Yakobo 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yakobo 2:1-26

Onyo Kuhusu Upendeleo

12:1 Mdo 7:2; 1Kor 2:8; Mit 24:23; Mdo 10:34Ndugu zangu, kama waaminio katika imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe na upendeleo kwa watu. 22:2 Ebr 10:25Kwa maana kama akija mtu katika kusanyiko lenu akiwa amevaa pete ya dhahabu na mavazi mazuri, pia akaingia mtu maskini mwenye mavazi yaliyochakaa, 3nanyi mkampa heshima yule aliyevaa mavazi mazuri na kumwambia, “Keti hapa mahali pazuri,” lakini yule maskini mkamwambia, “Wewe simama pale,” au “Keti hapa sakafuni karibu na miguu yangu,” 42:4 Yn 7:24je, hamjawabagua na kuwa mahakimu mioyoni mwenu mkihukumu kwa mawazo yenu maovu?

52:5 Yak 1:16, 19; Ay 34:19; 1Kor 1:26-28; Lk 12:21; Ufu 2:9; Yos 1:12Ndugu zangu, sikilizeni: Je, Mungu hakuwachagua wale walio maskini machoni pa ulimwengu kuwa matajiri katika imani na kuurithi Ufalme aliowaahidi wale wampendao? 62:6 1Kor 11:22; Mdo 8:3; 16:19Lakini ninyi mmemdharau yule aliye maskini. Je, hao matajiri si ndio wanaowadhulumu na kuwaburuta mahakamani? 7Je, si wao wanaolikufuru Jina lile lililo bora sana mliloitiwa?

82:8 Law 19:18; Mt 5:43Kama kweli mnaitimiza ile sheria ya kifalme inayopatikana katika Maandiko isemayo, “Mpende jirani yako kama unavyoipenda nafsi yako,” mnafanya vyema. 92:9 Kum 1:17; Yak 2:1Lakini kama mnakuwa na upendeleo kwa watu, mnatenda dhambi, na sheria inawahukumu kuwa ninyi ni wakosaji. 102:10 Mt 5:19; Gal 5:3Kwa maana mtu yeyote anayeishika sheria yote lakini akajikwaa katika kipengele kimoja tu, ana hatia ya kuivunja sheria yote. 112:11 Kut 20:14; Kum 5:18; 5:17; Kut 20:13Kwa sababu yeye aliyesema, “Usizini,” alisema pia, “Usiue.” Basi kama huzini lakini unaua, umekuwa mvunjaji wa sheria.

122:12 Yak 1:25; Mt 16:27Hivyo semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ile iletayo uhuru. 132:13 Mt 9:13; Lk 6:37Kwa kuwa hukumu bila huruma itatolewa kwa mtu yeyote asiyekuwa na huruma. Huruma huishinda hukumu.

Imani Na Matendo

142:14 Mt 7:26; Yak 1:22-25Ndugu zangu, yafaa nini ikiwa mtu atadai kuwa anayo imani lakini hana matendo? Je, imani kama hiyo yaweza kumwokoa? 152:15 Mt 25:35, 36; Ay 31:19; Lk 3:11Ikiwa ndugu yako au dada hana mavazi wala chakula, 162:16 Lk 3:11; 1Yn 3:17, 18mmoja wenu akamwambia, “Enenda zako kwa amani, ukaote moto na kushiba,” pasipo kumpatia yale mahitaji ya mwili aliyopungukiwa, yafaa nini? 172:17 Yak 2:20, 26; Gal 5:6Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.

182:18 Rum 3:28; Mt 7:16, 17; Yak 3:13Lakini mtu mwingine atasema, “Wewe unayo imani; mimi ninayo matendo.”

Nionyeshe imani yako pasipo matendo nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo. 192:19 Kum 6:4; Mt 12:29; 8:29; Lk 4:34Unaamini kwamba kuna Mungu mmoja. Vyema! Hata mashetani yanaamini hivyo na kutetemeka.

202:20 Yak 2:17, 26Ewe mpumbavu! Je, wataka kujua kwamba imani bila matendo haifai kitu? 212:21 Mwa 22:9, 12Je, Abrahamu baba yetu hakuhesabiwa haki kwa kile alichotenda, alipomtoa mwanawe Isaki madhabahuni? 222:22 Ebr 11:17; 1The 1:3Unaona jinsi ambavyo imani yake na matendo yake vilikuwa vinatenda kazi pamoja, nayo imani yake ikakamilishwa na kile alichotenda. 232:23 Mwa 15:6; Rum 4:3; 2Nya 20:7; Isa 41:8Kwa njia hiyo yakatimizwa yale Maandiko yasemayo, “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki,” naye akaitwa rafiki wa Mungu. 24Mnaona ya kwamba mtu huhesabiwa haki kwa yale anayotenda wala si kwa imani peke yake.

252:25 Ebr 11:31Vivyo hivyo, hata Rahabu, yule kahaba, hakuhesabiwa haki kwa yale aliyotenda alipowapokea wale wapelelezi na kuwaambia waende njia nyingine? 26Kama vile ambavyo mwili pasipo roho umekufa, kadhalika nayo imani pasipo matendo imekufa.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

雅各书 2:1-26

不可以貌取人

1我的弟兄姊妹,你们既然信了我们荣耀的主耶稣基督,就不可以貌取人。 2比方说,一个手戴金饰、衣着华丽的人来参加你们的聚会,一个衣衫褴褛的人也来参加, 3你们就看重那衣着华丽的,对他说:“请上座。”却对那穷人说:“你站在那边。”或“坐在我的脚凳边。” 4你们这样做难道不是偏心待人,心怀恶意地判断人吗?

5我亲爱的弟兄姊妹,请听我说,上帝不是拣选了穷人,使他们在信心上富足,并承受祂应许赐给那些爱祂之人的国度吗? 6你们反倒侮辱穷人。其实欺压你们、抓你们上法庭的不是那些富人吗? 7不正是他们亵渎你们所敬奉的尊名吗?

8如果你们能切实行出圣经中“要爱邻如己”这条至尊的律法,就好了。 9如果你们偏待人,嫌贫爱富,便是犯罪,律法要将你们定罪。 10人只要触犯律法中的一条,就等于违犯了全部, 11因为那位说“不可通奸”的,也说过“不可杀人”。如果你没有犯通奸罪,却杀了人,你仍违犯了律法。 12既然你们要按使人自由的律法受审判,就应该按律法行事为人。 13因为不怜悯人的会受到无情的审判,但怜悯胜过审判。

信心和行为

14我的弟兄姊妹,如果有人自称有信心,却没有行为来证实,有什么用呢?这种信心能够救他吗? 15如果有弟兄姊妹缺衣少食, 16你们只是对他们说:“安心走吧,愿你们穿得暖,吃得饱”,却不帮助他解决实际困难,这有什么用呢? 17因此,信心若没有行为,就是死的。

18必有人说:“你有信心,我有行为。”请把你没有行为的信心指给我看,我就借着行为把我的信心显给你看。 19你相信上帝只有一位,你信得没错,鬼魔也相信,而且恐惧战抖。

20愚蠢的人啊,你们不知道没有行为的信心是死的吗? 21我们的祖先亚伯拉罕把儿子以撒献在祭坛上的时候,难道不是因行为而被称为义人吗? 22可见他的信心和行为相称,而且信心要有行为才是完全的。 23这正应验了圣经的记载:“亚伯拉罕信上帝,就被算为义人”,并且被称为“上帝的朋友”。 24可见人要被上帝算为义人必须有与信心相称的行为,并非单有信心。 25还有妓女喇合,她收留使者,把他们藏在家里,又送他们从别的路逃生,不也是因行为而被称为义人吗?

26身体没有灵魂是死的,同样,信心没有行为也是死的。