Wimbo 4 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Wimbo 4:1-16

Mpenzi

14:1 Wim 1:15; 5:12; Mwa 37:25; Hes 32:1; Mwa 24:65; Yer 22:6; Mik 7:14Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu!

Ee, jinsi ulivyo mzuri!

Macho yako nyuma ya shela yako

ni kama ya hua.

Nywele zako ni kama kundi la mbuzi

zikishuka kutoka Mlima Gileadi.

24:2 Wim 6:6Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi,

watokao kuogeshwa.

Kila mmoja ana pacha lake,

hakuna hata mmoja aliye peke yake.

34:3 Wim 5:16; 6:7Midomo yako ni kama uzi mwekundu,

kinywa chako kinapendeza.

Mashavu yako nyuma ya shela yako

ni kama vipande viwili vya komamanga.

44:4 Eze 27:10; Neh 3:19; 2Sam 22:51; Za 144:12Shingo yako ni kama mnara wa Daudi,

uliojengwa kwa madaha,

juu yake zimetundikwa ngao elfu,

zote ni ngao za mashujaa.

54:5 Wim 7:3; 6:2-3; Mit 5:19; Isa 66:10-12Matiti yako mawili ni kama wana-paa wawili,

kama wana-paa mapacha

wajilishao katikati ya yungiyungi.

64:6 Wim 2:6-7; 3:6; 2:17Hata kupambazuke na vivuli vikimbie,

nitakwenda kwenye mlima wa manemane

na kwenye kilima cha uvumba.

74:7 Wim 1:15Wewe ni mzuri kote, mpenzi wangu,

hakuna hitilafu ndani yako.

84:8 Kum 3:9; 1Nya 5:23; Wim 5:1Enda nami kutoka Lebanoni, bibi arusi wangu,

enda nami kutoka Lebanoni.

Shuka kutoka ncha ya Amana,

kutoka juu ya Seniri, kilele cha Hermoni,

kutoka mapango ya simba

na kutoka mlima wapendapo kukaa chui.

94:9 Isa 54:5; Za 73:6; Yn 3:29; Mwa 41:43Umeiba moyo wangu, dada yangu, bibi arusi wangu;

umeiba moyo wangu

kwa mtazamo mmoja wa macho yako,

kwa kito kimoja cha mkufu wako.

104:10 Wim 7:6; 1:2; Amu 9:13; Za 45:8; Isa 57:9Tazama jinsi pendo lako linavyofurahisha,

dada yangu, bibi arusi wangu!

Pendo lako linafurahisha aje zaidi ya divai,

na harufu ya manukato yako zaidi ya kikolezo chochote!

114:11 Hos 14:6; Za 19:10; Mit 24:13-14; Mwa 27:27Midomo yako inadondosha utamu kama sega la asali,

bibi arusi wangu;

maziwa na asali viko chini ya ulimi wako.

Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ile ya Lebanoni.

124:12 Mit 5:15-18; Isa 58:11; Wim 6:2; 5:1Wewe ni bustani iliyofungwa, dada yangu,

bibi arusi wangu;

wewe ni chanzo cha maji kilichozungushiwa kabisa,

chemchemi yangu peke yangu.

134:13 Wim 6:11; 7:12; 1:14Mimea yako ni bustani ya mikomamanga

yenye matunda mazuri sana,

yenye hina na nardo,

144:14 Kut 30:23; Wim 3:6; 1:12; Hes 24:6nardo na zafarani,

mchai na mdalasini,

pamoja na kila aina ya mti wa uvumba,

manemane na udi,

na aina zote za vikolezo bora kuliko vyote.

154:15 Isa 27:2; 58:11; Yer 31:12; Mit 5:18Wewe ni chemchemi ya bustani,

kisima cha maji yatiririkayo,

yakitiririka kutoka Lebanoni.

Mpendwa

164:16 Wim 2:3Amka, upepo wa kaskazini,

na uje, upepo wa kusini!

Vuma juu ya bustani yangu,

ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ngʼambo.

Mpendwa wangu na aje bustanini mwake

na kuonja matunda mazuri sana.