Wagalatia 3 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Wagalatia 3:1-29

Imani Au Kushika Sheria?

13:1 Gal 5:7; 1Kor 1:23Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa. 23:2 Rum 10:17; Yn 20:22; Gal 3:5, 10; 2:16; Rum 10:17Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia? 33:3 Gal 4:9; Ebr 7:16; 9:10Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili? 43:4 Ebr 10:35, 36; 2Yn 8Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure! 53:5 1Kor 12:10; 2Kor 3:8Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?

63:6 Mwa 15:6; Rum 4:3Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.” 73:7 Yn 8:39; Rum 4:11, 12, 16Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu. 83:8 Mwa 18:18; Mdo 3:25Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.” 93:9 Rum 4:16; Gal 3:7; Rum 4:18-22Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.

Sheria Na Laana

103:10 Kum 27:26; Yer 11:3Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.” 113:11 Gal 2:16; Hab 2:4; Rum 1:17; Ebr 10:38Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.” 123:12 Rum 4:4, 5; Law 18:5; Neh 9:29; Eze 20:11Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.” 133:13 Rum 8:3; 2Kor 5:21; 4:5; Kum 21:23Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.” 143:14 Rum 4:9, 16; Isa 32:15; 44:3; Yer 31:33; 32:40; Eze 11:19Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.

Sheria Na Ahadi

153:15 Ebr 9:17; Rum 7:1Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii. 163:16 Mwa 17:19; Za 132:11; Mik 7:20; Lk 1:55; Rum 4:13, 16Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo. 173:17 Mwa 15:13, 14; Kut 12:40; Mdo 7:6Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile. 183:18 Rum 4:14Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.

Kusudi La Sheria

193:19 Rum 5:20; 3:16; Kum 33:2; Mdo 7:53; Kut 20:19Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi. 203:20 1Tim 2:5; Ebr 8:6; 9:15; 12:24Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.

213:21 Gal 2:17; Rum 7:12; Gal 2:21Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria. 223:22 Rum 3:9-19; 11:32Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.

233:23 Rum 11:32; Gal 3:25Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe. 243:24 Gal 3:19; Rum 10:4; 4:15; Gal 2:16Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani. 253:25 Rum 7:4; 10:4Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.

Watoto Wa Mungu

263:26 Rum 8:14; Yn 1:12; Rum 8:15, 16; Gal 4:5; 1Yn 3:1Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani. 273:27 Rum 6:3; 13:14; Mt 28:19Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo. 283:28 1Kor 12:13; Kol 3:11; Mwa 1:27; 5:2; Yoe 2:29; Yn 10:16Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu. 293:29 1Kor 3:22; Gal 3:16; Lk 3:8; Rum 8:17; Gal 3:16Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.

New International Version

Galatians 3:1-29

Faith or Works of the Law

1You foolish Galatians! Who has bewitched you? Before your very eyes Jesus Christ was clearly portrayed as crucified. 2I would like to learn just one thing from you: Did you receive the Spirit by the works of the law, or by believing what you heard? 3Are you so foolish? After beginning by means of the Spirit, are you now trying to finish by means of the flesh?3:3 In contexts like this, the Greek word for flesh (sarx) refers to the sinful state of human beings, often presented as a power in opposition to the Spirit. 4Have you experienced3:4 Or suffered so much in vain—if it really was in vain? 5So again I ask, does God give you his Spirit and work miracles among you by the works of the law, or by your believing what you heard? 6So also Abraham “believed God, and it was credited to him as righteousness.”3:6 Gen. 15:6

7Understand, then, that those who have faith are children of Abraham. 8Scripture foresaw that God would justify the Gentiles by faith, and announced the gospel in advance to Abraham: “All nations will be blessed through you.”3:8 Gen. 12:3; 18:18; 22:18 9So those who rely on faith are blessed along with Abraham, the man of faith.

10For all who rely on the works of the law are under a curse, as it is written: “Cursed is everyone who does not continue to do everything written in the Book of the Law.”3:10 Deut. 27:26 11Clearly no one who relies on the law is justified before God, because “the righteous will live by faith.”3:11 Hab. 2:4 12The law is not based on faith; on the contrary, it says, “The person who does these things will live by them.”3:12 Lev. 18:5 13Christ redeemed us from the curse of the law by becoming a curse for us, for it is written: “Cursed is everyone who is hung on a pole.”3:13 Deut. 21:23 14He redeemed us in order that the blessing given to Abraham might come to the Gentiles through Christ Jesus, so that by faith we might receive the promise of the Spirit.

The Law and the Promise

15Brothers and sisters, let me take an example from everyday life. Just as no one can set aside or add to a human covenant that has been duly established, so it is in this case. 16The promises were spoken to Abraham and to his seed. Scripture does not say “and to seeds,” meaning many people, but “and to your seed,”3:16 Gen. 12:7; 13:15; 24:7 meaning one person, who is Christ. 17What I mean is this: The law, introduced 430 years later, does not set aside the covenant previously established by God and thus do away with the promise. 18For if the inheritance depends on the law, then it no longer depends on the promise; but God in his grace gave it to Abraham through a promise.

19Why, then, was the law given at all? It was added because of transgressions until the Seed to whom the promise referred had come. The law was given through angels and entrusted to a mediator. 20A mediator, however, implies more than one party; but God is one.

21Is the law, therefore, opposed to the promises of God? Absolutely not! For if a law had been given that could impart life, then righteousness would certainly have come by the law. 22But Scripture has locked up everything under the control of sin, so that what was promised, being given through faith in Jesus Christ, might be given to those who believe.

Children of God

23Before the coming of this faith,3:22,23 Or through the faithfulness of Jesus… 23 Before faith came we were held in custody under the law, locked up until the faith that was to come would be revealed. 24So the law was our guardian until Christ came that we might be justified by faith. 25Now that this faith has come, we are no longer under a guardian.

26So in Christ Jesus you are all children of God through faith, 27for all of you who were baptized into Christ have clothed yourselves with Christ. 28There is neither Jew nor Gentile, neither slave nor free, nor is there male and female, for you are all one in Christ Jesus. 29If you belong to Christ, then you are Abraham’s seed, and heirs according to the promise.