Waefeso 2 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Waefeso 2:1-22

Tumefanywa Kuwa Hai Ndani Ya Kristo

12:1 Kol 2:13; Yn 5:24; Kol 2:13; Efe 2:5; 4:18Kwa habari zenu, mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu, 22:2 Tit 3:3; Yn 12:31; Efe 5:6ambazo mlizitenda mlipofuatisha namna ya ulimwengu huu na za yule mtawala wa ufalme wa anga, yule roho atendaye kazi sasa ndani ya wale wasiotii. 32:3 Gal 5:16-24; Kol 3:6; Tit 3:3; 1Pet 4:3; Gal 5:16; Za 51:5; Rum 5:12, 14Sisi sote pia tuliishi katikati yao hapo zamani, tukitimiza tamaa za asili yetu ya dhambi na kufuata tamaa zake na mawazo yake. Nasi kwa asili tulikuwa wana wa ghadhabu, kama mtu mwingine yeyote. 42:4 Yn 3:16; Rum 10:12; Efe 1:7; 2:7Lakini Mungu kwa upendo wake mwingi kwetu sisi, ambaye ni mwingi wa rehema, 52:5 Efe 2:1; 2:8; Za 103:12; Yn 5:24; Mdo 15:11hata tulipokuwa wafu kwa ajili ya makosa yetu, alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo Yesu, yaani, mmeokolewa kwa neema. 62:6 Efe 1:3, 20; Rum 8:10; Flp 3:20Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu, 72:7 Tit 3:4; Efe 1:7; Rum 2:4ili katika ule ulimwengu ujao apate kuonyesha wingi wa neema yake isiyopimika, iliyodhihirishwa kwetu kwa wema wake ndani ya Kristo Yesu. 82:8 Rum 4:2; 2Tim 1:9; Tit 3:5Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala si kwa matendo yenu mema. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu, 92:9 Kum 9:5; 1Kor 1:29si kwa matendo, ili mtu yeyote asije akajisifu. 102:10 Efe 4:24; Tit 2:14; Isa 29:23; 43:7; 60:21; Tit 2:14Kwa maana sisi ni kazi ya mikono ya Mungu, tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tupate kutenda matendo mema, ambayo Mungu alitangulia kuyaandaa tupate kuishi katika hayo.

Wamoja Katika Kristo

112:11 Kol 2:11; Efe 5:8; 2:2Kwa hiyo kumbukeni kwamba ninyi ambao hapo awali mlikuwa watu wa Mataifa kwa kuzaliwa na kuitwa “wasiotahiriwa” na wale wanaojiita “waliotahiriwa” (yaani tohara ifanyikayo katika mwili kwa mikono ya wanadamu), 122:12 Gal 3:17; 1The 4:13kumbukeni kwamba wakati ule mlikuwa mbali na Kristo, mkiwa mmetengwa kutoka jumuiya ya Israeli, na mkiwa wageni katika yale maagano ya ahadi, nanyi mkiwa hamna tumaini wala Mungu duniani. 132:13 Mdo 2:39; Kol 1:20Lakini sasa katika Kristo Yesu, ninyi ambao hapo kwanza mlikuwa mbali na Mungu, sasa mmeletwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.

142:14 1Kor 12:13; Isa 9:5; Gal 3:28; Kol 2:14Kwa maana yeye mwenyewe ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi tuliokuwa wawili, yaani, Wayahudi na watu wa Mataifa, tuwe wamoja kwa kuvunja kizuizi na kubomoa ule ukuta wa uadui uliokuwa kati yetu, 152:15 Kol 1:21-22; 2:14; Gal 3:28kwa kuibatilisha ile sheria pamoja na amri zake na maagizo yake alipoutoa mwili wake, ili apate kufanya ndani yake mtu mmoja mpya badala ya hao wawili, hivyo akifanya amani, 162:16 Kol 1:20, 22; Rum 6:6; 8:3; Kol 2:14naye katika mwili huu mmoja awapatanishe wote wawili na Mungu kupitia msalaba, ili kwa huo msalaba akaangamiza uadui wao. 172:17 Za 148:14; Isa 57:19Alikuja na kuhubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali na pia akahubiri amani kwao waliokuwa karibu. 182:18 Efe 3:12; Kol 1:12; 1Kor 12:13Kwa maana kwa kupitia kwake, sisi sote tunaweza kumkaribia Baba katika Roho mmoja.

192:19 Flp 3:20; Gal 6:10Hivyo basi, ninyi sasa si wageni tena wala wapitaji, bali mmekuwa wenyeji pamoja na watakatifu na pia jamaa wa nyumbani mwake Mungu. 202:20 Mt 16:18; 1Kor 3:10; 1Pet 2:4-8Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ndiye jiwe kuu la pembeni. 212:21 1Kor 3:16-17Ndani yake jengo lote limeshikamanishwa pamoja na kusimamishwa ili kuwa Hekalu takatifu katika Bwana. 22Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja ili mpate kuwa makao ambayo Mungu anaishi ndani yake kwa njia ya Roho wake.