Nehemia 12 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 12:1-47

Makuhani Na Walawi Waliorudi Na Zerubabeli

112:1 Neh 10:2-8; Zek 4:6-10; Ezr 3:2Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua:

Seraya, Yeremia, Ezra,

2Amaria, Maluki, Hatushi,

3Shekania, Rehumu, Meremothi,

412:4 Lk 1:5; 1Nya 24:10Ido, Ginethoni, Abiya,

5Miyamini, Moadia, Bilga,

612:6 1Nya 24:7Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,

712:7 Hag 1:1; Zek 5:1; Ezr 3:2Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya.

Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.

812:8 Neh 11:17; 1Nya 16:8Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani. 9Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.

1012:10 Ezr 10:24; Neh 3:20Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada, 11Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.

12Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani:

wa jamaa ya Seraya, Meraya;

wa jamaa ya Yeremia, Hanania;

13wa jamaa ya Ezra, Meshulamu;

wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;

14wa jamaa ya Maluki, Yonathani;

wa jamaa ya Shebania, Yosefu;

15wa jamaa ya Harimu, Adna;

wa jamaa ya Meremothi, Helkai;

1612:16 Neh 12:4wa jamaa ya Ido, Zekaria;

wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;

1712:17 1Nya 24:10wa jamaa ya Abiya, Zikri;

wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;

18wa jamaa ya Bilgai, Shamua;

wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;

19wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai;

wa jamaa ya Yedaya, Uzi;

20wa jamaa ya Salu, Kalai;

wa jamaa ya Amoki, Eberi;

21wa jamaa ya Hilkia, Hashabia;

wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.

22Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi. 2312:23 1Nya 9:14Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu. 2412:24 Ezr 2:40; 3:11; 1Nya 23:1Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.

25Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu. 2612:26 Neh 8:9; Ezr 7:6, 11Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.

Kuwekwa Wakfu Ukuta Wa Yerusalemu

2712:27 Kum 20:5; 2Sam 6:5; 1Nya 25:6; Za 81:1-3; 92:3Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze. 2812:28 1Nya 2:54; 9:16Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi, 29kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu. 3012:30 Kut 19:10; Ay 1:5Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.

3112:31 Neh 2:13; Ezr 3:10; Hes 10:2; 2Nya 5:12Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi. 32Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata, 33pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 3412:34 Ezr 1:5Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia, 3512:35 Ezr 3:10pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu, 3612:36 1Nya 23:5; 15:16; 2Nya 8:14pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano. 3712:37 Neh 2:14; 3:3-15; 3:26; 2Sam 5:7-9Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.

3812:38 Neh 3:8-11Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana, 3912:39 2Fal 14:13; Neh 8:16; 2Nya 33:14; Neh 3:1-6juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.

4012:40 Za 42:4Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa, 41na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao, 42na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia. 4312:43 Za 9:2; 92:4Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.

4412:44 Neh 13:4, 13; Law 27:30; Kum 18:8Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi. 4512:45 1Nya 25:1; 2Nya 8:14; 1Nya 6:31; 23:5Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe. 4612:46 2Nya 35:15; 29:27Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu. 4712:47 Hes 18:21; Kum 18:8Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

Swedish Contemporary Bible

Nehemja 12:1-47

Präster och leviter

1Dessa var de präster, som återvände med Serubbabel, Shealtiels son, och Jeshua:

Seraja, Jeremia, Esra,

2Amarja, Malluk, Hattush,

3Shekanja, Rechum, Meremot,

4Iddo, Ginneton, Avia,

5Mijamin, Maadja, Bilga,

6Shemaja, Jojariv, Jedaja,

7Sallu, Amok, Hilkia och Jedaja.

Dessa var ledare för prästerna och deras medhjälpare under Jeshuas tid.

8Leviter: Jeshua, Binnuj, Kadmiel, Sherevja, Juda och Mattanja som tillsammans med sina bröder ansvarade för lovsången. 9Bakbukja och Unni var deras medhjälpare och stod mitt emot dem under gudstjänsten.

10Jeshua var far till Jojakim, Jojakim var far till Eljashiv, Eljashiv var far till Jojada, 11Jojada var far till Jonatan och Jonatan var far till Jaddua.

12På Jojakims tid var överhuvudena för prästernas familjer följande:

Meraja för Seraja, Hananja för Jeremia,

13Meshullam för Esra, Jochanan för Amarja,

14Jonatan för Malluk, Josef för Shevanja,

15Adna för Harim, Helkaj för Merajot,

16Sakarja för Iddo, Meshullam för Ginneton,

17Sikri för Avias familj, …för Minjamin12:17 Ett namn saknas i grundtexten., och Piltaj för Moadja,

18Shammua för Bilga, Jonatan för Shemaja,

19Mattenaj för Jojariv, Ussi för Jedaja,

20Kallaj för Sallu, Ever för Amok,

21Hashavja för Hilkia och Netanel för Jedaja.

22Ett släktregister över leviternas överhuvuden på Eljashivs, Jojadas, Jochanans och Jadduas tid, och ett register över prästerna upprättades under den persiske kungen Dareios regering.

23Överhuvudena för leviternas släkter fanns också registrerade i krönikorna fram till Jochanans, Eljashivs sons, tid.

24De ledande bland leviterna var Hashavja, Sherevja och Jeshua, Kadmiels son, och deras medhjälpare, som stod mitt emot dem för att växelvis lova och prisa, enligt gudsmannen Davids anvisningar.

25Dörrvakter som tjänstgjorde vid förrådshusen vid portarna var Mattanja, Bakbukja, Obadja, Meshullam, Talmon och Ackuv. 26Dessa var samtida med Jojakim, som var son till Jeshua och sonson till Josadak, och med ståthållaren Nehemja och prästen Esra, den skriftlärde.

Muren invigs

27Vid invigningen av Jerusalems mur sökte man upp leviter från alla platser där de bodde för att föra dem till Jerusalem för att fira invignings- och glädjehögtid med lovsång till cymbaler, harpor och lyror. 28Sångare samlades då från regionen kring Jerusalem och från netofatéernas byar, 29från Bet Haggilgal och från trakterna kring Geva och Asmavet. De hade byggt sina byar runt Jerusalem. 30Prästerna och leviterna renade först sig själva och därefter folket, portarna och muren.

31Jag lät ledarna i Juda stiga upp på muren och ordnade två stora lovsångskörer. Den ena av dem gick till höger på muren, i riktning mot Dyngporten, 32och följdes av Hoshaja och hälften av ledarna i Juda, 33Asarja, Esra, Meshullam, 34Juda, Benjamin, Shemaja och Jeremia, 35och några präster som blåste i trumpet, Sakarja, son till Jonatan, son till Shemaja, son till Mattanja, son till Mikaja, son till Sackur, son till Asaf, 36och hans släktingar Shemaja, Asarel, Milalaj, Gilalaj, Maaj, Netanel, Juda och Hanani.

De använde gudsmannen Davids musikinstrument, och prästen Esra, den skriftlärde, gick framför dem. 37Vid Källporten fortsatte de rakt fram och uppför trapporna till Davids stad, på trappan på muren ovanför Davids hus, och sedan fram till Vattenporten mot öster.

38Den andra kören gick åt motsatta hållet, och jag följde efter dem med den andra hälften av folket. Vi gick på muren, förbi Ugnstornet till Breda muren 39och sedan förbi Efraimporten, Jeshanaporten, Fiskporten, Hananeltornet, Hundradetornet, bort till Fårporten och stannade vid Vaktporten.

40De två lovsångskörerna ställde sig sedan vid Guds hus, liksom jag, tillsammans med hälften av styresmännen 41och prästerna Eljakim, Maaseja, Minjamin, Mikaja, Eljoenaj, Sakarja och Hananja med sina trumpeter 42samt Maaseja, Shemaja, Elasar, Ussi, Jochanan, Malkia, Elam och Eser. Sångarna sjöng under ledning av Jisrachja.

43De bar fram stora offer på denna dag och gladde sig, för Gud hade gett dem en stor glädje. Också kvinnorna och barnen gladde sig. Glädjen från Jerusalem hördes vida omkring.

Underhåll till leviterna

44Vid samma tid tillsattes män att ansvara för skattkamrarna, där man förvarade offergåvorna, det första av skörden och tiondet. Dessa män skulle samla in från städernas åkrar det som enligt lagen tillföll prästerna och leviterna. I Juda gladde man sig åt att prästerna och leviterna nu gjorde tjänst igen. 45De skötte tjänsten för sin Gud och för reningarna, och sångarna och dörrvakterna skötte sin tjänst, så som David och hans son Salomo hade befallt. 46Redan för länge sedan, under Davids och Asafs tid, fanns det ledare för sångarna, som lovsjöng och prisade Gud. 47Nu, under Serubbabels och Nehemjas tid, gav israeliterna dagligen till sångarna och dörrvakterna vad de behövde. Man gav också leviterna deras helgade andel, och leviterna i sin tur gav Arons ättlingar deras helgade andel.