Yeremia 15 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 15:1-21

Adhabu Isiyoepukika

115:1 Kut 32:11; Hes 14:13-20; 1Sam 7:9; Eze 14:14, 20; 2Fal 17:20; Yer 16:13; 7:16Kisha Bwana akaniambia: “Hata kama Mose na Samweli wangesimama mbele zangu, moyo wangu usingewaelekea watu hawa. Waondoe mbele za macho yangu! Waache waende! 215:2 Yer 42:22; 44:13; Zek 11:9; Mao 4:9; Eze 12:11; Ufu 13:10; Yer 14:12Nao kama wakikuuliza, ‘Twende wapi?’ Waambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo:

“ ‘Wale waliowekwa kwa ajili ya kufa, wakafe;

waliowekwa kwa ajili ya upanga, kwa upanga;

waliowekwa kwa ajili ya njaa, kwa njaa:

waliowekwa kwa ajili ya kutekwa, watekwe.’ ”

315:3 Law 26:16; Hes 33:4; Kum 28:26; Eze 33:27; 14:21; 2Fal 9:36; 1Fal 21:19Bwana asema, “Nitatuma aina nne za waharabu dhidi yao: nazo ni upanga ili kuua na mbwa ili wakokote mbali, ndege wa angani na wanyama wa nchi ili kula na kuangamiza. 415:4 Eze 23:46; Yer 29:18; 34:17; Ay 17:6; 2Fal 21:2, 11; 23:26-27; Yer 24:9Nitawafanya wawe machukizo kwa falme zote za dunia kwa sababu ya kile alichofanya Manase mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda huko Yerusalemu.

515:5 Isa 27:11; Nah 3:7; Isa 51:19; Yer 13:14; 16:13; 21:7“Ni nani atakayekuhurumia, ee Yerusalemu?

Ni nani atakayeomboleza kwa ajili yako?

Ni nani atakayesimama ili kuuliza

kuhusu hali yako?

615:6 Kum 32:15; Yer 6:19; Isa 31:3; Hos 13:14; Yer 7:20; Amo 7:8Umenikataa mimi,” asema Bwana.

“Unazidi kukengeuka.

Hivyo nitanyoosha mkono wangu juu yako na kukuangamiza,

siwezi kuendelea kukuonea huruma.

715:7 Isa 9:13; Yer 18:21; Isa 41:16; 3:26; 2Nya 28:22Nitawapepeta kwa uma wa kupepetea

kwenye malango ya miji katika nchi.

Nitaleta msiba na maangamizi juu ya watu wangu,

kwa maana hawajabadili njia zao.

815:8 Isa 47:9; Yer 6:4; Ay 18:11Nitawafanya wajane wao kuwa wengi

kuliko mchanga wa bahari.

Wakati wa adhuhuri nitamleta mharabu

dhidi ya mama wa vijana wao waume;

kwa ghafula nitaleta juu yao

maumivu makuu na hofu kuu.

915:9 1Sam 2:5; Yer 21:7; 25:31; 7:19; Amo 8:9; 2Fal 25:7; Yer 19:7Mama mwenye watoto saba atazimia

na kupumua pumzi yake ya mwisho.

Jua lake litatua kungali bado mchana,

atatahayarika na kufedheheka.

Wale wote waliobaki nitawaua kwa upanga

mbele ya adui zao,”

asema Bwana.

1015:10 Ay 10:18-19; Law 25:36; Neh 5:1-12; Ay 3:1; Yer 6:10; 1:19Ole wangu, mama yangu, kwamba ulinizaa,

mtu ambaye ulimwengu wote

unashindana na kugombana naye!

Sikukopa wala sikukopesha,

lakini kila mmoja ananilaani.

1115:11 Yer 40:4; 37:3; 42:1-3; 21:1-2Bwana akasema,

“Hakika nitakuokoa kwa kusudi jema,

hakika nitawafanya adui zako wakuombe msaada

nyakati za maafa na nyakati za dhiki.

1215:12 Mao 1:14; Hos 10:11; Kum 28:48; Yer 28:14“Je, mtu aweza kuvunja chuma,

chuma kitokacho kaskazini, au shaba?

1315:13 Yer 17:3; Za 44:12; Eze 38:12-13; 2Fal 24:13; 25:15Utajiri wako na hazina zako nitavitoa kuwa nyara,

bila gharama,

kwa sababu ya dhambi zako zote

katika nchi yako yote.

1415:14 Kum 28:36; Yer 16:13; Kum 32:22; Za 21:9; Yer 5:19Nitakufanya uwe mtumwa wa adui zako

katika nchi usiyoijua,

kwa kuwa katika hasira yangu moto umewashwa

utakaowaka juu yako daima.”

1515:15 Yn 21:15-17; Yer 12:3; Za 69:7-9; 119:84; 44:22; Kut 34:6Wewe unafahamu, Ee Bwana,

unikumbuke na unitunze mimi.

Lipiza kisasi juu ya watesi wangu.

Kwa uvumilivu wako usiniondolee mbali;

kumbuka jinsi ninavyoshutumiwa.

1615:16 Ay 23:12; 15:11; Eze 2:8; Ufu 10:10; Za 119:72, 103; Yer 14:9; Isa 43:7Maneno yako yalipokuja, niliyala;

yakawa shangwe yangu

na furaha ya moyo wangu,

kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako,

Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

1715:17 Rut 3:3; Za 26:4-5; Yer 16:8; 2Fal 3:15Kamwe sikuketi katika kundi la wafanyao sherehe,

wala kamwe sikujifurahisha pamoja nao;

niliketi peke yangu kwa sababu mkono wako ulikuwa juu yangu,

na wewe ulikuwa umenijaza hasira.

1815:18 Mik 1:9; Ay 6:4; Za 9:10Kwa nini maumivu yangu hayakomi,

na jeraha langu ni la kuhuzunisha,

wala haliponyeki?

Je, utakuwa kwangu kama kijito cha udanganyifu,

kama chemchemi iliyokauka?

1915:19 Zek 3:7; Eze 22:26; Kut 4:16Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana:

“Kama ukitubu, nitakurejeza

ili uweze kunitumikia;

kama ukinena maneno yenye maana,

wala si ya upuzi,

utakuwa mnenaji wangu.

Watu hawa ndio watakaokugeukia,

wala si wewe utakayewageukia wao.

2015:20 Yer 42:11; Eze 3:8; Isa 50:7; Za 129:2; Yer 20:11Nitakufanya wewe uwe ukuta kwa watu hawa,

ngome ya ukuta wa shaba;

watapigana nawe

lakini hawatakushinda,

kwa maana mimi niko pamoja nawe

kukuponya na kukuokoa,”

asema Bwana.

2115:21 Yer 50:34; Mwa 48:16; Isa 49:25; Yer 1:8; Za 97:10“Nitakuokoa kutoka mikono ya waovu,

na kukukomboa kutoka makucha ya watu wakatili.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

耶利米書 15:1-21

猶大的災難

1耶和華對我說:「就算摩西撒母耳站在我面前求情,我也不會憐憫這些百姓。你把他們從我面前趕走,讓他們離開吧! 2如果他們問你,『我們該去哪裡,』你就告訴他們,耶和華這樣說,

「『該死的死,

該被殺的被殺,

該遭饑荒的遭饑荒,

該被擄的被擄。』

3「我要讓他們遭受四種禍患——刀殺、狗撕、鳥啄、獸吞。這是耶和華說的。 4因為希西迦的兒子猶大瑪拿西耶路撒冷的所作所為,我要使他們的遭遇令天下萬國驚懼。

5耶路撒冷啊,誰會同情你?

誰會為你悲哀?

誰會駐足向你問安?

6你棄絕我,背離我,

因此我要伸手攻擊你,毀滅你,

我已厭倦施憐憫。

這是耶和華說的。

7我要在這片土地上的各城門口用簸箕簸散我的子民,

使他們喪掉兒女;

我要滅絕他們,

因為他們不思悔改。

8我要使他們的寡婦比海沙還多,

使毀滅者在午間攻擊青年的母親,

讓她們突然陷入痛苦和驚恐。

9生過七個孩子的母親心力枯竭,奄奄一息。

她的太陽在白晝已經墜落,

她必蒙羞受辱。

我必使其餘的人喪身在敵人刀下。

這是耶和華說的。」

耶利米訴苦

10母親啊,我真不幸,因為你生了我這個跟全猶大爭論、激辯的人。我沒有向人借貸,也沒有借貸給人,然而人人都咒罵我。 11耶和華說:「我必拯救你,使你受益。我必使仇敵在災禍、困難來臨時哀求你。 12誰能折斷來自北方之敵的鐵拳銅臂呢? 13因為你們境內罪惡氾濫,我要使敵人任意搶掠你們的財寶, 14把你們擄到陌生的地方。我的怒火已被點燃,要燒滅你們。」

15耶和華啊,你知道我的遭遇。

求你顧念我,眷顧我,

報應迫害我的人。

求你不要取走我的性命,

因為你不輕易發怒,

你知道我為了你忍受辱罵。

16萬軍之上帝耶和華啊,

我得到你的話便吃了下去,

你的話是我心中的快樂和喜悅,

因為我屬於你的名下。

17我沒有與作樂的人為伍,

沒有與他們同樂。

我獨坐一處,因為你的手按在我身上,

你使我義憤填膺。

18為什麼我的痛楚無休無止?

為什麼我的創傷無法治癒?

難道你要像一條時斷時流的小溪一樣靠不住嗎?

19因此,耶和華對我說:

「如果你回心轉意,

我就讓你重新事奉我。

你若說有益的話,

不說無益的話,

就可以做我的發言人,

百姓便會歸向你,

但你不可歸向他們。

20我要使你在這些百姓面前成為堅固的銅牆。

他們要攻擊你,卻不能勝過你,

因為我與你同在,我會搭救你,

拯救你。

這是耶和華說的。

21我要把你從惡人手中救出,

從殘暴之徒的權勢下贖回。」