Ufunuo 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Ufunuo 2:1-29

Kwa Kanisa Lililoko Efeso

12:1 Ufu 1:16; 1:12-13“Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika:

“Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu. 22:2 1Yn 4:1; 2Kor 11:13Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo. 32:3 Yn 15:21Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.

42:4 Yer 2:2; Mt 24:12“Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza. 52:5 Ufu 1:20Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake. 62:6 Ufu 2:15; Za 139:21Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.

72:7 Mt 11:15; Ufu 13:9; Mwa 2:9; Ufu 22:2, 14; Lk 23:43“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradiso2:7 Paradiso hapa ina maana ya Bustani, yaani shamba dogo la miti izaayo matunda. ya Mungu.

Kwa Kanisa Lililoko Smirna

82:8 Ufu 1:11-13“Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika:

“Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka. 92:9 Yak 2:5; Ufu 3:9; Mt 4:10Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani. 102:10 Ufu 3:10; Dan 1:12-14Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.

112:11 Ufu 20:6-14; 21:8“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.

Kwa Kanisa Lililoko Pergamo

122:12 Ufu 1:11-16; 1:17, 18; 2:7“Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika:

“Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili. 132:13 Ufu 14:12Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.

142:14 1Pet 2:15; 1Kor 6:13“Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati. 152:15 Ufu 2:6Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai. 162:16 2The 2:8Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.

172:17 Yn 6:49-50; Isa 62:2; Ufu 19:12“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.

Kwa Kanisa Lililoko Thiatira

182:18 Ufu 1:11-15“Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika:

“Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana. 192:19 Ufu 2:2Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.

202:20 1Fal 21:25; 2Fal 9:7“Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu. 212:21 Rum 2:4; Ufu 9:20Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki. 222:22 Ufu 17:2; 18:9Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake. 232:23 1Sam 16:7; Yer 11:20Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake. 242:24 Mdo 15:28Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu): 252:25 Ufu 3:11Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.

262:26 Za 2:8; Ufu 3:21“Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:

272:27 Ufu 12:5; Za 2:9; Yer 19:11“ ‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma,

atawavunja vipande vipande

kama chombo cha udongo’:

kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu. 282:28 Ufu 22:16Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi. 29Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

启示录 2:1-29

给以弗所教会的信

1“你要写信告诉以弗所教会的天使,那位右手拿着七颗星、往来于七个金灯台中间的主说, 2‘我知道你的行为、劳碌和坚忍,也知道你嫉恶如仇,曾查验出那些假冒的使徒,揭穿他们的虚假。 3你曾坚定不移地为我的名受苦,没有气馁。 4但有一件事我要责备你,就是你把起初的爱心丢弃了。 5因此,要回想你在哪里跌倒了,并且悔改,照起初所行的去行。否则,我就要到你那里,将你的灯台从原处拿走。 6然而你还有一点可取之处,就是你跟我一样痛恨尼哥拉党人的行径。

7“‘圣灵对各教会所说的话,凡有耳朵的都应当听。我必将上帝乐园中生命树上的果子赐给得胜者吃。’

给士每拿教会的信

8“你要写信告诉士每拿教会的天使,那位首先的、末后的、死而复活的主说, 9‘我知道你遭受的苦难和贫穷,其实你是富足的。我也知道那些人对你的毁谤,他们自称是犹太人,其实他们不是,而是撒旦的会众。 10你不要害怕将要遭受的苦难。看啊,魔鬼要将你们当中的一些人下在监牢,使你们受试炼,你们必遭受十天的迫害。你要至死忠心,我必赐给你生命的冠冕。

11“‘圣灵对各教会所说的话,凡有耳朵的都应当听。得胜者必不被第二次死亡所害。’

给别迦摩教会的信

12“你要写信告诉别迦摩教会的天使,那位有两刃利剑的主说, 13‘我知道你住在撒旦称王的地方。但你仍然坚守我的名,即使我忠心的见证人安提帕在你们这撒旦盘踞之处殉道的时候,你也没有否认对我的信仰。 14不过有几件事我要责备你:你那里有人随从巴兰的教导,这巴兰从前教巴勒以色列人面前设置绊脚石,使他们吃祭过偶像的食物并陷入淫乱。 15同样,你那里也有人附从尼哥拉党的教导。 16所以你要悔改,否则我必迅速到你那里,用我口中的剑攻击他们。

17“‘圣灵对各教会所说的话,凡有耳朵的都应当听。我必将隐藏的吗哪赐给得胜者。我也要赐给他一块白石,石上写着一个新名字,除了那领受的人以外,没有人认识。’

给推雅推喇教会的信

18“你要写信告诉推雅推喇教会的天使,双目如炬、双脚像闪亮精铜的上帝的儿子说, 19‘我知道你的行为、爱心、信心、事奉和坚忍,也知道你现在所做的善事比起初更多。 20但有一件事我要责备你,就是你容许那自称是先知的妇人耶洗别教导我的众奴仆,诱骗他们陷入淫乱并吃祭过偶像的食物。 21我曾给她悔改的机会,她却不肯痛改自己的淫乱行为, 22所以我必叫她卧病在床。那些与她有染的人若不悔改,也必遭受极大的苦难。 23我要击杀她的爪牙2:23 “爪牙”希腊文是“儿女”。,使众教会都知道我洞察人的心思意念,我要照你们各人的行为对待你们。

24“‘至于你们其余在推雅推喇的人,就是不听那邪说,没有学习所谓的撒旦玄学的人,我告诉你们,我不会将别的重担放在你们身上。 25但你们要持守所拥有的,一直到我来。 26-27我怎样从我父领受了权柄,也必照样把统治列国的权柄赐给遵守我命令到底的得胜者,他必用铁杖管辖列国,将他们如同陶器一般打得粉碎。2:26‑27 诗篇2:9 28我也要把晨星赐给他。

29“‘圣灵对各教会所说的话,凡有耳朵的都应当听。’