Wakolosai 2 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 2:1-23

12:1 Kol 1:29; 4:12; 4:13, 15, 16; Ufu 1:11Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi. 22:2 Efe 6:22; Kol 4:8; Rum 16:25Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe, 32:3 Isa 11:2; Yer 23:5; Rum 11:33; 1Kor 1:24, 30ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa. 42:4 Rum 16:18Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi. 52:5 1Kor 5:4; 1The 2:17Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.

Ukamilifu Wa Maisha Katika Kristo

62:6 Yn 13:13; Kol 1:10Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake, 72:7 Efe 3:17; 4:22mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.

82:8 1Tim 6:20; Kol 2:20; Gal 4:2Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.

92:9 Yn 1:16Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu, 102:10 Efe 1:22; Mt 28:18nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka. 112:11 Rum 2:29; Flp 3:3; Gal 5:24Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo, 122:12 Mt 28:19; Rum 6:5; Mdo 2:24mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.

132:13 Efe 2:15; 2:5; 4:32Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote, 142:14 Efe 2:15; 1Pet 2:24akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake. 152:15 Kol 2:10; Efe 6:12; Mt 12:29; Lk 10:18; Yn 12:31Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.

162:16 Rum 14:3, 4; Mk 7:19; Rum 14:17; Law 23:2; Rum 14:5Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato. 172:17 Ebr 8:5; 10:1Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo. 182:18 Kol 2:23; 1Kor 9:24; Flp 3:14Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu. 192:19 Efe 1:22; 1Kor 2:8; Gal 4:3, 9, 14, 16Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.

Maonyo Dhidi Ya Walimu Wa Uongo

20Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri: 212:21 1Tim 4:3“Msishike! Msionje! Msiguse!”? 222:22 1Kor 6:13; Isa 29:13; Mt 15:9; Tit 1:14Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu. 232:23 Kol 2:18Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.

Knijga O Kristu

Kološanima 2:1-23

1Želim da znate koliko sam se mučio za vas, za Crkvu u Laodiceji i za sve one koji me još nisu osobno upoznali. 2Želim da se njihova srca ohrabre, povezana u ljubavi, da dobiju bogatu i punu spoznaju Božje tajne: Krista. 3U njemu su skrivena sva bogatstva mudrosti i spoznaje.

4Govorim vam to da vas nitko ne prevari uvjerljivim riječima. 5Iako sam daleko od vas, u mislima sam s vama. Veoma me raduje što živite kako treba i što je vaša vjera u Krista čvrsta.

Sloboda od pravila i novi život u Kristu

6Kako ste prihvatili Krista za Gospodina, tako nastavite s njime živjeti. 7Budite u njemu ukorijenjeni pa ćete se izgrađivati i učvršćivati u vjeri kako ste i poučeni. Obilno zahvaljujte Bogu.

8Nemojte da vas tko odvuče ispraznim mudrovanjem koje se temelji na ljudskim predajama i na počelima ovoga svijeta, a ne na Kristu. 9Jer u Kristu doslovce prebiva sva punina božanstva, 10a vi ste ispunjeni kroz zajedništvo s njime, koji je iznad svakoga poglavarstva i vlasti u svemiru.

11Kad ste došli Kristu, “obrezani” ste, ali ne tjelesno. Bio je to duhovni zahvat—“odrezana” je vaša grešna narav. 12Jer s Kristom ste ukopani pri krštenju. I s njim ste uskrsnuli u novi život jer ste se pouzdali u moćnu Božju silu, koja je i Krista podignula od mrtvih.

13Bili ste nekoć mrtvi zbog svojih prijestupa i zbog toga što vaša grešna narav još nije bila “odrezana”. Tada vas je Bog oživio s Kristom. Oprostio nam je sve prijestupe. 14Izbrisao je zadužnicu čije su odredbe bile protiv nas. Pribio ju je na Kristov križ i uništio. 15Tako je Bog razoružao zle vladare i vlasti. Javno ih je osramotio pobjedom na Kristovu križu.

16Neka vas zato nitko ne osuđuje zbog jela, pića ili zbog svetkovanja blagdana, mlađaka ili subote. 17Jer ta su pravila bila tek sjena prave stvarnosti—Krista. 18Ne dajte da vam oni koji uživaju u lažnoj poniznosti i štovanju anđela kažu kako niste zaslužili nagradu. Takvi ljudi, oholi zbog svoje tjelesne pameti, unedogled nabrajaju pojedinosti viđenja koja su imali. 19Ali ne drže se Krista, glave Tijela koje je snažno povezano i koje raste samo dobivajući hranu i snagu od Boga.

20Ako ste zaista umrli s Kristom, onda vas je on oslobodio temeljnih počela ovoga svijeta. Zašto se onda, kao da još pripadate ovomu svijetu, podvrgavate propisima kao što su: 21“Ne jedi! Ne kušaj! Ne takni!” 22Takva pravila obična su ljudska umotvorina jer se odnose na stvari koje uporabom nestaju. 23Ti propisi prividno su mudri zbog samozvanog bogoštovlja, poniznosti i trapljenja tijela, ali ne pomažu čovjeku da nadvlada svoje zle misli i želje.