Ufunuo 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Ufunuo 7:1-17

Waisraeli 144,000 Watiwa Muhuri

17:1 Yer 49:36; Mt 24:31Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote. 27:2 Ufu 9:4; Mt 16:16Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema, 37:3 Ufu 6:6; Eze 9:4; Ufu 22:4“Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.” 47:4 Ufu 9:16; 14:1-3Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.

5Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri,

kutoka kabila la Reubeni 12,000,

kutoka kabila la Gadi 12,000,

6kutoka kabila la Asheri 12,000,

kutoka kabila la Naftali 12,000,

kutoka kabila la Manase 12,000,

7kutoka kabila la Simeoni 12,000,

kutoka kabila la Lawi 12,000,

kutoka kabila la Isakari 12,000,

8kutoka kabila la Zabuloni 12,000,

kutoka kabila la Yosefu 12,000,

na kutoka kabila la Benyamini 12,000.

Umati Mkubwa Wa Watu Kutoka Mataifa Yote

97:9 Ufu 5:9; 13:7; 7:15; Rum 11:25; Ufu 3:5; 6:11; 7:4Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao. 107:10 Za 3:8; Ufu 19:1Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema:

“Wokovu una Mungu wetu,

yeye aketiye kwenye kiti cha enzi,

na Mwana-Kondoo!”

117:11 Ufu 4:4-10Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu, 127:12 Rum 11:36; Ufu 5:12-14wakisema:

“Amen!

Sifa na utukufu

na hekima na shukrani na heshima

na uweza na nguvu

viwe kwa Mungu wetu milele na milele.

Amen!”

137:13 Ufu 3:4; 7:9Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”

147:14 Ufu 22:14; Ebr 9:14; 1Yn 1:7Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.”

Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa. 157:15 Ufu 22:3; 11:19; Isa 4:5-6Kwa hiyo,

“Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu

na kumtumikia usiku na mchana

katika hekalu lake;

naye aketiye katika kile kiti cha enzi

atatanda hema yake juu yao.

167:16 Isa 49:10Kamwe hawataona njaa

wala kiu tena.

Jua halitawapiga

wala joto lolote liunguzalo.

177:17 Za 23:1; Yn 10:11; Isa 51:11; Ufu 21:3Kwa maana Mwana-Kondoo

aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi

atakuwa Mchungaji wao;

naye atawaongoza kwenda

kwenye chemchemi za maji yaliyo hai.

Naye Mungu atafuta kila chozi

kutoka macho yao.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

啟示錄 7:1-17

為上帝的僕人蓋印

1此後,我看見四位天使分別站在地的四個角落控制著四面的風,使風不再吹向地面、海洋和樹木。 2我又看見一位天使從東方日出之地上來,手裡拿著永活上帝的印。他對那領受權柄能傷害地和海的四位天使大聲說: 3「我們在上帝的奴僕額上蓋印之前,你們不可傷害地、海和樹木。」 4我聽見以色列各支派中蓋了印的共有十四萬四千人: 5猶大支派有一萬二千,呂便支派有一萬二千,迦得支派有一萬二千, 6亞設支派有一萬二千,拿弗他利支派有一萬二千,瑪拿西支派有一萬二千, 7西緬支派有一萬二千,利未支派有一萬二千,以薩迦支派有一萬二千, 8西布倫支派有一萬二千,約瑟支派有一萬二千,便雅憫支派有一萬二千。

劫後餘生的上帝子民

9此後,我觀看,見有一大群人,不可勝數,他們來自各國家、各部落、各民族、各語言族群,身穿白袍,手拿棕樹枝,站在寶座和羔羊面前, 10大聲呼喊說:「救恩來自我們坐在寶座上的上帝,也來自羔羊!」 11眾天使都站在寶座、眾長老和四個活物的周圍,在寶座前俯伏敬拜上帝,說: 12「阿們!願頌讚、榮耀、智慧、感謝、尊貴、權柄、能力都歸給我們的上帝,直到永永遠遠。阿們!」

13其中一位長老問我:「這些身穿白袍的人是誰?他們從哪裡來?」

14我回答說:「先生,你知道答案。」

他便說:「這些都是經過大災難的人,他們用羔羊的血將衣裳洗得潔白。 15因此,他們在上帝的寶座前,在聖殿中不分晝夜地事奉上帝。坐在寶座上的那位要庇護他們。 16他們不會再受饑餓和乾渴的折磨,也不會再受太陽和酷熱的煎熬,7·16 以賽亞書25·8 17因為在寶座中央的羔羊要作他們的牧人,引導他們到生命的泉水邊,上帝要擦乾他們所有的眼淚。」7·17 以賽亞書49·10