Nehemia 12 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Nehemia 12:1-47

Makuhani Na Walawi Waliorudi Na Zerubabeli

112:1 Neh 10:2-8; Zek 4:6-10; Ezr 3:2Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua:

Seraya, Yeremia, Ezra,

2Amaria, Maluki, Hatushi,

3Shekania, Rehumu, Meremothi,

412:4 Lk 1:5; 1Nya 24:10Ido, Ginethoni, Abiya,

5Miyamini, Moadia, Bilga,

612:6 1Nya 24:7Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,

712:7 Hag 1:1; Zek 5:1; Ezr 3:2Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya.

Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.

812:8 Neh 11:17; 1Nya 16:8Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani. 9Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.

1012:10 Ezr 10:24; Neh 3:20Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada, 11Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.

12Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani:

wa jamaa ya Seraya, Meraya;

wa jamaa ya Yeremia, Hanania;

13wa jamaa ya Ezra, Meshulamu;

wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;

14wa jamaa ya Maluki, Yonathani;

wa jamaa ya Shebania, Yosefu;

15wa jamaa ya Harimu, Adna;

wa jamaa ya Meremothi, Helkai;

1612:16 Neh 12:4wa jamaa ya Ido, Zekaria;

wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;

1712:17 1Nya 24:10wa jamaa ya Abiya, Zikri;

wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;

18wa jamaa ya Bilgai, Shamua;

wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;

19wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai;

wa jamaa ya Yedaya, Uzi;

20wa jamaa ya Salu, Kalai;

wa jamaa ya Amoki, Eberi;

21wa jamaa ya Hilkia, Hashabia;

wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.

22Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi. 2312:23 1Nya 9:14Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu. 2412:24 Ezr 2:40; 3:11; 1Nya 23:1Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.

25Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu. 2612:26 Neh 8:9; Ezr 7:6, 11Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.

Kuwekwa Wakfu Ukuta Wa Yerusalemu

2712:27 Kum 20:5; 2Sam 6:5; 1Nya 25:6; Za 81:1-3; 92:3Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze. 2812:28 1Nya 2:54; 9:16Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi, 29kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu. 3012:30 Kut 19:10; Ay 1:5Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.

3112:31 Neh 2:13; Ezr 3:10; Hes 10:2; 2Nya 5:12Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi. 32Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata, 33pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 3412:34 Ezr 1:5Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia, 3512:35 Ezr 3:10pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu, 3612:36 1Nya 23:5; 15:16; 2Nya 8:14pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano. 3712:37 Neh 2:14; 3:3-15; 3:26; 2Sam 5:7-9Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.

3812:38 Neh 3:8-11Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana, 3912:39 2Fal 14:13; Neh 8:16; 2Nya 33:14; Neh 3:1-6juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.

4012:40 Za 42:4Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa, 41na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao, 42na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia. 4312:43 Za 9:2; 92:4Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.

4412:44 Neh 13:4, 13; Law 27:30; Kum 18:8Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi. 4512:45 1Nya 25:1; 2Nya 8:14; 1Nya 6:31; 23:5Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe. 4612:46 2Nya 35:15; 29:27Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu. 4712:47 Hes 18:21; Kum 18:8Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

New International Version

Nehemiah 12:1-47

Priests and Levites

1These were the priests and Levites who returned with Zerubbabel son of Shealtiel and with Joshua:

Seraiah, Jeremiah, Ezra,

2Amariah, Malluk, Hattush,

3Shekaniah, Rehum, Meremoth,

4Iddo, Ginnethon,12:4 Many Hebrew manuscripts and Vulgate (see also verse 16); most Hebrew manuscripts Ginnethoi Abijah,

5Mijamin,12:5 A variant of Miniamin Moadiah, Bilgah,

6Shemaiah, Joiarib, Jedaiah,

7Sallu, Amok, Hilkiah and Jedaiah.

These were the leaders of the priests and their associates in the days of Joshua.

8The Levites were Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Judah, and also Mattaniah, who, together with his associates, was in charge of the songs of thanksgiving. 9Bakbukiah and Unni, their associates, stood opposite them in the services.

10Joshua was the father of Joiakim, Joiakim the father of Eliashib, Eliashib the father of Joiada, 11Joiada the father of Jonathan, and Jonathan the father of Jaddua.

12In the days of Joiakim, these were the heads of the priestly families:

of Seraiah’s family, Meraiah;

of Jeremiah’s, Hananiah;

13of Ezra’s, Meshullam;

of Amariah’s, Jehohanan;

14of Malluk’s, Jonathan;

of Shekaniah’s,12:14 Very many Hebrew manuscripts, some Septuagint manuscripts and Syriac (see also verse 3); most Hebrew manuscripts Shebaniah’s Joseph;

15of Harim’s, Adna;

of Meremoth’s,12:15 Some Septuagint manuscripts (see also verse 3); Hebrew Meraioth’s Helkai;

16of Iddo’s, Zechariah;

of Ginnethon’s, Meshullam;

17of Abijah’s, Zikri;

of Miniamin’s and of Moadiah’s, Piltai;

18of Bilgah’s, Shammua;

of Shemaiah’s, Jehonathan;

19of Joiarib’s, Mattenai;

of Jedaiah’s, Uzzi;

20of Sallu’s, Kallai;

of Amok’s, Eber;

21of Hilkiah’s, Hashabiah;

of Jedaiah’s, Nethanel.

22The family heads of the Levites in the days of Eliashib, Joiada, Johanan and Jaddua, as well as those of the priests, were recorded in the reign of Darius the Persian. 23The family heads among the descendants of Levi up to the time of Johanan son of Eliashib were recorded in the book of the annals. 24And the leaders of the Levites were Hashabiah, Sherebiah, Jeshua son of Kadmiel, and their associates, who stood opposite them to give praise and thanksgiving, one section responding to the other, as prescribed by David the man of God.

25Mattaniah, Bakbukiah, Obadiah, Meshullam, Talmon and Akkub were gatekeepers who guarded the storerooms at the gates. 26They served in the days of Joiakim son of Joshua, the son of Jozadak, and in the days of Nehemiah the governor and of Ezra the priest, the teacher of the Law.

Dedication of the Wall of Jerusalem

27At the dedication of the wall of Jerusalem, the Levites were sought out from where they lived and were brought to Jerusalem to celebrate joyfully the dedication with songs of thanksgiving and with the music of cymbals, harps and lyres. 28The musicians also were brought together from the region around Jerusalem—from the villages of the Netophathites, 29from Beth Gilgal, and from the area of Geba and Azmaveth, for the musicians had built villages for themselves around Jerusalem. 30When the priests and Levites had purified themselves ceremonially, they purified the people, the gates and the wall.

31I had the leaders of Judah go up on top of12:31 Or go alongside the wall. I also assigned two large choirs to give thanks. One was to proceed on top of12:31 Or proceed alongside the wall to the right, toward the Dung Gate. 32Hoshaiah and half the leaders of Judah followed them, 33along with Azariah, Ezra, Meshullam, 34Judah, Benjamin, Shemaiah, Jeremiah, 35as well as some priests with trumpets, and also Zechariah son of Jonathan, the son of Shemaiah, the son of Mattaniah, the son of Micaiah, the son of Zakkur, the son of Asaph, 36and his associates—Shemaiah, Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethanel, Judah and Hanani—with musical instruments prescribed by David the man of God. Ezra the teacher of the Law led the procession. 37At the Fountain Gate they continued directly up the steps of the City of David on the ascent to the wall and passed above the site of David’s palace to the Water Gate on the east.

38The second choir proceeded in the opposite direction. I followed them on top of12:38 Or them alongside the wall, together with half the people—past the Tower of the Ovens to the Broad Wall, 39over the Gate of Ephraim, the Jeshanah12:39 Or Old Gate, the Fish Gate, the Tower of Hananel and the Tower of the Hundred, as far as the Sheep Gate. At the Gate of the Guard they stopped.

40The two choirs that gave thanks then took their places in the house of God; so did I, together with half the officials, 41as well as the priests—Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah and Hananiah with their trumpets— 42and also Maaseiah, Shemaiah, Eleazar, Uzzi, Jehohanan, Malkijah, Elam and Ezer. The choirs sang under the direction of Jezrahiah. 43And on that day they offered great sacrifices, rejoicing because God had given them great joy. The women and children also rejoiced. The sound of rejoicing in Jerusalem could be heard far away.

44At that time men were appointed to be in charge of the storerooms for the contributions, firstfruits and tithes. From the fields around the towns they were to bring into the storerooms the portions required by the Law for the priests and the Levites, for Judah was pleased with the ministering priests and Levites. 45They performed the service of their God and the service of purification, as did also the musicians and gatekeepers, according to the commands of David and his son Solomon. 46For long ago, in the days of David and Asaph, there had been directors for the musicians and for the songs of praise and thanksgiving to God. 47So in the days of Zerubbabel and of Nehemiah, all Israel contributed the daily portions for the musicians and the gatekeepers. They also set aside the portion for the other Levites, and the Levites set aside the portion for the descendants of Aaron.