Waamuzi 9 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 9:1-57

Abimeleki Ajaribu Kuanzisha Ufalme

19:1 Amu 8:31; 6:32Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake, 29:2 Mwa 29:14“Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”

3Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.” 49:4 Amu 8:33; 11:3; 1Sam 25:25; 2Nya 13:7; Ay 30:8Wakampa shekeli sabini9:4 Shekeli 70 za fedha ni sawa na gramu 800. za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake. 59:5 Amu 8:30; 2Fal 11:2; 2Nya 22:9Akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra, na juu ya jiwe moja wakawaua ndugu zake sabini, ambao ni wana wa Yerub-Baali. Lakini Yothamu, mwana mdogo wa wote wa Yerub-Baali, akaokoka kwa kujificha. 69:6 2Fal 12:20; Mwa 12:6; Amu 4:11Ndipo watu wote wa Shekemu na Beth-Milo wakakusanyika pamoja chini ya mti mkubwa wa mwaloni penye nguzo iliyoko Shekemu wakamvika Abimeleki taji kuwa mfalme.

79:7 Kum 27:12; Yn 4:20Yothamu alipoambiwa hayo, akapanda juu ya kilele cha mlima Gerizimu, akawapazia sauti yake akawaambia, “Nisikilizeni enyi watu wa Shekemu, ili Mungu naye apate kuwasikiliza ninyi. 8Siku moja miti ilitoka ili kwenda kujitawazia mfalme. Ikauambia mzeituni, ‘Wewe uwe mfalme wetu.’

9“Lakini mzeituni ukaijibu, ‘Je, niache kutoa mafuta yangu ambayo kwake miungu na wanadamu huheshimiwa, ili nikawe juu ya miti?’

10“Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo na uwe mfalme wetu!’

11“Lakini mtini ukaijibu, ‘Je, niache kutoa matunda yangu mazuri na matamu, ili niende nikawe juu ya miti?’

12“Ndipo miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’

139:13 Mwa 14:18; Mhu 2:3; Wim 4:10“Lakini mzabibu ukaijibu, ‘Je, niache kutoa divai yangu inayofurahisha miungu na wanadamu ili nikawe juu ya miti?’

14“Mwishoni miti yote ikauambia mti wa miiba, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’

159:15 Isa 30:2; Kum 3:25; 1Fal 5:6; Za 29:5; 92:12; Isa 2:13“Nao mti wa miiba ukaijibu, ‘Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu, basi njooni mpate kupumzika chini ya kivuli changu. Lakini kama sivyo, moto na utoke kwenye mti wa miiba ukateketeze mierezi ya Lebanoni!’

16“Basi ikiwa mmetenda kwa uaminifu na heshima kumfanya Abimeleki kuwa mfalme, na kama mmetendea vyema Yerub-Baali na jamaa yake kama ilivyostahili: 179:17 Amu 12:3; 1Sam 19:5; 28:21; Ay 13:14; Za 119:109kwa kuwa baba yangu aliwapigania ninyi na kuhatarisha nafsi yake na kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwa Wamidiani 189:18 Amu 8:30(lakini leo mmeasi dhidi ya jamaa ya baba yangu, na kuwaua wanawe sabini juu ya jiwe moja, nanyi mkamfanya Abimeleki mwana wa mwanamke mtumwa kuwa mfalme juu ya Shekemu, kwa kuwa yeye ni ndugu yenu), 19nanyi kama basi mmemtendea Yerub-Baali na jamaa yake kwa heshima na uaminifu, basi Abimeleki na awe furaha yenu, nanyi mwe furaha yake pia! 20Lakini kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na uwateketeze, ninyi watu wa Shekemu na Beth-Milo, nao moto utoke kwenu, watu wa Shekemu na Beth-Milo umteketeze Abimeleki!”

219:21 Hes 21:16Ndipo Yothamu akakimbia, akatoroka akaenda Beeri, akaishi huko, kwa sababu alimwogopa ndugu yake Abimeleki.

22Baada ya Abimeleki kutawala Israeli kwa muda wa miaka mitatu, 239:23 1Sam 16:14; 18:10; 19:9; 1Fal 22:22Mungu akaruhusu roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu, nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa hila. 249:24 Amu 8:30; Mwa 9; 6; Hes 35:33; 1Fal 2:32; Kum 27:25Hili lilitokea ili ule ukatili waliotendewa hao wana sabini wa Yerub-Baali upatilizwe, na damu yao iwe juu ya Abimeleki ndugu yao aliyewaua, na pia iwe juu ya watu wa Shekemu, ambao walimsaidia kuua ndugu zake. 25Hivyo, kutokana na uadui juu yake watu wa Shekemu wakaweka watu wa kumvizia katika vilele vya milima. Wakawanyangʼanya watu wote waliopita karibu nao, nayo haya yakaarifiwa kwa Abimeleki.

26Basi Gaali mwana wa Ebedi akaenda pamoja na ndugu zake wakaingia Shekemu, nao watu wa huko wakamtumainia yeye. 279:27 Isa 16:10; Amo 5:11; 9:13; Amu 8:33Wakaenda mashambani mwao kuvuna zabibu na kuzisindika hizo zabibu, wakafanya sikukuu katika hekalu la mungu wao. Wakati wakila na kunywa, wakamlaani Abimeleki. 289:28 1Sam 25:10; 1Fal 12:16; Mwa 33:19; 34:2-6Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerub-Baali? Naye Zebuli si ndiye msaidizi wake? Basi watumikieni watu wa Hamori, babaye Shekemu. Kwa nini tumtumikie Abimeleki? 299:29 2Sam 15; 4Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu! Basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Ningemwambia Abimeleki, ‘Ondoa jeshi lako lote.’ ”

30Zebuli aliyekuwa mtawala wa mji aliposikia aliyosema Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana. 31Akatuma ujumbe uende kwa Abimeleki kwa siri na kusema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wamekuja Shekemu, na wanauchochea mji huu kinyume chako. 329:32 Yos 8:2Sasa, basi, usiku huu wewe uondoke na watu wako ili mje kuwavizia mashambani. 339:33 1Sam 10:7Kisha asubuhi wakati wa kuchomoza jua, amka mapema na ujipange dhidi ya huo mji. Wakati yeye na jeshi lililo pamoja naye watakapotoka kukabiliana nanyi, mwaweza kuwatendea kwa kadiri mnavyoweza.”

34Kwa hiyo Abimeleki pamoja na jeshi lake lote wakaondoka usiku na kujificha karibu na Shekemu wakiwa vikosi vinne. 359:35 Yos 2:5; Za 32:7; Isa 28:15-17; Yer 49:10Basi Gaali mwana wa Ebedi alikuwa ametoka nje akawa amesimama katika ingilio la mji wakati ule ule ambao Abimeleki na watu wake walipokuwa wanatoka sehemu zao za maficho.

36Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama, watu wanashuka kutoka kwenye vilele vya milima!”

Zebuli akajibu, “Wewe unaona vivuli vya milima kana kwamba ni watu.”

37Lakini Gaali akasema tena, “Tazama, watu wanashuka kutoka katikati ya nchi na kikosi kimoja kinakuja kutoka Tabur-Ezeri na kikosi kingine kutoka upande wa Elon-Meonenimu.”

38Ndipo Zebuli akamwambia, “Kuko wapi kujivuna kwako sasa, wewe uliyesema, ‘Huyo Abimeleki ni nani hata tumtumikie?’ Hawa si wale watu uliowadharau? Toka nje sasa ukapigane nao!”

39Basi Gaali akatoka akawaongoza watu wa Shekemu kupigana na Abimeleki. 40Abimeleki akamfukuza, watu wengi wakajeruhiwa katika kukimbia huko, njia nzima hadi kwenye ingilio la lango. 41Abimeleki akakaa Aruma, naye Zebuli akawafukuza Gaali na ndugu zake watoke Shekemu.

42Kesho yake watu wa Shekemu wakatoka wakaenda mashambani, Abimeleki akaambiwa juu ya jambo hili. 439:43 Amu 7:16; Yos 8:2Hivyo akawachukua watu wake, akawagawanya katika vikosi vitatu na kuwaweka waviziao huko mashambani. Alipowaona watu wanatoka kwenda nje ya mji, akainuka dhidi yao na kuwashambulia. 44Abimeleki pamoja na vile vikosi wakaharakisha kwenda mbele kwenye nafasi, mahali pa ingilio la lango la mji. Vile vikosi viwili vikawawahi wale waliokuwa mashambani na kuwaua. 459:45 Yer 48:9Siku hiyo nzima Abimeleki akazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji hadi akawa ameuteka na kuwaua watu wa huo mji. Kisha akauangamiza mji na kusambaza chumvi juu yake.

469:46 Amu 8:33Kwa kusikia jambo hili watu wote katika mnara wa Shekemu, wakaingia kwenye ngome ya hekalu la El-Berithi. 47Abimeleki aliposikia kuwa wamekusanyika huko, 489:48 Za 68:14yeye na watu wake wote wakakwea kwenye Mlima Salmoni. Abimeleki akachukua shoka, akakata baadhi ya matawi, ambayo aliyachukua mabegani. Akawaagiza wale watu waliokuwa pamoja naye kuwa, “Fanyeni kile mlichoona mimi nikifanya!” 49Basi watu wote wakakata matawi na kumfuata Abimeleki. Wakayakusanya hayo matawi juu ya ngome na kuitia moto ili kuwachoma wale watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo watu wote katika mnara wa Shekemu, karibia watu 1,000 waume kwa wake, pia wakafa.

509:50 2Sam 11:21Baadaye Abimeleki akaenda Thebesi na kuuzingira kwa jeshi na kuuteka. 51Hata hivyo, ndani ya huo mji kulikuwa na mnara imara, ambako watu wote wa mji wanaume na wanawake, watu wote wa mji, walikimbilia ndani yake. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa la mnara. 52Abimeleki akaja kwenye ule mnara na kuushambulia, lakini alipokaribia kwenye ingilio la mnara ili kuuchoma kwa moto, 539:53 2Sam 11:21mwanamke mmoja akaangusha sehemu ya juu ya jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, likapasua fuvu la kichwa chake.

549:54 1Sam 31:4; 2Sam 1:9Akamwita kwa haraka kijana yule aliyechukua silaha zake, na kumwambia, “Chukua upanga wako na uniue, watu wasije wakasema kwamba, ‘Mwanamke amemuua.’ ” Basi yule kijana akamchoma upanga, naye akafa. 55Waisraeli walipoona kuwa Abimeleki amekufa, kila mtu akaenda nyumbani kwake.

56Hivyo ndivyo Mungu alivyolipiza uovu ule ambao Abimeleki alikuwa ameutenda kwa baba yake kwa kuwaua ndugu zake sabini. 579:57 Za 94:23Mungu akawapatiliza watu wa Shekemu uovu wao juu ya vichwa vyao, na juu yao ikaja laana ya Yothamu mwana wa Yerub-Baali.

Священное Писание

Судьи 9:1-57

Ави-Малик

1Ави-Малик, сын Иеруб-Баала, пришёл к братьям своей матери в Шехем и сказал им и всему клану своей матери:

2– Спросите всех жителей Шехема: «Что для вас лучше, чтобы вами правили все семьдесят сыновей Иеруб-Баала или всего лишь один?» Помните, что я ваша плоть и кровь.

3Когда братья его матери пересказали всё это жителям Шехема, те склонились на сторону Ави-Малика, потому что говорили: «Он наш брат». 4Они дали ему восемьсот сорок граммов9:4 Букв.: «семьдесят шекелей». серебра из храма Баал-Берита, и Ави-Малик нанял на них праздных и безрассудных людей, которые пошли за ним. 5Он пришёл в дом своего отца в Офре и убил семьдесят своих братьев, сыновей Иеруб-Баала, на одном камне. Но Иотам, самый младший сын Иеруб-Баала, спрятался и спасся. 6А все жители Шехема и Бет-Милло собрались у великого дерева в Шехеме и сделали Ави-Малика царём.

7Когда об этом рассказали Иотаму, он поднялся на вершину горы Геризим и закричал им:

– Послушайте меня, жители Шехема, чтобы и Всевышний послушал вас! 8Решили однажды деревья поставить над собою царя. Они сказали оливе: «Царствуй над нами». 9Но олива ответила: «Бросить ли мне своё масло – им славят богов и людей, – чтобы править деревьями?» 10Деревья сказали инжиру: «Ты приди, царствуй над нами». 11Но инжир им ответил: «Бросить ли мне свой плод – такой хороший и вкусный, – чтобы править деревьями?» 12Деревья сказали виноградной лозе: «Ты приди, царствуй над нами». 13Но лоза им ответила: «Бросить ли мне своё вино – оно веселит богов и людей, – чтобы править деревьями?» 14Тогда деревья сказали терновнику: «Ты приди, царствуй над нами». 15И терновник ответил деревьям: «Если вы и вправду хотите поставить меня над собою царём, то приходите, покойтесь в моей тени. Но если нет, то пусть выйдет из терновника пламя и пожрёт ливанские кедры».

16Итак, честно ли и достойно ли вы поступили, сделав Ави-Малика царём? По совести ли вы поступили с Иеруб-Баалом и его семьёй, так ли обошлись с ним, как он того заслуживает? 17Мой отец сражался за вас, рисковал жизнью, чтобы избавить вас от руки мадианитян, 18но сегодня вы восстали против семьи моего отца, убили семьдесят его сыновей на одном камне и сделали Ави-Малика, сына его рабыни, царём над жителями Шехема, потому что он ваш брат. 19Если сегодня вы поступили с Иеруб-Баалом и его семьёй честно и достойно, то радуйтесь за Ави-Малика, и пусть он радуется за вас! 20Но если нет, то пусть из Ави-Малика выйдет пламя и пожрёт вас, жители Шехема и Бет-Милло, и пусть из вас, жители Шехема и Бет-Милло, выйдет пламя и пожрёт Ави-Малика!

21И Иотам бежал и поселился в городе Беэре, потому что боялся своего брата Ави-Малика.

22Ави-Малик правил Исраилом три года. 23Но Всевышний наслал злого духа между Ави-Маликом и жителями Шехема, и жители Шехема не стали покоряться Ави-Малику. 24Это случилось, чтобы жестокость по отношению к семидесяти сыновьям Иеруб-Баала была наказана, и кровь их легла на их брата Ави-Малика и на жителей Шехема, которые помогли ему убить своих братьев. 25Жители Шехема из вражды к нему устраивали засады на горных вершинах, чтобы грабить каждого, кто проходит мимо, и об этом было донесено Ави-Малику.

26А в Шехем пришёл Гаал, сын Эведа, вместе со своими братьями, и жители Шехема доверились ему. 27Они вышли в поле, собирали виноград, давили его и праздновали. Они пошли в храм своего бога, ели и пили и проклинали Ави-Малика.

28Гаал, сын Эведа, сказал:

– Кто такой Ави-Малик и кто такие мы в Шехеме, чтобы подчиняться ему? Разве он не сын Иеруб-Баала и разве не Зевул его наместник? Служите людям Еммора, отца Шехема! Зачем нам служить Ави-Малику? 29Если бы только эти люди были у меня под началом! Тогда я избавился бы от Ави-Малика. Я бы сказал ему: «Собери своё войско и выходи!»

30Когда Зевул, правитель города, услышал слова Гаала, сына Эведа, он очень разгневался. 31Он тайно послал вестников к Ави-Малику, чтобы сказать ему:

– Гаал, сын Эведа, и его братья пришли в Шехем и настраивают город против тебя. 32Итак, приходи ночью со своими воинами и устрой в поле засаду. 33А утром, на рассвете, напади на город. Когда Гаал и его воины выйдут против тебя, делай с ними всё, что хочешь.

34И Ави-Малик вместе со всеми своими воинами отправился в путь, и они залегли в засаду у Шехема четырьмя отрядами. 35А Гаал, сын Эведа, вышел и стоял у входа в городские ворота как раз тогда, когда Ави-Малик и его воины выходили из засады.

36Увидев их, Гаал сказал Зевулу:

– Смотри, с горных вершин спускаются люди!

Зевул ответил:

– Тени от гор кажутся тебе людьми.

37Но Гаал вновь сказал:

– Смотри, с горы9:37 Букв.: «Табур-Эрец», что переводится как «пуп земли». Возможно, это была гора Геризим. спускаются люди, и один отряд идёт со стороны дуба прорицателей9:37 Или: «из Елон-Меоненина»..

38Зевул сказал ему:

– Где твоя похвальба, ты, говоривший: «Кто такой Ави-Малик, чтобы нам ему подчиняться?» Разве не этих людей ты высмеивал? Выходи же теперь и сразись с ними!

39И Гаал пошёл во главе жителей Шехема и сразился с Ави-Маликом. 40Ави-Малик погнался за ним, и Гаал побежал от него. Многие пали ранеными у самого входа в ворота. 41И Ави-Малик расположился в Аруме, а Зевул выгнал Гаала и его братьев из Шехема.

42На следующий день жители Шехема вышли в поле, и об этом донесли Ави-Малику. 43Он взял своих воинов, разделил их на три отряда и устроил в поле засаду. Увидев людей, которые выходили из города, он поднялся и напал на них. 44Ави-Малик и отряд, который был с ним, поспешили занять место у входа в городские ворота, а два отряда ринулись на тех, кто был в поле, и стали убивать их. 45Весь день Ави-Малик воевал с городом, пока не взял его и не перебил его жителей. После этого он сровнял город с землёй и засыпал это место солью.

46Услышав об этом, все жители, бывшие в Шехемской башне, вошли в убежище храма Баал-Берита9:46 Букв.: «Ил-Берит» – другое название Баал-Берита (см. ст. 4).. 47Когда Ави-Малику донесли, что они собрались там, 48он вместе со всеми своими воинами поднялся на гору Цалмон. Он взял топор, срубил несколько веток и положил их на плечи. Затем он приказал воинам, которые были с ним:

– Быстро делайте то же, что и я.

49И все его воины нарубили веток и пошли за Ави-Маликом. Они сложили их у убежища и подожгли его вместе с теми, кто в нём был. И все, кто был в Шехемской башне, около тысячи мужчин и женщин погибли.

50Затем Ави-Малик пошёл к Тевецу, осадил его и захватил. 51Но в городе была крепкая башня, и туда бежали все мужчины и женщины – все жители города. Они заперлись изнутри и поднялись на крышу башни. 52Ави-Малик пришёл к башне и напал на неё, но когда он приблизился к входу, чтобы поджечь её, 53одна женщина сбросила ему на голову обломок жёрнова и проломила ему череп.

54Он тотчас же подозвал своего оруженосца и сказал ему:

– Вытащи меч и убей меня, чтобы не говорили обо мне: «Его убила женщина».

Слуга пронзил его, и он умер. 55Увидев, что Ави-Малик умер, исраильтяне разошлись по домам.

56Так Всевышний воздал за зло, которое Ави-Малик сделал своему отцу, убив семьдесят своих братьев. 57Ещё Всевышний воздал за всё их зло жителям Шехема. Их постигло проклятие Иотама, сына Иеруб-Баала.