwa 31:21; Mt 10:23; 1Fal 19:2-3; Yer 2:30; Mt 23:37Mfalme Yehoyakimu na wakuu wake wote na maafisa waliposikia maneno yake, mfalme alitafuta kumuua. Lakini Uria alipata habari, na kwa kuogopa akakimbilia Misri. 2226:22 Yer 36:12, 25; Mit 29:12Hata hivyo, Mfalme Yehoyakimu alimtuma Elnathani mwana wa Akbori huko Misri, pamoja na watu wengine ili kwenda kumkamata Uria. 2326:23 2Fal 23:6; Ebr 11:37Wakamrudisha Uria kutoka Misri na kumpeleka kwa Mfalme Yehoyakimu, ambaye alimuua kwa upanga, na mwili wake kutupwa kwenye eneo la makaburi ya watu wasio na cheo.)

2426:24 2Fal 22:12; Yer 39:14Zaidi ya hayo, Ahikamu mwana wa Shafani akamuunga mkono Yeremia, kwa hiyo hakutiwa tena mikononi mwa watu ili auawe.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 26:1-24

耶利米被捕

1猶大約西亞的兒子約雅敬執政初期,耶和華對耶利米說: 2「這是耶和華說的,『你要站在我殿的院子裡,把我吩咐你的話一字不漏地告訴從猶大各城前來敬拜的人。 3或許他們會聽從我的話,改邪歸正,那樣我會施憐憫,取消原本用來懲治他們罪惡的災禍。 4你要告訴他們,耶和華這樣說,「如果你們不聽從我的話,不遵行我賜給你們的律法, 5不聽從我屢次派我的僕人——眾先知傳給你們的話, 6我必使這殿像示羅一樣被毀,使耶路撒冷被萬國咒詛。」』」

7祭司、先知和民眾都聽見了耶利米在耶和華的殿裡說的這些話。 8耶利米傳達完耶和華的話之後,祭司、先知和民眾就抓住他,說:「你真該死! 9你為什麼奉耶和華的名預言這殿必像示羅一樣被毀,這城必要荒無人煙呢?」於是,他們在耶和華的殿裡把耶利米圍了起來。

10猶大的首領得知後,就離開王宮,上到耶和華的殿,坐在耶和華殿新門的入口。 11祭司和先知對官員和民眾說:「這人該被處死!因為他預言這城要被毀,這是你們親耳聽到的。」

12耶利米對官員和民眾說:「你們剛才聽見的這些關於這殿和這城的預言都是耶和華差我說的。 13你們要改邪歸正,聽從你們上帝耶和華的話,這樣耶和華必施憐憫,取消本來要降給你們的災禍。 14至於我,我已落在你們手中,你們認為怎樣好就怎樣待我吧! 15不過,你們要知道,如果你們置我於死地,你們和這城及城中的居民必擔當濫殺無辜的罪,因為確實是耶和華派我來告訴你們這些預言的。」

16官員和民眾便對祭司和先知說:「這人不該被處死,因為他是奉我們上帝耶和華的名對我們說話。」 17有幾個長老站起來對眾人說: 18猶大希西迦執政期間,摩利沙彌迦猶大眾人預言說,

『萬軍之耶和華說錫安必被夷為平地,

耶路撒冷必淪為廢墟,

聖殿山要成為一片荒林。』

19「但猶大希西迦猶大眾人並沒有處死他。希西迦敬畏耶和華,求祂開恩,耶和華才施憐憫,沒有把原本預備的災禍降給他們。若處死這人,我們會大禍臨頭。」

20當時,基列·耶琳示瑪雅的兒子烏利亞也奉耶和華的名預言這城和這地方將被毀,內容與耶利米說的一樣。 21約雅敬王和他的王公大臣聽見烏利亞的話,就想處死他。烏利亞得知後,嚇得逃到埃及去了。 22約雅敬王便派亞革波的兒子以利拿單率隨從去埃及捉拿他。 23他們把烏利亞埃及押到約雅敬王面前,王用刀殺了他,把屍首拋在平民的墳地中。 24然而,沙番的兒子亞希甘保護耶利米,他才沒被交給民眾處死。