Tito 2 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Tito 2:1-15

Fundisha Mafundisho Manyofu

12:1 1Tim 1:10; 6:3; 2Tim 1:13Inakupasa kufundisha itikadi sahihi. 22:2 Tit 1:13; 1Tim 5:1; 3:2; Tit 2:5, 6, 12; 1:8, 13Wafundishe wazee kuwa na kiasi, wastahivu, wenye busara na wanyofu katika imani, upendo na saburi.

32:3 1Tim 3:8; 3:11Vivyo hivyo, wafundishe wanawake wazee kuwa na mwenendo wa utakatifu, wala wasiwe wasingiziaji au walevi, bali wafundishe yale yaliyo mema, 42:4 1Tim 5:2, 14ili waweze kuwafundisha wanawake vijana kuwa na kiasi, wawapende waume zao na kuwapenda watoto wao, 52:5 Efe 5:22; 1Tim 6:1wawe waaminifu, watakatifu, wakitunza vyema nyumba zao, wema, watiifu kwa waume zao, ili mtu yeyote asije akalikufuru neno la Mungu.

62:6 1Tim 5:1Vivyo hivyo, himiza vijana wawe na kiasi. 72:7 1Tim 4:12; Tit 2:14Katika kila jambo uwe kielelezo kwa kutenda mema. Katika mafundisho yako uonyeshe uadilifu, utaratibu, 82:8 1Pet 2:12; 1Tim 6:3; Neh 5:9; 1Tim 5:14; 2The 3:14na usemi sahihi usio na lawama, ili wanaokupinga watahayari, wakose neno lolote baya la kusema juu yetu.

92:9 Efe 6:5; Kol 3:22; 1Tim 6:12; 1Pet 2:18; Efe 5:24Wafundishe watumwa kuwatii mabwana zao katika kila jambo, wakijitahidi kuwapendeza wala wasijibizane nao, 102:10 Mt 5:16; Flp 2:15; Tit 1:3; Lk 1:47wala wasiwaibie, bali waonyeshe kuwa wanaweza kuaminika kabisa, ili kwa kila namna wayafanye mafundisho ya Mungu Mwokozi wetu yawe ya kuvutia.

112:11 1Tim 2:4; Rum 3:24; 2Tim 1:10Kwa maana neema ya Mungu ambayo inawaokoa wanadamu wote imefunuliwa. 122:12 Tit 3:3; 2Tim 3:12Nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia, ili tupate kuishi maisha ya kiasi, ya haki na ya utaua katika ulimwengu huu wa sasa, 132:13 2Pet 1:1; 1Kor 1:7; 1Tim 6:14; Flp 3:20huku tukilitazamia tumaini lenye baraka na ufunuo wa utukufu wa Mungu wetu Mkuu, aliye Mwokozi wetu Yesu Kristo. 142:14 Za 85:4; Mit 16:7Ndiye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe kutoka uovu wote na kujisafishia watu kuwa mali yake Mwenyewe, yaani, wale walio na juhudi katika kutenda mema.

15Basi wewe fundisha mambo haya. Onya na kukaripia kwa mamlaka yote. Mtu yeyote asikudharau.