Yeremia 20 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 20:1-18

Yeremia Ateswa Na Pashuri

120:1 1Nya 24:14; 2Fal 25:18; Lk 22:52Ikawa kuhani Pashuri mwana wa Imeri, mkuu wa maafisa wa Hekalu la Bwana, alipomsikia Yeremia akitoa unabii juu ya mambo haya, 220:2 Kum 25:2-3; 2Kor 11:24; Ay 13:27; Zek 14:10; Ay 29:7; Yer 15:15; 37:15; 29:26; Mdo 16:24; Ebr 11:36akaamuru Yeremia nabii apigwe na kufungwa kwenye mkatale katika Lango la Juu la Benyamini huko Hekaluni la Bwana. 3Siku ya pili Pashuri alipomwachia kutoka kwenye mkatale, Yeremia akamwambia, “Bwana hakukuita jina lako kuwa Pashuri bali Magor-Misabibu.20:3 Magor-Misabibu maana yake hapa ni Vitisho pande zote. 420:4 Ay 18:11; Yer 29:21; 25:9; 52:27; 39:9; 21:10; 13:19Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitakufanya kuwa hofu kuu kwako wewe mwenyewe na rafiki zako wote, na kwa macho yako mwenyewe utawaona wakianguka kwa upanga wa adui zao. Nitawatia Yuda wote mikononi mwa mfalme wa Babeli, ambaye atawachukua na kuwapeleka Babeli, ama awaue kwa upanga. 520:5 2Fal 25:15; Yer 17:3; 3:24; 2Fal 20:17Nitatia utajiri wote wa mji huu kwa adui zao: yaani mazao yao yote, vitu vyao vyote vya thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda. Watavitwaa kwa nyara na kuvipeleka Babeli. 620:6 Yer 14:15; Mao 2:14; Yer 28:15Nawe Pashuri pamoja na wote waishio katika nyumba yako mtakwenda uhamishoni Babeli. Mtafia humo na kuzikwa, wewe na rafiki zako wote ambao umewatabiria uongo.’ ”

Malalamiko Ya Yeremia

720:7 Kut 5:23; 22:16; Isa 8:11; 1Kor 9:16; Ay 12:4Ee Bwana, umenidanganya,

nami nikadanganyika;

wewe una nguvu kuniliko,

nawe umenishinda.

Ninadharauliwa mchana kutwa,

kila mmoja ananidhihaki.

820:8 Yer 28:8; 2Nya 36:16; Yer 6:7-10Kila ninenapo, ninapiga kelele

nikitangaza ukatili na uharibifu.

Kwa hiyo neno la Bwana limeniletea matukano

na mashutumu mchana kutwa.

920:9 Za 39:3; Yer 4:19; Amo 3:8; Mdo 4:20; 18:5; Yer 44:16Lakini kama nikisema, “Sitamtaja

wala kusema tena kwa jina lake,”

neno lake linawaka ndani ya moyo wangu kama moto,

moto uliofungwa ndani ya mifupa yangu.

Nimechoka sana kwa kulizuia ndani mwangu;

kweli, siwezi kujizuia.

1020:10 Yer 6:25; Neh 6:6-13; Ay 19:14; Lk 11:54; Za 57:4Ninasikia minongʼono mingi,

“Hofu iko pande zote!

Mshtakini! Twendeni tumshtaki!”

Rafiki zangu wote wananisubiri niteleze,

wakisema,

“Labda atadanganyika;

kisha tutamshinda

na kulipiza kisasi juu yake.”

1120:11 Rum 8:31; Yer 15:15; 17:18; 23:40; 7:19; Za 129:2Lakini Bwana yu pamoja nami

kama shujaa mwenye nguvu;

hivyo washtaki wangu watajikwaa

na kamwe hawatashinda.

Watashindwa, nao wataaibika kabisa;

kukosa adabu kwao hakutasahauliwa.

1220:12 Yer 17:10; Za 54:7; Rum 12:19; Za 62:8; Yer 11:20; Za 7:9; Kum 32:35Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,

wewe umjaribuye mwenye haki

na kupima moyo na nia,

hebu nione ukilipiza kisasi juu yao,

kwa maana kwako

nimeliweka shauri langu.

1320:13 Za 35:10; Yak 2:5-6; Isa 12:6; Za 34:6; 97:10Mwimbieni Bwana!

Mpeni Bwana sifa!

Yeye huokoa uhai wa mhitaji

kutoka mikononi mwa waovu.

1420:14 Yer 15:10; Ay 3:8, 16Ilaaniwe siku niliyozaliwa!

Nayo isibarikiwe ile siku

mama yangu aliyonizaa!

15Alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari,

yule aliyemfanya afurahi sana, akisema,

“Mtoto amezaliwa kwako,

tena mtoto wa kiume!”

1620:16 Mwa 19:25; Yer 18:22; 6:26Mtu huyo na awe kama miji ile

ambayo Bwana Mungu

aliiangamiza bila huruma.

Yeye na asikie maombolezo asubuhi

na kilio cha vita adhuhuri.

1720:17 Ay 3:10-16; 10:18-19Kwa sababu hakuniua nikiwa tumboni,

hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu,

nalo tumbo lake la uzazi

lingebaki kuwa kubwa daima.

1820:18 1Fal 19:4; Za 102:3; Ay 3:20; 3:10-11; Mhu 4:2; Mwa 3:17; Ay 5:7; Za 90:9Kwa nini basi nilitoka tumboni

ili kuona taabu na huzuni,

na kuzimaliza siku zangu katika aibu?

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

耶利米書 20:1-18

耶利米受迫害

1音麥的兒子巴施戶珥祭司在耶和華的殿中做總管。他聽見耶利米預言這些事, 2便叫人毆打耶利米先知,用枷鎖把他鎖在耶和華殿的便雅憫上門處。 3第二天,他打開枷鎖釋放了耶利米耶利米對他說:「耶和華不再叫你巴施戶珥,要叫你瑪歌珥·米撒畢20·3 「瑪歌珥·米撒畢」意思是「四面有恐怖」。4因為耶和華說,『我要使你和你的朋友都驚慌失措,讓你親眼看見你的朋友死在敵人刀下。我要把猶大人都交在巴比倫王手中,使他們或被擄到巴比倫或死於刀下。 5我要把這城裡所有的財富、出產、珍寶,甚至猶大列王的寶物都交給敵人,帶到巴比倫作戰利品。 6巴施戶珥和你所有的家人,以及聽你說假預言的朋友都要被擄到巴比倫,死在那裡,葬在那裡。』」

耶利米的抱怨

7耶和華啊,

你欺騙我,我被你騙了。

你制伏我,勝過我。

如今,我終日被嘲笑,人人戲弄我。

8我每次說預言,都大聲疾呼:

「暴力和毀滅要來了!」

我因傳講耶和華的話而終日遭受侮辱和譏笑。

9有時我打算不再提起耶和華,

不再奉祂的名宣講,

但祂的話如一團火在我心中燃燒,

憋在我骨頭裡,

我無法隱忍,不得不說。

10我聽見許多人竊竊私語,

恐怖四下瀰漫。

他們說:「我們告發他!告發他!」

我的好友都盼著我滅亡,說:

「或許他會受騙,

那樣我們便能打倒他,

一洩心頭之恨。」

11但耶和華與我同在,

祂像勇猛的戰士。

所以迫害我的人必一敗塗地,

他們因失敗而羞愧難當,留下永遠的恥辱。

12考驗義人、洞悉人心的萬軍之耶和華啊,

求你讓我看見你報應他們,

因為我已向你稟明案情。

13你們要歌頌耶和華!

要讚美耶和華!

因為祂從惡人手中救出窮人。

14願我出生的那天受咒詛!

願我母親生我的那天不蒙祝福!

15願那告訴我父親喜得貴子、

使他歡喜的人受咒詛!

16願那人像被耶和華無情毀滅的城!

願他早晨聽見哀鳴,

中午聽見戰爭的吶喊,

17因為他沒有把我殺死在母腹中,

沒有使母腹成為我的墳墓,

讓我永遠留在裡面。

18為什麼我要從母胎出來,

經歷患難和痛苦,

在羞辱中度過一生呢?