Wafilipi 4 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Wafilipi 4:1-23

14:1 Flp 1:8; 1Kor 16:13Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.

Mausia

24:2 Flp 2:2; 3:16Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana. 34:3 Flp 2:25; Ufu 20:12Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.

44:4 Za 85:6; 97:12; Hab 3:18; Mt 5:12; Rum 12:12; Flp 3:1Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini! 54:5 Za 119:151; 145:18; Ebr 10:37; Yak 5:8, 9Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu. 64:6 Mt 6:25-34; Kol 4:2; 1Pet 5:7; Za 145:18; Efe 6:18; 1Tim 2:1Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. 74:7 Isa 26:3; Yn 14:27; Efe 3:19Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

84:8 1The 5:22; Rum 12:17Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo. 94:9 1Kor 4:16; Rum 12:17Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.

Shukrani Kwa Matoleo Yenu

104:10 2Kor 11:9Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo. 114:11 1Tim 6:6, 8; Ebr 13:5Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote. 124:12 1Kor 4:11; 2Kor 11:9Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa. 134:13 2Kor 12:9; Efe 3:16; Kol 1:11; 1Tim 1:12; 2Tim 4:17Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

144:14 Flp 1:7Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu. 154:15 Flp 1:5; Mdo 16:9; 2Kor 11:8, 9Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi. 164:16 Mdo 17:1; 1The 2:9Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja. 174:17 1Kor 9:11, 12Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu. 184:18 Flp 2:25; 2Kor 2:14Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu. 194:19 Za 23:1; 2Kor 9:8; Rum 2:4Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.

204:20 Gal 1:4; 1The 1:3; 3:11, 13; Rum 11:36Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen.

Salamu Za Mwisho

214:21 Gal 1:2Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu. 224:22 Mdo 9:13Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.

234:23 Rum 16:20; Gal 6:18Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.