Warumi 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Warumi 7:1-25

Hatufungwi Tena Na Sheria

17:1 Gal 3:15; 5:18Ndugu zangu (sasa ninasema na wale wanaoijua sheria), je, hamjui ya kwamba sheria ina mamlaka tu juu ya mtu wakati akiwa hai? 27:2 1Kor 7:39Kwa mfano, mwanamke aliyeolewa amefungwa kwa mumewe wakati akiwa hai, lakini yule mume akifa, yule mwanamke amefunguliwa kutoka sheria ya ndoa. 37:3 Lk 16:18; Mt 5:32Hivyo basi, kama huyo mwanamke ataolewa na mwanaume mwingine wakati mumewe akiwa bado yuko hai, ataitwa mzinzi. Lakini kama mumewe akifa, mwanamke huyo hafungwi tena na sheria ya ndoa, naye akiolewa na mtu mwingine haitwi mzinzi.

47:4 Gal 2:19; 4:31; Kol 1:22Vivyo hivyo, ndugu zangu, ninyi mmeifia sheria kwa njia ya mwili wa Kristo, ili mweze kuwa mali ya mwingine, yeye ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu, ili tupate kuzaa matunda kwa Mungu. 57:5 Rum 7:7-11; 6:13Kwa maana tulipokuwa tunatawaliwa na asili ya dhambi, tamaa za dhambi zilizochochewa na sheria zilikuwa zikitenda kazi katika miili yetu, hivyo tulizaa matunda ya mauti. 67:6 Rum 2:29Lakini sasa, kwa kufia kile kilichokuwa kimetufunga kwanza, tumewekwa huru kutokana na sheria ili tutumike katika njia mpya ya Roho, wala si katika njia ya zamani ya sheria iliyoandikwa.

Sheria Na Dhambi

77:7 Rum 3:20; 4:15; Kut 20:17; Kum 5:21Tuseme nini basi? Kwamba sheria ni dhambi? La, hasha! Lakini, isingekuwa kwa sababu ya sheria, nisingalijua dhambi. Nisingalijua kutamani ni nini kama sheria haikusema, “Usitamani.” 87:8 Rum 4:15; 1Kor 15:56Lakini dhambi kwa kupata nafasi katika amri, hii ikazaa ndani yangu kila aina ya tamaa. Kwa maana pasipo sheria, dhambi imekufa. 9Wakati fulani nilikuwa hai pasipo sheria, lakini amri ilipokuja, dhambi ikawa hai, nami nikafa. 107:10 Law 18:5; Lk 10:26-28Nikaona kwamba ile amri iliyokusudiwa kuleta uzima, ilileta mauti. 117:11 Mwa 3:13Kwa maana dhambi kwa kupata nafasi katika amri, ilinidanganya, na kupitia katika hiyo amri, ikaniua. 127:12 Gal 3:21; 1Tim 1:8Hivyo basi, sheria yenyewe ni takatifu, na amri ni takatifu na ya haki, tena ni njema.

137:13 Rum 6:23; 7:12; 5:20Je, kile kilicho chema basi kilikuwa mauti kwangu? La, hasha! Lakini ili dhambi itambuliwe kuwa ni dhambi, ilileta mauti ndani yangu kupitia kile kilichokuwa chema, ili kwa njia ya amri dhambi izidi kuwa mbaya kupita kiasi.

Mgongano Wa Ndani

147:14 1Kor 3:1; 1Fal 21:20-25; 2Fal 17:17Kwa maana tunajua kwamba sheria ni ya kiroho, lakini mimi ni wa kimwili nikiwa nimeuzwa kwenye utumwa wa dhambi. 157:15 Gal 5:17Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia. 167:16 Rum 7:12Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, ni kwamba ninakubali kuwa sheria ni njema. 177:17 Rum 7:20Lakini, kwa kweli si mimi tena nitendaye lile nisilotaka bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 187:18 Gal 5:24Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna jema lolote likaalo ndani yangu, yaani, katika asili yangu ya dhambi. Kwa kuwa nina shauku ya kutenda lililo jema, lakini siwezi kulitenda. 197:19 Rum 7:15Sitendi lile jema nitakalo kutenda, bali lile baya nisilolitaka, ndilo nitendalo. 207:20 Rum 7:17Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.

217:21 Rum 7:23, 25Hivyo naiona sheria ikitenda kazi. Ninapotaka kutenda jema, jambo baya liko papo hapo. 227:22 Efe 3:16; Za 1:2; 40:8Kwa maana katika utu wangu wa ndani naifurahia sheria ya Mungu. 237:23 Yak 4:1; 1Pet 2:11Lakini ninaona kuna sheria nyingine inayotenda kazi katika viungo vya mwili wangu inayopigana vita dhidi ya ile sheria ya akili yangu. Sheria hii inanifanya mateka wa ile sheria ya dhambi inayofanya kazi katika viungo vya mwili wangu.

247:24 Rum 6:6; 8:2Ole wangu mimi maskini! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?

25Ashukuriwe Mungu kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu! Hivyo basi, mimi mwenyewe kwa akili zangu ni mtumwa wa sheria ya Mungu, lakini katika asili ya dhambi ni mtumwa wa sheria ya dhambi.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

羅馬書 7:1-25

婚姻關係的例子

1弟兄姊妹,我現在對那些熟悉律法的人說:你們難道不知道律法只在人活著的時候管轄人嗎? 2比方說,一個婦人結了婚,只要丈夫還在世,她就受律法的約束要與丈夫在一起。如果丈夫死了,她就脫離了與丈夫的婚姻關係。 3丈夫還活著的時候,她若與別的男人通姦,便被稱為淫婦。丈夫若死了,她就脫離了與丈夫的婚姻關係,即使改嫁,也不是淫婦。

4我的弟兄姊妹,同樣,你們藉著基督的身體向著律法也死了,使你們可以歸於另一位,就是從死裡復活的基督,好為上帝結果子。 5從前我們受自己本性7·5 「本性」希臘文是「肉體」,以下皆用相同譯法。的控制,因律法而激發的罪惡慾望在我們體內發作,以致結出死亡的果子。 6但現在,我們既然向著一度捆綁我們的律法死了,就脫離了律法的控制,能夠以聖靈所賜的新樣式,而不是按律法條文的舊樣式事奉上帝。

律法使人知罪

7那麼,我們該怎麼說呢?律法是罪嗎?當然不是!要是沒有律法,我就不知道什麼是罪。律法若不說「不可貪心」7·7 出埃及記20·17申命記5·21,我就不知道什麼是貪心。 8然而,罪卻趁機利用誡命在我裡面生出各種貪念,因為沒有律法,罪是死的。 9從前沒有律法的時候,我是活的,但誡命來了之後,罪就活了,而我卻死了。 10我發現那本來要使人活的誡命反而叫我死, 11因為罪利用誡命趁機誘騙我,而且藉著誡命殺了我。 12可見律法是聖潔的,誡命也是聖潔、公義、良善的。

13既然如此,難道是良善的誡命叫我死嗎?當然不是!是罪藉著良善的誡命叫我死,好讓我們認識罪的真面目,並且罪藉著誡命更顯得邪惡至極!

善惡相爭

14我們知道律法是屬靈的,我卻屬乎肉體,已經賣給罪做奴隸了。 15我不明白自己的所作所為,因為我想做的,我不去做;而我憎恨的,我偏偏去做! 16如果我做我不想做的,我就承認律法是好的。 17其實不再是我在做,而是住在我裡面的罪在做。 18我也知道,在我裡面,就是我的本性裡面毫無良善,我有行善的心願,卻沒有行善的力量。 19我想行善,卻不去行;我不想作惡,反倒去作。 20如果我做我不想做的,就不再是我在做,而是住在我裡面的罪在做。

21因此,我發現一個律:我想行善的時候,惡就不放過我。 22按著我裡面的意思7·22 「裡面的意思」希臘文是「裡面的人」。,我喜愛上帝的律。 23然而,我發覺在我身體內另有一個律和我心中的律作戰,將我俘虜,使我服從身體內犯罪的律。 24我真是苦啊!誰能救我脫離這個被死亡控制的身體呢? 25感謝上帝,祂藉著我們的主耶穌基督救了我!這樣看來,我的內心服從上帝的律法,但我的本性卻服從犯罪的律。