Yeremia 12 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 12:1-17

Lalamiko La Yeremia

112:1 Ay 8:3; 12:6; Dan 9:14; Ay 21:7, 13; Ezr 9:15; Ay 5:8; Eze 18:25; Yer 5:27-28Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana,

niletapo mashtaka mbele yako.

Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako:

Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa?

Kwa nini wasio waaminifu

wote wanaishi kwa raha?

212:2 Isa 29:13; Eze 22:27; Yer 11:17; Mk 7:6; Ay 5:3; Yer 3:10; Mt 15:8; Tit 1:16Umewapanda, nao wameota,

wanakua na kuzaa matunda.

Daima u midomoni mwao,

lakini mbali na mioyo yao.

312:3 Yer 17:18; Za 7:9; 11:5; Yer 20:11; 16:18Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana;

unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe.

Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa!

Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!

412:4 Yer 4:25-28; Yoe 1:10-12; Kum 28:15-18; Za 107:34; Yer 4:26; 9:10Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini,

na majani katika kila shamba kunyauka?

Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu,

wanyama na ndege wameangamia.

Zaidi ya hayo, watu wanasema,

Bwana hataona yatakayotupata sisi.”

Jibu La Mungu

512:5 Yer 49:19; 50:44“Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda,

unawezaje kushindana na farasi?

Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama,

utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?

612:6 Mit 26:24-25; Yer 9:4; Za 12:2Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe:

hata wao wamekusaliti;

wameinua kilio kikubwa dhidi yako.

Usiwaamini, ingawa wanazungumza

mema juu yako.

7“Nitaiacha nyumba yangu,

nitupe urithi wangu;

nitamtia yeye nimpendaye

mikononi mwa adui zake.

812:8 Amo 6:8; 2Nya 36:16; Za 17:12; Hos 9:15Urithi wangu umekuwa kwangu

kama simba wa msituni.

Huningurumia mimi,

kwa hiyo ninamchukia.

912:9 Kum 28:26; Isa 56:9; Yer 15:3; Eze 23:25; 39:17-20Je, urithi wangu haukuwa

kama ndege wa mawindo wa madoadoa

ambaye ndege wengine wawindao

humzunguka na kumshambulia?

Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni;

walete ili wale.

1012:10 Yer 25:34; Eze 33:2; Isa 5:1-7; Yer 9:10; 25:11Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu

na kulikanyaga shamba langu;

watalifanya shamba langu zuri

kuwa jangwa la ukiwa.

1112:11 Isa 42:25; Yer 23:10; Isa 5:6; 24:4; Yer 9:12; 14:4Litafanywa kuwa jangwa,

lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu;

nchi yote itafanywa jangwa

kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.

1212:12 Kum 32:41; Eze 33:2; Yer 3:2; Eze 21:3-4; Isa 31:8; Yer 46:10; Eze 14:17Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani

mharabu atajaa,

kwa maana upanga wa Bwana utawala,

kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine;

hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.

1312:13 Mik 6:15; Kut 15:7; Yer 4:26; Law 26:16-20; Kum 28:38Watapanda ngano lakini watavuna miiba;

watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote.

Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako

kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”

1412:14 Zek 2:7-9; Sef 2:8-10; Yer 32:37; 2Nya 7:20; Za 9:6; Kum 29:28Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao. 1512:15 Kum 30:3; Amo 9:14-15; Eze 28:25; Za 6:2Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe. 1612:16 Yer 4:2; Yos 23:7; Efe 2:20; Isa 26:18; 49:6; Yer 18:8; 3:17Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu. 1712:17 Mwa 27:29; Isa 60:12; Za 2:8-9Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.

New Russian Translation

Иеремия 12:1-17

Жалоба Иеремии

1Господи, Ты праведен,

когда бы я ни обратился к Тебе с тяжбой.

Но позволь говорить с Тобой о правосудии.

Почему путь нечестивых успешен?

Почему процветают вероломные?

2Ты посадил их, и они пустили корни,

выросли и приносят плод.

Ты всегда у них на губах,

но далек от сердец их.

3А меня Ты, Господи, знаешь;

видишь меня и мои мысли о Тебе исследуешь.

Веди же их на бойню, как овец!

Отдели их на день заклания!

4Долго ли земле быть пересохшей

и траве вянуть на каждом поле?

Гибнут животные и птицы

из-за злодеяний ее жителей,

из-за того, что народ говорит:

«Он не увидит, что будет с нами12:4 Или: нашего будущего.».

Божий ответ

5«Если ты бежал с пешими,

и они тебя утомили,

как тебе состязаться с конями?

Если ты чувствуешь себя уверенно только на открытом поле12:5 Или: «Если ты споткнулся на ровной земле…»,

что же с тобой будет в зарослях у реки Иордан12:5 Или: в разлив Иордана.?

6Даже твои братья и все твои родственники,

даже они тебя предали;

провожают тебя громким криком.

Не доверяй им,

даже когда они говорят с тобою дружелюбно.

7Покину Свой дом,

брошу Свое владение,

самое дорогое Мне отдам

в руки его врагов.

8Стало Мое владение,

как лев в чаще:

рычит на Меня;

ненавижу его за это.

9Уподобилось Мое владение хищной птице,

на которую напали со всех сторон другие хищные птицы.

Ступайте, соберите всех диких зверей

и приведите их, чтобы они пожирали Мое владение.

10Множество пастухов погубило Мой виноградник,

вытоптало Мой надел;

они превратили Мой прекрасный надел

в разоренный пустырь.

11Превратили его в пустыню;

разоренный, он плачет предо Мной.

В разорении вся земля,

потому что никто не заботится о ней».

12По голым гребням пустынных гор

несутся опустошители.

Пожирает Господень меч

от края до края земли.

Нет мира ни для кого.

13Сажали пшеницу, пожали колючки,

утомились, но не было прока.

Огорчайтесь из-за вашего урожая,

потому что пылающий гнев Господа лишил вас его.

14Так говорит Господь: «Теперь обо всех Моих нечестивых соседях, что тянут свои руки к земле, которую Я отдал в наследие Моему народу, Израилю: Я искореню их из их земли, а дом Иуды вырву из их среды. 15Но вырвав их, Я снова помилую и верну каждого из них в его землю, в его страну. 16И если они научатся путям Моего народа, чтобы клясться Моим именем: „Верно, как и то, что жив Господь“, как некогда они учили Мой народ клясться Баалом, тогда они укоренятся среди Моего народа. 17Но если какой-нибудь из народов не станет слушать Меня, Я полностью искореню его и погублю», — возвещает Господь.