Wakolosai 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 1:1-29

Salamu

11:1 1Kor 1:1; 2Kor 1:1; Mdo 16:1Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu:

21:2 Kol 4:18; Rum 1:7Kwa ndugu watakatifu na waaminifu katika Kristo, waishio Kolosai:

Neema na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu ziwe nanyi.

Shukrani Na Maombi

31:3 Rum 1:8Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea ninyi, 41:4 Gal 5:6; Mdo 9:13; Efe 1:15; Flm 5kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo wenu mlio nao kwa watakatifu wote: 51:5 Kol 1:23; 1The 5:8; Tit 1:2; 1Pet 1:4; 2Tim 2:15imani na upendo ule utokao katika tumaini mlilowekewa akiba mbinguni, na ambalo mmesikia habari zake katika neno la kweli, yaani, ile Injili 61:6 Kol 1:23; Rum 10:18; Yn 15:16iliyowafikia ninyi. Duniani kote Injili hii inazaa matunda na kuenea kama ilivyokuwa kwenu tangu siku ile mlipoisikia na kuielewa neema ya Mungu katika kweli yote. 71:7 Kol 4:12; Flm 23; Kol 4:7Mlijifunza habari zake kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu mpendwa, yeye aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu, 81:8 Rum 15:30ambaye pia ametuambia kuhusu upendo wenu katika Roho.

91:9 Kol 1:4; Efe 1:15; Rum 1:10; Efe 5:17Kwa sababu hii, tangu siku ile tuliposikia habari zenu, hatujakoma kuomba kwa ajili yenu na kumsihi Mungu awajaze ninyi maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote ya kiroho na ufahamu. 101:10 Efe 4:1; 2Kor 5:9; Kol 1:6Nasi tunaomba haya ili mpate kuishi maisha yanayostahili mbele za Bwana, na mpate kumpendeza kwa kila namna: mkizaa matunda kwa kila kazi njema, mkikua katika kumjua Mungu, 111:11 Flp 4:13; Efe 4:2mkiwa mmetiwa nguvu kwa uwezo wote kwa kadiri ya nguvu yake yenye utukufu, ili mpate kuwa na wingi wa saburi na uvumilivu. Nanyi kwa furaha 121:12 Efe 5:20; Mdo 20:32; 26:18mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru. 131:13 Mdo 26:13; 2Pet 1:11; Mt 3:17Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa, 141:14 Rum 3:24; Efe 1:7ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.

Ukuu Wa Kristo

151:15 Yn 14:9; 1:18; 1Tim 1:17; Ebr 11:27; Kol 1:18Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 161:16 Yn 1:3; Efe 1:20, 21; Rum 11:36Kwake yeye vitu vyote vilivyoko mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya enzi au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake. 171:17 Yn 1:2Yeye alikuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja. 181:18 Efe 1:22; Kol 1:24; 1Kor 12:27; Za 89:27; Rum 8:29Yeye ndiye kichwa cha mwili, yaani kanisa, naye ndiye mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, ili yeye awe mkuu katika vitu vyote. 191:19 Efe 1:15; Yn 1:16Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba utimilifu wake wote ukae ndani yake, 201:20 Rum 5:10; Efe 1:10; Lk 2:14; Efe 2:13na kwa njia yake aweze kuvipatanisha vitu vyote na yeye mwenyewe, viwe ni vitu vilivyo duniani au vilivyo mbinguni, kwa kufanya amani kwa damu yake, iliyomwagika msalabani.

211:21 Rum 5:10; Efe 2:3Hapo kwanza mlikuwa mmetengana na Mungu, na mlikuwa adui zake katika nia zenu kwa sababu ya mienendo yenu mibaya. 221:22 Kol 1:20; Rum 5:10; 7:4; 2Kor 4:14; Efe 1:4; 5:27Lakini sasa Mungu amewapatanisha ninyi kwa njia ya mwili wa Kristo kupitia mauti, ili awalete mbele zake mkiwa watakatifu, bila dosari wala lawama, 23ikiwa mnaendelea katika imani yenu mkiwa imara na thabiti, pasipo kuliacha tumaini lililoahidiwa katika Injili. Hii ndiyo ile Injili mliyoisikia, ambayo imehubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu, na ambayo mimi Paulo nimekuwa mtumwa wake.

Taabu Ya Paulo Kwa Ajili Ya Kanisa

241:24 2Kor 6:10; 1:5; 1Kor 12:27Sasa nafurahia kule kuteseka kwangu kwa ajili yenu, na katika mwili wangu ninatimiliza yale yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa. 251:25 Kol 1:23; 1Kor 3:5; Efe 3:2; Ebr 4:12Mimi nimekuwa mtumishi wa kanisa kwa wajibu alionipa Mungu ili kuwaletea ninyi Neno la Mungu kwa ukamilifu: 261:26 Rum 16:25Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. 271:27 Mt 13:11; Rum 2:11, 24; 8:10Kwao, Mungu amechagua kujulisha miongoni mwa watu wa Mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, ambayo ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.

281:28 Kol 3:16; 1Kor 2:6, 7; Mt 5:48; Efe 5:27Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja akiwa amekamilika katika Kristo. 291:29 1Kor 15:10; 2Kor 11:23; Kol 2:1; Efe 1:19; 3:7Kwa ajili ya jambo hili, ninajitaabisha, nikijitahidi kwa kadiri ya nguvu zake ambazo hutenda kazi ndani yangu kwa uweza mwingi.

New International Reader’s Version

Colossians 1:1-29

1I, Paul, am writing this letter. I am an apostle of Christ Jesus just as God planned. Our brother Timothy joins me in writing.

2We are sending this letter to you, our brothers and sisters in Colossae. You belong to Christ. You are holy and faithful.

May God our Father give you grace and peace.

Paul Prays and Gives Thanks

3We always thank God, the Father of our Lord Jesus Christ, when we pray for you. 4We thank him because we have heard about your faith in Christ Jesus. We have also heard that you love all God’s people. 5Your faith and love are based on the hope you have. What you hope for is stored up for you in heaven. You have already heard about it. You were told about it when the true message was given to you. I’m talking about the good news 6that has come to you. In the same way, the good news is bearing fruit. It is bearing fruit and growing all over the world. It has been doing that among you since the day you heard it. That is when you really understood God’s grace. 7You learned the good news from Epaphras. He is dear to us. He serves Christ together with us. He faithfully works for Christ and for us among you. 8He also told us about your love that comes from the Holy Spirit.

9That’s why we have not stopped praying for you. We have been praying for you since the day we heard about you. We keep asking God to fill you with the knowledge of what he wants. We pray he will give you the wisdom and understanding that the Spirit gives. 10Then you will be able to lead a life that is worthy of the Lord. We pray that you will please him in every way. So we want you to bear fruit in every good thing you do. We pray that you will grow to know God better. 11We want you to be very strong, in keeping with his glorious power. We want you to be patient. We pray that you will never give up. 12We want you to give thanks with joy to the Father. He has made you fit to have what he will give to all his holy people. You will all receive a share in the kingdom of light. 13He has saved us from the kingdom of darkness. He has brought us into the kingdom of the Son he loves. 14Because of what the Son has done, we have been set free. Because of him, all our sins have been forgiven.

The Son of God Is Better Than Everything Else

15The Son is the exact likeness of God, who can’t be seen. The Son is first, and he is over all creation. 16All things were created in him. He created everything in heaven and on earth. He created everything that can be seen and everything that can’t be seen. He created kings, powers, rulers and authorities. All things have been created by him and for him. 17Before anything was created, he was already there. He holds everything together. 18And he is the head of the body, which is the church. He is the beginning. He is the first to be raised from the dead. That happened so that he would be far above everything. 19God was pleased to have his whole nature living in Christ. 20God was pleased to bring all things back to himself. That’s because of what Christ has done. These things include everything on earth and in heaven. God made peace through Christ’s blood, by his death on the cross.

21At one time you were separated from God. You were enemies in your minds because of your evil ways. 22But because Christ died, God has brought you back to himself. Christ’s death has made you holy in God’s sight. So now you don’t have any flaw. You are free from blame. 23But you must keep your faith steady and firm. You must not move away from the hope the good news holds out to you. This is the good news that you heard. It has been preached to every creature under heaven. I, Paul, now serve the good news.

Paul’s Work for the Church

24I am happy because of what I am suffering for you. My suffering joins with and continues the sufferings of Christ. I suffer for his body, which is the church. 25I serve the church. God appointed me to bring the complete word of God to you. 26That word contains the mystery that has been hidden for many ages. But now it has been made known to the Lord’s people. 27God has chosen to make known to them the glorious riches of that mystery. He has made it known among the Gentiles. And here is what it is. Christ is in you. He is your hope of glory.

28Christ is the one we preach about. With all the wisdom we have, we warn and teach everyone. When we bring them to God, we want them to be like Christ. We want them to be grown up as people who belong to Christ. 29That’s what I’m working for. I work hard with all the strength of Christ. His strength works powerfully in me.