Waefeso 4 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version

Waefeso 4:1-32

Umoja Katika Mwili Wa Kristo

14:1 Efe 3:1; Kol 1:10; 1The 2:12Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa. 24:2 Kol 3:12, 13; Efe 1:4Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo. 34:3 Kol 3:14; Rum 15:5Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 44:4 1Kor 12:13Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja. 54:5 1Kor 8:6; 2Kor 11:4; Yud 3; Gal 3:27, 28; Ebr 6:6Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja, 64:6 Rum 11:36; 1Kor 12:6; Mal 2:10; 1Kor 8:6; 12:6; Rum 11:36Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.

74:7 1Kor 12:7, 11; Rum 12:3Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo. 84:8 Kol 2:15; Za 68:18Kwa hiyo husema:

“Alipopaa juu zaidi, 4:8 Juu zaidi hapa ina maana mbingu za mbingu.

aliteka mateka,

akawapa wanadamu vipawa.”

94:9 Yn 3:13; 6:33, 62(Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?4:9 Pande za chini sana za dunia hapa maana yake Sheol kwa Kiebrania, yaani Kuzimu. 104:10 Mdo 1:9, 11; 1Tim 3:16; Ebr 4:14; 7:26; 9:24; Mdo 2:13; Mit 30:1-4; Efe 1:23Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.) 114:11 2Pet 3:2; Mdo 21:8Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu, 124:12 1Kor 12:27; 1Pet 2:5; 2Tim 3:17kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa 134:13 Kol 1:28mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.

144:14 1Kor 14:20; Yn 1:6; Efe 6:11Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu. 154:15 Efe 1:22Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo. 164:16 Kol 2:19Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.

Maisha Ya Zamani Na Maisha Mapya

174:17 Rum 1:21Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao. 184:18 Rum 1:21; Efe 2:12; 2Kor 3:14Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao. 194:19 1Tim 4:2; Rum 1:24; Kol 3:5Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.

20Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo. 214:21 Efe 1:13Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu. 224:22 1Pet 2:1; Rum 6:6Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu, 234:23 Kol 3:10ili mfanywe upya roho na nia zenu, 244:24 Rum 6:4; Efe 2:10mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.

Kanuni Za Maisha Mapya

254:25 Law 19:11; Rum 12:15Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja. 264:26 Za 4:4; Yak 1:19, 20; Mt 5:22Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika, 274:27 Yak 4:7; 1Pet 5:9wala msimpe ibilisi nafasi. 284:28 Mdo 20:35; 1The 4:11; Lk 3:11Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.

294:29 Kol 3:8; Mt 12:36; Efe 5:4; Kol 3:8; 4:6; 1The 5:11Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao. 304:30 1The 5:19; Rum 8:23Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi. 314:31 Kol 3:8; Tit 3:2; Yak 4:11; 1Pet 2:1; Tit 3:3Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu. 324:32 Mt 6:14, 15Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Nueva Versión Internacional

Efesios 4:1-32

Unidad en el cuerpo de Cristo

1Por eso yo, que estoy preso por la causa del Señor, les ruego que vivan de una manera digna del llamamiento que han recibido, 2siempre humildes y amables, pacientes, tolerantes unos con otros en amor. 3Esfuércense por mantener la unidad del Espíritu mediante el vínculo de la paz. 4Hay un solo cuerpo y un solo Espíritu, así como también fueron llamados a una sola esperanza; 5un solo Señor, una sola fe, un solo bautismo; 6un solo Dios y Padre de todos, que está sobre todos y por medio de todos y en todos.

7Pero a cada uno de nosotros se nos ha dado gracia en la medida en que Cristo ha repartido los dones. 8Por esto dice:

«Cuando ascendió a lo alto,

se llevó consigo a los cautivos

y dio dones a los hombres».4:8 Sal 68:18.

9¿Qué quiere decir eso de que «ascendió», sino que también descendió a las regiones bajas de la tierra? 10El que descendió es el mismo que ascendió por encima de todos los cielos, para llenarlo todo. 11Él mismo constituyó a unos como apóstoles; a otros, profetas; a otros, evangelistas; y a otros, pastores y maestros, 12a fin de capacitar al pueblo de Dios para la obra de servicio, para edificar el cuerpo de Cristo. 13De este modo, todos llegaremos a la unidad de la fe y del conocimiento del Hijo de Dios, a una humanidad perfecta que se conforme a la plena estatura de Cristo.

14Así ya no seremos niños, zarandeados por las olas y llevados de aquí para allá por todo viento de enseñanza y por la astucia y las artimañas de quienes emplean métodos engañosos. 15Más bien, al vivir la verdad con amor, creceremos hasta ser en todo como aquel que es la cabeza, es decir, Cristo. 16Por su acción todo el cuerpo crece y se edifica en amor, sostenido y ajustado por todos los ligamentos, según la actividad propia de cada miembro.

Vivan como hijos de luz

17Así que les digo esto e insisto en el Señor: no vivan más con pensamientos frívolos como los paganos. 18A causa de la ignorancia que los domina y por la dureza de sus corazones, estos tienen oscurecido el entendimiento y están alejados de la vida que proviene de Dios. 19Han perdido toda vergüenza, se han entregado a la inmoralidad y no se sacian de cometer toda clase de actos indecentes.

20No fue esta la enseñanza que ustedes recibieron acerca de Cristo, 21si de veras se les habló y enseñó de Jesús según la verdad que está en él. 22Con respecto a la vida que antes llevaban, se les enseñó que debían quitarse el ropaje de la vieja naturaleza, la cual está corrompida por los deseos engañosos; 23ser renovados en la actitud de su mente; 24y ponerse el ropaje de la nueva naturaleza, creada a imagen de Dios, en verdadera justicia y santidad.

25Por lo tanto, dejando la mentira, hable cada uno a su prójimo con la verdad, porque todos somos miembros de un mismo cuerpo. 26«Si se enojan, no pequen».4:26 Sal 4:4. No permitan que el enojo les dure hasta la puesta del sol 27ni den cabida al diablo. 28El que robaba, que no robe más, sino que trabaje honradamente con las manos para tener qué compartir con los necesitados.

29Eviten toda conversación obscena. Por el contrario, que sus palabras contribuyan a la necesaria edificación y sean de bendición para quienes escuchan. 30No agravien al Espíritu Santo de Dios con el que fueron sellados para el día de la redención. 31Abandonen toda amargura, ira y enojo, gritos y calumnias y toda forma de malicia. 32Más bien, sean bondadosos y compasivos unos con otros y perdónense mutuamente, así como Dios los perdonó a ustedes en Cristo.