Waamuzi 19 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 19:1-30

Mlawi Na Suria Wake

119:1 Amu 18:1; Rut 1:1Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme.

Basi Mlawi mmoja aliyeishi sehemu za mbali katika nchi ya vilima ya Efraimu, akamchukua suria mmoja kutoka Bethlehemu ya Yuda. 2Lakini suria wake akafanya ukahaba dhidi yake, naye akamwacha akarudi nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Baada ya kukaa huko kwa muda wa miezi minne, 3mume wake akaenda kumsihi ili arudi. Alikwenda na mtumishi wake na punda wawili. Yule mwanamke akamkaribisha nyumbani mwa baba yake, baba yake alipomwona akamkaribisha kwa furaha. 419:4 Kut 32:6Baba mkwe wake, yaani, baba yake yule msichana, akamzuia ili akae, hivyo akakaa na huyo baba mkwe wake kwa siku tatu, wakila, wakinywa na kulala huko.

519:5 Mwa 15:8Siku ya nne wakaamka mapema naye akajiandaa kuondoka, lakini baba wa yule msichana akamwambia mkwewe, “Ujiburudishe kwa kula kitu chochote, ndipo uweze kwenda.” 619:6 Amu 16:25Basi wakaketi wote wawili ili kula na kunywa pamoja. Baadaye baba wa msichana akamwambia, “Tafadhali ubakie usiku huu upate kujifurahisha nafsi yako.” 7Basi yule mtu alipotaka kuondoka baba wa yule msichana akamsihi, basi akabaki usiku ule. 8Asubuhi ya siku ya tano, alipoamka ili aondoke, baba wa yule msichana akamwambia, “Jiburudishe nafsi yako. Ngoja mpaka mchana!” Kwa hiyo wote wawili wakala chakula pamoja.

9Basi wakati yule mtu alipoinuka aende zake, pamoja na suria wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani, baba wa yule msichana akamwambia, “Tazama sasa jioni inakaribia. Ulale hapa usiku unakaribia. Ukae, ukajifurahishe nafsi yako. Kesho unaweza kuamka mapema asubuhi na uende nyumbani kwako.” 1019:10 Mwa 10:16; Yos 15:8; 1Nya 11:4-5Lakini akakataa kulala tena, akaondoka na kwenda mpaka Yebusi (ndio Yerusalemu), akiwa na punda wake wawili waliotandikiwa, pamoja na suria wake.

1119:11 Mwa 10:16; Yos 3:10Alipokaribia Yebusi na usiku ukiwa umekaribia, mtumishi akamwambia bwana wake, “Haya sasa natuingie katika mji huu wa Wayebusi tulale humo.”

12Lakini bwana wake akamjibu, “Hapana. Hatutaingia kwenye mji wa kigeni, ambao watu wake si Waisraeli. Tutaendelea mpaka tufike Gibea.” 1319:13 Yos 18:25Akasema, “Haya, tujitahidi tufike Gibea au Rama, nasi tutalala katika mji mmojawapo.” 1419:14 Yos 15:57; 1Sam 10:26; 11:4; 13:2; 15:34; Isa 10:29Hivyo wakaendelea na safari, jua likachwea walipokaribia Gibea ambao ni mji wa Benyamini. 1519:15 Mwa 24:23; 19:2Wakageuka ili kuingia na kulala Gibea. Wakaingia humo, wakaketi kwenye uwanja wa mji, wala hakuna mtu yeyote aliyewakaribisha kwake ili wapate kulala.

1619:16 Za 104:23Jioni ile mtu mmoja mzee toka nchi ya vilima ya Efraimu, aliyekuwa anaishi huko Gibea (watu wa sehemu ile walikuwa Wabenyamini), akarudi kutoka kwenye kazi za shamba. 1719:17 Mwa 29:4Alipotazama na kuwaona hao wasafiri katika uwanja wa mji, yule mzee akawauliza, “Ninyi mnakwenda wapi? Nanyi mmetoka wapi?”

1819:18 Amu 18:31Akamwambia, “Tumepita kutoka Bethlehemu ya Yuda, tunaelekea katika nchi ya vilima ya Efraimu, ambako ndiko ninakoishi. Nilikwenda Bethlehemu ya Yuda na sasa ninakwenda katika nyumba ya Bwana. Hakuna mtu yeyote aliyenikaribisha katika nyumba yake. 1919:19 Mwa 24:25; 42:27; 14:18Tunazo nyasi na chakula cha punda wetu na mkate na divai kwa ajili yetu sisi watumishi wako, yaani mimi, mtumishi wako mwanamke, pamoja na huyu kijana tuliyefuatana naye. Hatuhitaji kitu chochote.”

20Yule mzee akawaambia, “Amani iwe kwenu! Karibuni nyumbani mwangu. Nitawapa mahitaji yenu yote, msilale katika uwanja huu wa mji.” 2119:21 Mwa 24:32-33; Lk 7:44Hivyo akamwingiza nyumbani mwake na kuwalisha punda wake. Baada ya kunawa miguu yao, wakala na kunywa.

2219:22 Amu 16:25; Kum 13:13; Mwa 19:4-5; Amu 20:5; Rum 1:26-27Walipokuwa wakijiburudisha, watu waovu wa mji huo, wakaizingira ile nyumba. Wakagonga mlango na kusema na yule mzee mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mtu aliyeingia kwako, tupate kumlawiti.”

2319:23 Mwa 19:6; 34:7; Law 19:29; Yos 7:15; Amu 20:6; Rum 1:27Yule mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Hapana, ndugu zangu msiwe waovu namna hii, ninawasihi. Kwa kuwa huyu mtu ni mgeni wangu msifanye jambo hili la aibu. 2419:24 Mwa 19:8; Kum 21:14Tazameni, hapa yupo binti yangu ambaye ni bikira na suria wa huyu mtu. Nitawatoleeni hawa sasa, mkawatwae kwa nguvu na kuwafanyia lolote mtakalo. Lakini kwa mtu huyu msimfanyie jambo ovu hivyo.”

2519:25 Mwa 20:5; 1Sam 31:4Lakini wale watu hawakumsikia. Hivyo yule mtu akamtoa yule suria wake nje kwa wale watu, nao wakambaka na kumnajisi usiku ule kucha mpaka asubuhi. Kulipoanza kupambazuka wakamwachia aende. 26Alfajiri yule mwanamke akarudi kwenye ile nyumba bwana wake alikokuwa, akaanguka chini mlangoni, akalala pale hata kulipopambazuka.

27Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua mlango wa nyumba na kutoka nje ili kuendelea na safari yake, tazama, yule suria wake alikuwa ameanguka pale penye ingilio la nyumba na mikono yake ikiwa penye kizingiti cha chini. 28Akamwambia yule suria, “Inuka, twende.” Lakini hakujibu. Yule bwana akamwinua akampandisha juu ya punda wake, wakaondoka kwenda nyumbani.

2919:29 Mwa 22:6; Amu 20:6; 1Sam 11:7Alipofika nyumbani, akachukua kisu na kumkatakata yule suria kiungo kwa kiungo, sehemu kumi na mbili, na kuvipeleka hivyo vipande katika sehemu zote za Israeli. 3019:30 Hes 9:9; Amu 20:7; Mit 13:10Kila mtu aliyeona akasema, “Jambo la namna hii halijaonekana wala kutendeka, tangu Israeli walipopanda kutoka Misri. Fikirini juu ya jambo hili! Tafakarini juu ya jambo hili! Tuambieni tufanye nini!”

New Russian Translation

Судей 19:1-30

Левит и его наложница

1В те дни у Израиля не было царя.

Однажды левит, который жил в нагорьях Ефрема, взял себе наложницу из Вифлеема в Иудее. 2Но она поссорилась с ним19:2 Или: «стала ему изменять». и ушла в дом своего отца в Вифлееме. Она пробыла там четыре месяца, 3и муж отправился к ней, чтобы убедить ее вернуться. С ним был слуга и два осла. Она ввела его в дом своего отца, и тот, увидев его, принял с радостью. 4Тесть, отец молодой женщины, убедил его остаться, и он остался у него на три дня, ел, пил и спал там.

5На четвертый день они встали ранним утром, и он собрался уходить, но отец молодой женщины сказал зятю:

– Сначала подкрепись, а потом пойдете.

6И они вместе сели за еду и питье. После этого отец молодой женщины сказал:

– Прошу тебя, останься еще на ночь и приятно проведи время.

7И хотя тот человек встал, чтобы идти, тесть убедил его, и он остался там еще на ночь. 8Утром пятого дня, когда он собрался уходить, отец молодой женщины сказал:

– Подкрепись. Подождите до полудня!

И они вместе ели. 9А когда этот человек вместе со своей наложницей и слугой встал, чтобы уйти, отец молодой женщины сказал ему:

– Смотри, уже почти вечер. Переночуйте здесь, ведь день уже на исходе. Останься и приятно проведи время. А завтра рано утром соберетесь в дорогу, и ты пойдешь домой.

10Но не желая оставаться еще на ночь, этот человек ушел и направился к Иевусу (то есть Иерусалиму) с двумя навьюченными ослами и наложницей.

11Когда они были рядом с Иевусом и день уже почти прошел, слуга сказал своему господину:

– Свернем-ка в этот город иевусеев и заночуем там.

12Его господин ответил:

– Нет. Мы не свернем в город чужаков, которые не принадлежат к народу Израиля. Мы пойдем дальше к городу Гиве.

13И добавил:

– Идем, постараемся добраться до Гивы или Рамы и заночевать в одном из этих мест.

14Они пошли дальше, и когда подошли к Гиве, что в земле Вениамина, солнце уже село. 15Они завернули туда на ночлег, вошли в город и сели на городской площади, но никто не позвал их в дом переночевать.

16В тот вечер один старик, который был родом из нагорий Ефрема, но жил в Гиве (а жители этого места были вениамитянами), возвращался с поля после работы. 17Увидев странника на городской площади, старик спросил:

– Куда ты идешь и откуда?

18Он ответил:

– Мы идем из Вифлеема, что в Иудее, в далекие места нагорий Ефрема, где я живу. Я ходил в Вифлеем, что в Иудее, и теперь возвращаюсь в дом Господа19:18 В одном из древних переводов: «к себе домой» (ср. 19:29).. Но никто не позвал меня в свой дом. 19А у нас есть и солома, и корм для наших ослов, и хлеб с вином для нас самих, твоих слуг, – для меня, твоей служанки и юноши, который с нами. Больше нам ничего не нужно.

20– Пойдемте ко мне домой, – сказал старик. – Я сам позабочусь о ваших нуждах. Только не ночуй на площади.

21Он привел его к себе домой и накормил его ослов. А сами они, вымыв ноги, стали есть и пить.

22Пока они приятно проводили время, жители города, порочные люди, окружили дом. Колотя в дверь, они кричали старику, хозяину дома:

– Выведи того человека, который к тебе пришел, чтобы нам с ним поразвлечься19:22 Букв.: «чтобы мы их познали»..

23Хозяин дома вышел к ним и сказал:

– Нет, друзья мои, не поступайте так низко. Ведь этот человек – мой гость, не делайте такой подлости. 24Смотрите, вот моя девственница-дочь и его наложница. Сейчас я выведу их к вам. Смирите19:24 Или: «Насилуйте». их и делайте с ними, что хотите. Но с этим человеком не делайте такой подлости.

25Но люди не хотели его слушать. Тогда гость вывел к ним свою наложницу. Они насиловали19:25 Букв.: «познали ее». и бесчестили ее всю ночь, а когда начало светать, отпустили. 26На рассвете женщина вернулась к дому, где был ее господин, упала у двери и лежала там, пока не рассвело.

27Когда утром ее господин встал, открыл дверь и собрался идти дальше, он увидел свою наложницу, лежавшую у двери, держась за порог. 28Он сказал ей:

– Вставай, пойдем.

Но ответа не было19:28 В древнем переводе присутствуют слова: « … потому что она умерла».. Тогда тот человек положил ее на осла и отправился домой.

29Добравшись до дома, он взял нож, разрезал свою наложницу на двенадцать частей и разослал их по всем областям Израиля. 30Всякий, кто видел это, говорил:

– Такого никогда не видели и не делали со дня выхода израильтян из Египта до сегодняшнего дня. Подумайте об этом! Посоветуйтесь и скажите, как тут быть!