Walawi 25 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 25:1-55

Mwaka Wa Sabato

(Kumbukumbu 15:1-11)

125:1 Kut 19:11Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai, 225:2 Kut 23:10; Law 26:34-35; 2Nya 36:21“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana. 325:3 Kut 23:10; 25:4Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake. 425:4 Law 26:35; 2Nya 36:21; Isa 36:16; 37:30Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi. 525:5 2Fal 19:29; Mwa 40:10; Hes 6:3; 13:20; Kum 23:24; Neh 13:15; Isa 5:2; 37:30Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko. 6Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu, 725:7 Kut 23:11vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.

Mwaka Wa Yubile

8“ ‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa. 925:9 Law 16:29; 23:24; Hes 10:8; Yos 6:4; Amu 3:27; 7:16; 1Sam 13:3; Isa 27:13; Zek 9:14; Kut 30:10Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote. 1025:10 Isa 61:1; Yer 34:8, 15, 17; Lk 4:19; Law 27:17, 21; Hes 36:4; Eze 46:17; Kut 20:2; Ezr 6:3; Gal 5:1Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile25:10 Yubile ni baragumu iliopigwa kila mwaka wa hamsini; ni Sabato ya nchi ya kila mwaka wa hamsini uliokuwa mwaka wa ukombozi, yaani kuachia huru. kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake. 11Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa. 12Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.

13“ ‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.

1425:14 Law 19:13; 1Sam 12:3-4; 1Kor 6:8; Za 10:18; Mik 2:2“ ‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine. 1525:15 Law 27:18, 23Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno. 16Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao. 1725:17 Law 19:13, 14, 32; Ay 31:16; Mit 22:22; Yer 7:5-6; 21:12; 22:3; Zek 7:9-10; 1The 4:6; Mit 14:31; Eze 22:29Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

1825:18 Mwa 26:5; Law 26:4-5; Kum 12:10; 33:28; Ay 5:22; Za 4:8; Yer 23:6; 30:10; 32:37; 33:16; Eze 28:26; 34:25; 38:14“ ‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi. 1925:19 Law 26:4; Kum 11:14; 28:12; Isa 55:10; Mt 6:25; Hes 11:4-13; 2Fal 6:15Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama. 20Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?” 2125:21 Kum 28:8-12; Za 133:3; 134:3; 147:13; Eze 44:30; Hag 2:19; Mal 3:10; Kut 16:5Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu. 2225:22 Law 26:10; 2Fal 19:29; Yos 5:11Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.

2325:23 Hes 36:7; 1Fal 21:3; Eze 46:18; Kut 19:5; Mwa 23:4; Ebr 11:13“ ‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu. 2425:24 Rut 4:7; Yer 32:8Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.

2525:25 Rut 2:20; 4:4; Yer 32:7; Law 27:13-31“ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza. 26Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa, 27ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake. 28Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.

29“ ‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa. 30Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile. 31Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.

3225:32 Hes 35:1-8; Yos 21:2“ ‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki. 33Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli. 3425:34 Hes 35:2-5; Eze 48:14; Mdo 4:36Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.

3525:35 Kum 24:14-15; 15:8; Za 37:21-26; Mit 21:26; Lk 6:35; Mdo 11:29; Rum 12:18; 1Yn 3:17; Kum 15:7“ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako. 3625:36 Kut 22:25; Yer 15:10; Law 19:32; Kum 23:19; Neh 5:7; Za 15:5; Mit 28:8; Eze 18:8Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako. 3725:37 Kut 22:25Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida. 3825:38 Mwa 10:19; 17:7; Law 11:45Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.

3925:39 1Fal 5:13; 9:23; Yer 34:14; Kut 21:2; 22:3; Kum 15:12“ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa. 40Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile. 41Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake. 4225:42 Rum 6:22; 1Kor 7:23Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa. 4325:43 Kut 1:13; Eze 34:4; Kol 4:1; Mwa 42:18; Isa 47:6; Efe 6:9; Kum 25:18; Mal 3:5Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.

44“ ‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa. 45Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako. 46Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.

4725:47 Neh 5:5; Ay 24:9“ ‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni, 48anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa: 49Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe. 5025:50 Ay 7:1; 14:6; Isa 16:14; 21:16Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka. 51Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye. 52Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake. 5325:53 Kol 4:1Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.

54“ ‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile, 5525:55 Law 11:44-45kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Левит 25:1-55

Субботний год

1Вечный сказал Мусо на горе Синай:

2– Говори с исроильтянами и скажи им: «Когда вы войдёте в землю, которую Я отдаю вам, пусть земля отдыхает каждый седьмой год во славу Вечного. 3Шесть лет засевайте поле, обрезайте виноградник и собирайте урожай. 4Но в седьмой год пусть у земли будет суббота покоя, суббота Вечного. Не засевайте поле и не обрезайте виноградник. 5Не убирайте того, что выросло само по себе, и не собирайте гроздья с необрезанных лоз. Пусть у земли будет год покоя. 6Всё, что произрастит земля в седьмой год, будет вам пищей – вам, вашим рабам и рабыням, наёмным слугам, живущим у вас поселенцам, 7вашему скоту и диким зверям вашей земли. Всё, что произведёт земля, можно есть».

Юбилейный год

8«Отсчитайте семь субботних лет – семь раз по семь лет, – чтобы семь субботних лет составили сорок девять лет. 9В десятый день седьмого месяца протрубите в рог; в День очищения протрубите в рог по всей вашей земле. 10Освятите пятидесятый год и возвестите свободу по всей земле всем её обитателям. Он будет для вас юбилейным; каждый из вас должен вернуться к своему владению, каждый – к своему клану. 11Пятидесятый год будет для вас юбилейным; не сейте и не жните то, что выросло само, и не собирайте ягоды с необрезанных лоз. 12Это юбилейный год: пусть он будет свят для вас; ешьте лишь то, что вырастет в поле само по себе.

13В этот юбилейный год пусть каждый вернётся к своему земельному наделу.

14Продавая землю соплеменнику или покупая у него, не обманывайте друг друга. 15Покупая, платите лишь за число лет, остающихся до следующего юбилейного года. А продавец пусть берёт лишь за число лет, оставшихся для сбора урожая. 16Если осталось много лет, повышайте цену, а если мало, понижайте, ведь продаётся только число урожаев. 17Не обманывайте друг друга; бойтесь вашего Бога. Я – Вечный, ваш Бог.

18Соблюдайте Мои установления и прилежно исполняйте Мои законы, и вы будете безопасно жить на этой земле. 19Тогда земля будет плодоносить, и вы будете есть досыта и жить на ней в безопасности. 20Вы спросите: „Что нам есть в седьмой год, если мы не посеем и не соберём урожай?“ 21В шестой год Я так благословлю вас, что земля принесёт трёхлетний урожай. 22Приступив к севу в восьмом году, вы ещё будете есть прежний урожай. Вы будете есть его, пока не подоспеет жатва девятого года».

Восстановление прав собственности

23«Землю нельзя продавать навсегда, потому что земля Моя, а вы у Меня чужеземцы и поселенцы. 24При всякой покупке земли разрешайте выкупать её обратно.

25Если твой соплеменник обеднеет и продаст часть владения, то его ближайший родственник придёт и выкупит то, что он продал. 26Если же у него нет никого, кто выкупил бы для него, но он преуспеет и найдёт средства для выкупа сам, 27пусть сосчитает годы со времени продажи и выплатит разницу тому, кому он продал. Тогда он может вернуться к своему владению. 28А если он не найдёт средств, чтобы возвратить ему, то проданное им останется во владении у покупателя до юбилейного года, а потом земля будет возвращена тому, кто её продал. И тогда он может вернуться к своему владению.

29Если кто-то продаст жилой дом в обнесённом стеной городе, он сохраняет право выкупа целый год после продажи. В течение этого времени он может выкупить его. 30Если жилой дом в обнесённом стеной городе не выкуплен до того, как прошёл полный год, он навеки отходит к покупателю и его потомкам. Он не будет возвращён даже в юбилейный год. 31Но дома в селениях, не обнесённых стенами, считаются открытым полем. Их можно выкупать. Их нужно возвращать в юбилейный год.

32Но у левитов всегда есть право выкупать дома в городах, которыми они владеют. 33Собственность левитов – дом в городе, которым они владеют, – подлежит выкупу и должна возвращаться в юбилейный год, потому что дома в городах левитов – это их собственность у исроильтян. 34Но пастбища при их городах продавать нельзя – это их вечное владение».

Освобождение рабов

35«Если твой соплеменник обеднеет и впадёт в зависимость от тебя, помоги ему, как помог бы чужеземцу или поселенцу, чтобы он жил с тобой и дальше. 36Не бери с него процентов; бойся своего Бога, чтобы твой соплеменник жил с тобой и дальше. 37Не одалживай ему под проценты и не продавай ему пищу ради прибыли. 38Я – Вечный, ваш Бог, Который вывел вас из Египта, чтобы дать вам землю Ханона и быть вашим Богом.

39Если твой соплеменник обеднеет и продаст себя, не заставляй его работать как раба. 40Пусть он будет у тебя как наёмный слуга или поселенец. Он будет работать на тебя до юбилейного года. 41Тогда он со своими детьми уйдёт от тебя и вернётся к своему клану и владению предков. 42Исроильтяне – Мои слуги, которых Я вывел из Египта, их нельзя продавать в рабство. 43Повелевая ими, не будь жесток. Бойся своего Бога.

44Пусть твои рабы и рабыни будут из народов, которые вокруг вас; покупайте себе рабов из их числа. 45Ещё покупайте их из поселенцев, которые живут у вас, из членов их кланов, которые родились в вашей стране, и они станут вашей собственностью. 46Вы можете передавать их по наследству в собственность вашим детям. С ними вы можете обращаться как с рабами, но не будьте жестоки, повелевая своими соплеменниками-исроильтянами.

47Если живущий у тебя чужеземец или поселенец разбогатеет, а твой соплеменник обеднеет и продаст себя живущему у тебя чужеземцу или члену его семьи, 48то после того, как он себя продал, у него остаётся право на выкуп. Его может выкупить родственник: 49дядя, двоюродный брат или любой кровный родственник в его клане. А если он преуспеет, то может выкупить себя сам. 50Пусть он и его покупатель посчитают время с того года, в который он продал себя, до юбилейного года. Цена за его освобождение должна соответствовать плате наёмного слуги за эти годы. 51Если остаётся много лет, он должен заплатить за свой выкуп большую долю цены, заплаченной за него. 52Если же до юбилейного года остаётся мало лет, пусть он подсчитает их и заплатит за свой выкуп в соответствии с ними. 53Во все годы с ним следует обращаться как с наёмным слугой; следи, чтобы его хозяин, повелевая им, не был жесток.

54Даже если он не будет выкуплен как сказано, он и его дети выйдут на свободу в юбилейный год, 55потому что исроильтяне служат Мне. Они Мои слуги, которых Я вывел из Египта. Я – Вечный, ваш Бог».