Yakobo 3 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Yakobo 3:1-18

Kuufuga Ulimi

13:1 1Fal 8:46; 1Yn 1:8; Mit 10:19; 1Pet 3:10; Mt 12:37; Yak 1:26Ndugu zangu, msiwe walimu wengi, kwa maana mnafahamu kwamba sisi tufundishao tutahukumiwa vikali zaidi. 23:2 Za 12:3, 4; 73:8, 9Sisi sote tunajikwaa katika mambo mengi. Ikiwa mtu yeyote hakosei kamwe katika yale anayosema, yeye ni mkamilifu, naye anaweza kuuzuia pia na mwili wake wote.

33:3 Za 32:9Tunapotia lijamu kwenye vinywa vya farasi ili kuwafanya watutii, tunaweza kuigeuza miili yao yote. 4Au angalia pia meli, ingawa ni kubwa sana, nazo huchukuliwa na upepo mkali, lakini hugeuzwa kwa usukani mdogo sana, kokote anakotaka nahodha. 53:5 Mt 15:11, 18, 19; Za 12:3, 4; 73:8, 9Vivyo hivyo ulimi ni kiungo kidogo sana katika mwili, lakini hujivuna majivuno makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa! 63:6 Mit 16:27; Mt 15:11, 18, 19; 5:22Ulimi pia ni moto, ndio ulimwengu wa uovu kati ya viungo vya mwili. Ulimi huutia mwili wote wa mtu unajisi na kuuwasha moto mfumo mzima wa maisha yake, nao wenyewe huchomwa moto wa jehanamu.

7Kwa maana kila aina ya wanyama, ndege, wanyama watambaao na viumbe vya baharini vinafugika na vimefugwa na binadamu, 83:8 Za 140:10; Rum 3:13lakini hakuna mtu awezaye kuufuga ulimi. Ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

93:9 Mwa 1:26-27Kwa ulimi tunamhimidi Bwana, yaani Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu walioumbwa kwa mfano wa Mungu. 10Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo. 113:11 Kut 20:14; Kum 5:8; 5:17; Kut 5:18Je, chemchemi yaweza kutoa katika tundu moja maji matamu na maji ya chumvi? 123:12 Yak 1:25Je, ndugu zangu, mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Wala chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.

Aina Mbili Za Hekima

133:13 Mt 9:13; Lk 6:37Ni nani aliye na hekima na ufahamu miongoni mwenu? Basi na aionyeshe hiyo kwa maisha yake mema na kwa matendo yake yaliyotendwa kwa unyenyekevu utokanao na hekima. 143:14 Mt 6:27; Yak 1:22-25Lakini ikiwa mna wivu na ni wenye chuki na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu kwa ajili ya hayo wala msiikatae kweli. 153:15 Mt 25:35, 36Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni, bali ni ya kidunia, isiyo ya kiroho, na ya kishetani. 163:16 Lk 3:11; 1Yn 3:17, 18Kwa maana panapokuwa na wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na uovu wa kila namna.

17Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha inapenda amani, tena ni ya upole, iliyo tayari kusikiliza wengine kwa unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, tena isiyokuwa na unafiki. 183:18 Rum 3:28; Mt 7:16, 18Mavuno ya haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

雅各书 3:1-18

邪恶的舌头

1我的弟兄姊妹,不要个个当教师,因为你们知道,我们为人师表的将受到更严格的评判。 2因为我们在许多方面难免有过失。如果谁在言语上没有过失,他就是纯全的人,也能在各方面保持自制。 3我们如果把嚼环放在马嘴里,便可以驯服它,驾驭它。 4一艘大船被强风吹袭时,船身虽然庞大,但舵手只要操纵一个小小的舵,就能随意驾驶它。 5同样,人的舌头虽然很小,却能说夸大的话。

看啊,小火星能点燃大森林。 6舌头就是火,是我们身体上的一个充满邪恶的世界,能玷污人的全身,足以烧毁人的一生,它是从地狱点燃的火。 7自然界中的各类走兽、飞禽、爬虫、水族都可以被驯服,也已经被人类驯服了, 8但无人能驯服自己的舌头,因为舌头是个蠢蠢欲动的邪恶之物,充满了致命的毒气。 9我们用舌头来赞美我们的主和天父,也用舌头来咒诅照着上帝的形象被造的人。 10赞美和咒诅竟然从同一张嘴里发出来。我的弟兄姊妹,这是不应该的! 11同一个泉源能涌出甜苦两样水吗? 12我的弟兄姊妹,无花果树能结出橄榄吗?葡萄树能结出无花果吗?一个咸水泉必流不出甜水来。

天上的智慧

13你们当中谁是有智慧、有见识的呢?请他带着从智慧而来的谦和在善行上表现出来。 14但如果你们心怀苦涩的嫉妒和自私的野心,就不要自夸,也不要违背真理去撒谎。 15这种智慧并非来自天上,而是从世俗、私欲和魔鬼来的。 16哪里有嫉妒和自私的野心,哪里就会有混乱和各种恶事。

17但从天上来的智慧首先是纯洁,然后是爱好和平、温良柔顺、充满怜悯、多结善果、不存偏见、没有虚伪。 18使人和睦的人撒下和平的种子,必收获仁义的果实。