Warumi 12 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Warumi 12:1-21

Maisha Mapya Katika Kristo

112:1 Rum 6:13, 16, 19; 1Kor 6:20; 1Pet 2:5Kwa hiyo, ndugu zangu, nawasihi kwa rehema zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu na inayompendeza Mungu, hii ndiyo ibada yenu yenye maana. 212:2 1Pet 1:14; Efe 5:17; 1Kor 1:20; 2Kor 10; 2; 1Yn 2:15; 1Tim 5:4Msifuatishe tena mfano wa ulimwengu huu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Ndipo mtaweza kuonja na kuhakikisha ni nini mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yanayopendeza machoni pake na ukamilifu.

312:3 Rum 15:15; Gal 2:9; 1Kor 15:10; Efe 3:7; 4:7; 1Pet 4:10, 11Kwa ajili ya neema niliyopewa nawaambia kila mmoja miongoni mwenu, asijidhanie kuwa bora kuliko impasavyo, bali afikiri kwa busara kwa kulingana na kipimo cha imani Mungu aliyompa. 412:4 1Kor 12:12-14; Efe 4:16Kama vile katika mwili mmoja tulivyo na viungo vingi, navyo viungo vyote havina kazi moja, 512:5 1Kor 6:15; 10:17; 12:12, 20, 27; Efe 2:16; 4:4, 25; Kol 3:15vivyo hivyo na sisi tulio wengi, tu mwili mmoja katika Kristo, nasi kila mmoja ni kiungo cha mwenzake. 612:6 1Kor 7:7; 12:4, 8-10; Efe 4:11; 1Pet 4:10, 11Tuna karama zilizotofautiana kila mmoja kutokana na neema tuliyopewa. Kama ni unabii na tutoe unabii kwa kadiri ya imani. 712:7 Efe 4:11; 1Pet 4:10, 11; Mdo 13:1; Efe 4:11Kama ni kuhudumu na tuhudumu, mwenye kufundisha na afundishe, 812:8 Mdo 11:23; 13:15; 15:32; 2Kor 8:2; 9:5-13kama ni kutia moyo na atie moyo, kama ni kuchangia kwa ajili ya mahitaji ya wengine na atoe kwa ukarimu, kama ni uongozi na aongoze kwa bidii, kama ni kuhurumia wengine na afanye hivyo kwa furaha.

Alama Za Mkristo Wa Kweli

912:9 2Kor 6:6; 1Tim 1:5; Za 97:10; Amo 5:15; 1The 5:21, 22Upendo lazima usiwe na unafiki. Chukieni lililo ovu, shikamaneni na lililo jema. 1012:10 Za 133:1; 1The 4:9; Ebr 13:1; 1Pet 1:22; Flp 2:3Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa upendo wa ndugu. Waheshimuni na kuwatanguliza wengine. 1112:11 Mdo 18:25; Ufu 3:15Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana. 1212:12 Rum 5:2; Ebr 10:32, 36; Lk 18:1Kuweni na furaha katika tumaini, katika dhiki kuweni na saburi, dumuni katika maombi. 1312:13 Mdo 24:17; 2Fal 4:10; Ay 31:32; 1Tim 3:2; 5:10Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni.

14Wabarikini wale wanaowatesa, barikini wala msilaani. 15Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao. 16Kaeni kwa amani ninyi kwa ninyi. Msijivune, bali mwe tayari kushirikiana na wanyonge. Wala msiwe watu wenye kujivuna kwamba mnajua kila kitu.

1712:17 Mit 20:22; 24:29; 2Kor 8:21Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Jitahidini ili mtende yaliyo mema machoni pa watu wote. 1812:18 Mk 9:50; Rum 14:19Kama ikiwezekana, kwa upande wenu kaeni kwa amani na watu wote. 1912:19 Law 19:18; Mit 20:22; 22:29; Kum 32:35; Mwa 50:19; Isa 26:10Wapendwa, msilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa: “Ni juu yangu kulipiza kisasi, nitalipiza,” asema Bwana. 2012:20 Kut 23:4; Mt 5:44; Mit 25:21, 22; Lk 6:27Badala yake:

“Kama adui yako ana njaa, mlishe;

kama ana kiu, mpe kinywaji.

Kwa kufanya hivyo,

unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake.”

21Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

Nueva Versión Internacional

Romanos 12:1-21

Sacrificios vivos

1Por lo tanto, hermanos, tomando en cuenta la misericordia de Dios, ruego que cada uno de ustedes, en adoración espiritual,12:1 espiritual. Alt. racional. ofrezca su cuerpo como sacrificio vivo, santo y agradable a Dios. 2No se amolden al mundo actual, sino sean transformados mediante la renovación de su mente. Así podrán comprobar cómo es la voluntad de Dios: buena, agradable y perfecta.

3Por la gracia que se me ha dado, digo a todos ustedes: Nadie tenga un concepto de sí más alto que el que debe tener, sino más bien piense de sí mismo con moderación, según la medida de fe que Dios le haya dado. 4Pues, así como cada uno de nosotros tiene un solo cuerpo con muchos miembros, y no todos estos miembros desempeñan la misma función, 5también nosotros, siendo muchos, formamos un solo cuerpo en Cristo, y cada miembro está unido a todos los demás. 6Tenemos dones diferentes, según la gracia que se nos ha dado. Si el don de alguien es el de profecía, que lo use en proporción con su fe;12:6 en proporción con su fe. Alt. de acuerdo con la fe. 7si es el de prestar un servicio, que lo preste; si es el de enseñar, que enseñe; 8si es el de animar a otros, que los anime; si es el de socorrer a los necesitados, que dé con generosidad; si es el de dirigir, que dirija con esmero; si es el de mostrar compasión, que lo haga con alegría.

El amor

9El amor debe ser sincero. Aborrezcan el mal; aférrense al bien. 10Ámense los unos a los otros con amor fraternal, respetándose y honrándose mutuamente. 11Nunca dejen de ser diligentes; antes bien, sirvan al Señor con el fervor que da el Espíritu. 12Alégrense en la esperanza, muestren paciencia en el sufrimiento, perseveren en la oración. 13Ayuden a los hermanos necesitados. Practiquen la hospitalidad. 14Bendigan a quienes los persigan; bendigan y no maldigan. 15Alégrense con los que están alegres; lloren con los que lloran. 16Vivan en armonía los unos con los otros. No sean arrogantes, sino háganse solidarios con los humildes.12:16 háganse … humildes. Alt. estén dispuestos a ocuparse en oficios humildes. No se crean los únicos que saben.

17No paguen a nadie mal por mal. Procuren hacer lo bueno delante de todos. 18Si es posible, y en cuanto dependa de ustedes, vivan en paz con todos. 19No tomen venganza, queridos hermanos, sino dejen el castigo en las manos de Dios, porque está escrito: «Mía es la venganza; yo pagaré»,12:19 Dt 32:35. dice el Señor. 20Antes bien,

«Si tu enemigo tiene hambre, dale de comer;

si tiene sed, dale de beber.

Actuando así, harás que se avergüence de su conducta».12:20 harás … conducta. Lit. ascuas de fuego amontonarás sobre su cabeza (Pr 25:21,22).

21No te dejes vencer por el mal; al contrario, vence el mal con el bien.