Wagalatia 4 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Wagalatia 4:1-31

1Lile nisemalo ni kwamba wakati wote mrithi bado ni mtoto, hana tofauti na mtumwa, ingawa ndiye mmiliki wa mali yote. 2Yeye huwa yuko chini ya uangalizi wa walezi na wadhamini mpaka ufike wakati uliowekwa na baba yake. 34:3 Gal 4:9; 5:1; Kol 2:8, 20; Ebr 9:10Vivyo hivyo na sisi, tulipokuwa bado watoto wadogo, tulikuwa utumwani chini ya taratibu za kawaida za ulimwengu. 44:4 Mk 1:15; Rum 5:6; Efe 1:10; Yn 3:17; 1:14; Lk 2:27Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe, ambaye alizaliwa na mwanamke, akazaliwa chini ya sheria, 54:5 Rum 3:24; Yn 1:12; Rum 8:14kusudi awakomboe wale waliokuwa chini ya sheria, ili tupate kupokea zile haki kamili za kufanywa watoto wa Mungu. 64:6 Mdo 16:7; Rum 5:5; 8:15, 16Kwa sababu ninyi ni watoto wa Mungu, Mungu amemtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, anayelia, “Abba,4:6 Abba ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni Baba; lingeweza kutumiwa tu na mtoto wa kuzaa. Baba.” 74:7 Rum 8:17; Gal 3:29Kwa hiyo, wewe si mtumwa tena, bali ni mtoto, kwa kuwa wewe ni mtoto, Mungu amekufanya wewe pia kuwa mrithi kwa kupitia Kristo.

Paulo Awashawishi Wagalatia

84:8 Rum 1:28; 1Kor 1:21; 15:34; 1The 4:5; 2The 1:8; Gal 4:3Zamani, mlipokuwa hammjui Mungu, mlikuwa watumwa wa viumbe ambavyo kwa asili si Mungu. 94:9 1Kor 8:3; Gal 4:3; Kol 2:20Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu, au zaidi mmejulikana na Mungu, inakuwaje mnarejea tena katika zile kanuni za kwanza zenye udhaifu na upungufu? Mnataka ziwafanye tena watumwa? 104:10 Rum 14:5; Kol 2:16Mnaadhimisha siku maalum, miezi, nyakati na miaka! 114:11 1The 3:5; Gal 2:2; 5:2, 4Nina hofu juu yenu, kwamba kazi niliyofanya kwa ajili yenu inaweza kuwa nimejitaabisha bure.

124:12 Rum 7:1; Gal 6:18; 2Kor 2:5Ndugu zangu, nawasihi mwe kama mimi, kwa sababu mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea jambo lolote baya. 134:13 1Kor 2:3; 2Kor 11:30; 12:7, 9; Gal 1:6Ninyi mwajua kwamba ni kwa ajili ya udhaifu wangu niliwahubiria Injili. 144:14 Mt 10:40; 2Sam 19:27; Mal 2:7; Zek 12:8; Mt 10:40; Lk 10:16Ingawa hali yangu iliwatia majaribuni, hamkunidharau wala kunidhihaki, bali mlinikaribisha kama malaika wa Mungu, kama vile Kristo Yesu. 15Ile hali ya furaha mliyokuwa nayo imekwenda wapi? Naweza kushuhudia kwamba, kama ingewezekana mngengʼoa macho yenu na kunipa mimi. 164:16 Gal 2:5, 14; Amo 5:10Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa kuwaambia kweli?

174:17 Gal 2:4, 12; Rum 10:12; 1Kor 11:2Hao wana shauku ya kuwapata lakini si kwa kusudi zuri. Wanachotaka ni kuwatenga mbali nasi, ili ninyi mpate kuwaonea wao shauku. 184:18 Gal 4:13, 14Ni vizuri wakati wote kuwa na shauku kwa ajili ya kusudi zuri, si wakati nikiwa pamoja nanyi tu. 194:19 1The 2:11; Rum 8:29; Efe 4:13Watoto wangu wapendwa, ambao kwa mara nyingine ninawaonea utungu, ninatamani kwamba Kristo aumbike ndani yenu. 20Natamani kama ningekuwa pamoja nanyi sasa, pengine ningebadilisha sauti yangu. Kwa maana nina wasiwasi kwa ajili yenu.

Mfano Wa Hagari Na Sara

214:21 Rum 2:12Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je, hamjui sheria inavyosema? 22Kwa maana imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wawili, mmoja wa mwanamke mtumwa na wa pili wa mwanamke huru. 234:23 Gal 4:28, 29; Rum 9:7, 8; Mwa 17:16-21; 18:10-14; 4:24Lakini, mtoto wa mwanamke mtumwa alizaliwa kwa mapenzi ya mwili, na yule mwingine wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.

24Mambo haya yanaweza kuchukuliwa kama mfano. Kwa maana hao wanawake wawili ni mfano wa maagano mawili: Agano la kwanza, ni lile lililofanyika katika Mlima Sinai, lizaalo watoto wa utumwa. Hili ndilo huyo Hagari. 25Basi Hagari anawakilisha Mlima Sinai ulioko Arabuni, na unafanana na Yerusalemu ya sasa ambayo iko utumwani pamoja na watoto wake. 264:26 Flp 2:3; Ebr 12:22; Isa 2:2; Ufu 3:12; 21:2, 10Lakini Yerusalemu wa juu ni huru, nayo ndiye mama yetu. 274:27 Isa 54:1Kwa maana imeandikwa:

“Furahi, ewe mwanamke tasa,

wewe usiyezaa;

paza sauti, na kuimba kwa furaha,

wewe usiyepatwa na utungu wa kuzaa;

kwa maana watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume.”

284:28 Mdo 3:25; Rum 9:8; Gal 3:29Basi, sisi ndugu zangu, ni kama Isaki, tu watoto wa ahadi. 294:29 Mwa 21:9; Gal 5:11; 6:12Lakini, kama vile ilivyokuwa siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomchokoza yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo hata sasa. 304:30 Mwa 21:10Lakini Maandiko yasemaje? “Mwondoe mwanamke mtumwa pamoja na mwanawe, kwa sababu mwana wa mwanamke mtumwa kamwe hatarithi pamoja na mwana wa aliye huru.” 314:31 Rum 7:4; Gal 4:22Kwa hiyo ndugu zangu, sisi si watoto wa mwanamke mtumwa, bali wa yule aliye huru.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

加拉太书 4:1-31

儿子与奴仆

1然而,继承人还年幼时,虽然身为产业的主人,实际上和奴仆没有分别。 2他一样要受监护人和管家的约束,一直到他父亲指定他继承产业的日子为止。 3我们也一样,在孩童时期受世界基本规条的辖制。 4然而,时候一到,上帝就差遣自己的儿子借着一位女子降生,并受律法的约束, 5为要救赎一切受律法约束的人,使我们成为祂的儿女。

6我们4:6 “我们”希腊文是“你们”。既然成为儿女,上帝就差遣祂儿子的灵进入我们的心里,呼求:“阿爸,父啊!” 7由此可见,你们从今以后不再是奴仆,而是儿女。既然身为儿女,就可以靠着上帝成为产业继承人。

保罗对加拉太人的关怀

8从前,你们不认识上帝,做那些假神的奴隶。 9现在,你们既然认识了上帝,或者更应该说是上帝认识了你们,为什么还要回到那些脆弱无用的基本规条之下,甘愿再做它们的奴隶呢? 10你们竟然还在拘守什么日子、月份、节期和年份! 11我真担心我在你们身上的一番心血都枉费了。

12弟兄姊妹,我劝你们现在要像我一样,因为我已经像你们一样。你们向来没有亏待过我。 13你们知道,当初是因为我生病才有机会首次向你们传福音。 14那时,你们虽然因为我生病而受累,却没有轻视我、嫌弃我,反而接待我,就像接待上帝的天使,接待基督耶稣一样。 15我可以为你们作证,如果可能的话,你们那时就是把眼睛剜出来给我,也心甘情愿。你们当初的善意哪里去了? 16现在我因为告诉你们真理,就成了你们的仇人吗?

17那些人非常热心地对待你们,其实他们心怀不轨,想要离间你们和我们的关系,使你们热心地对待他们。 18有人热心待你们当然很好,但总要动机纯正、始终如一,不应该只是我和你们在一起时才热心待你们。 19孩子们,为了你们,我像一位母亲再次经历生产的剧痛,一直到基督的生命在你们里面成形。 20我恨不得立刻赶到你们身边,换种口气说话,因为我为你们困惑不安。

夏甲与撒拉的例子

21你们这些甘愿在律法之下的人啊!告诉我,你们没听过律法怎么说吗? 22律法书上说:亚伯拉罕有两个儿子,一个是婢女生的,一个是主母生的。 23婢女的儿子是按着人的意愿生的,主母的儿子是按着上帝的应许生的。 24这些事都有寓意,两个妇人代表两个约。夏甲代表颁布于西奈山的约,她生的孩子是奴仆。 25夏甲代表阿拉伯西奈山,相当于现今的耶路撒冷,她和她的儿女都是奴仆。 26那天上的耶路撒冷则是自由的,是我们的母亲。 27因为圣经上说:

“不生育、未生养的妇人啊,

要快乐;

未曾生产的女子啊,

要高声欢呼,

因为没有丈夫的比有丈夫的儿女更多。”4:27 以赛亚书54:1

28弟兄姊妹,你们都像以撒一样是照着上帝的应许出生的。 29当时,那按着人的意愿生的儿子迫害那靠着圣灵生的儿子,现在的情况也和当时一样。 30但圣经上怎么说呢?圣经上说:“赶走婢女和她的儿子,因为婢女的儿子不能与主母的儿子一同承受产业。”4:30 创世记21:10 31弟兄姊妹,这样看来,我们不是婢女的儿女,而是主母的儿女。