Nahumu 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Nahumu 2:1-13

Ninawi Kuanguka

12:1 Yer 51:20Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi.

Linda ngome,

chunga barabara,

jitieni nguvu wenyewe,

kusanya nguvu zako zote!

22:2 Eze 37:23; Isa 60:15Bwana atarudisha fahari ya Yakobo,

kama fahari ya Israeli,

ingawa waangamizi wamewaacha ukiwa

na wameharibu mizabibu yao.

32:3 Eze 23:14-15Ngao za askari wake ni nyekundu,

mashujaa wamevaa nguo nyekundu.

Chuma kwenye magari ya vita chametameta,

katika siku aliyoyaweka tayari,

mikuki ya mierezi inametameta.

42:4 Yer 4:13; Eze 23:24Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani,

yakikimbia nyuma na mbele uwanjani.

Yanaonekana kama mienge ya moto;

yanakwenda kasi kama umeme.

52:5 Yer 46:12Anaita vikosi vilivyochaguliwa,

lakini bado wanajikwaa njiani.

Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wa mji,

ile ngao ya kuwakinga imetayarishwa.

62:6 Isa 45:1; Nah 3:13Malango ya mto yamefunguliwa wazi,

na jumba la kifalme limeanguka.

72:7 Mwa 8:8; Isa 59:11; 32:12Imeagizwa kwamba mji uchukuliwe

na upelekwe uhamishoni.

Vijakazi wake wanaomboleza kama hua

na kupigapiga vifua vyao.

8Ninawi ni kama dimbwi,

nayo maji yake yanakauka.

Wanalia, “Simama! Simama!”

Lakini hakuna anayegeuka nyuma.

9Chukueni nyara za fedha!

Chukueni nyara za dhahabu!

Wingi wake hauna mwisho,

utajiri kutoka hazina zake zote!

102:10 Yos 2:11; 7:5; Isa 29:22Ameharibiwa, ametekwa nyara, ameachwa uchi!

Mioyo inayeyuka, magoti yanalegea,

miili inatetemeka,

na kila uso umebadilika rangi.

112:11 Isa 5:29Liko wapi sasa pango la simba,

mahali ambapo waliwalisha watoto wao,

ambapo simba dume na simba jike walikwenda

na ambapo wana simba walikwenda

bila kuogopa chochote?

122:12 Yer 51:34; 4:7; Isa 37:18Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake,

alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake,

akijaza makao yake kwa alivyoua

na mapango yake kwa mawindo.

132:13 Isa 10:5-13; Yer 21:13; Nah 3:5; Za 46:9; 2Sam 2:26; Mik 5:6Bwana Mwenye Nguvu Zote anatangaza,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Magari yenu ya vita nitayateketeza kwa moto,

na upanga utakula wana simba wako.

Sitawaachia mawindo juu ya nchi.

Sauti za wajumbe wako

hazitasikika tena.”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

那鸿书 2:1-13

尼尼微的覆灭

1尼尼微啊,

攻击者已经向你扑来。

你要进驻堡垒,

把守道路,

集中全力,

准备上阵!

2虽然掳掠者曾掳掠雅各

掳掠以色列

毁坏他们的葡萄树枝,

但耶和华必恢复雅各的荣耀,

恢复以色列的荣耀。

3他的勇士手持红色盾牌,

他的士兵身穿朱红战衣。

他们整装待发之日,

战车铁光闪闪,

松木矛枪在空中挥舞。

4战车在街道上狂奔,

在广场上横冲直撞,

亮如火炬,疾似闪电。

5亚述王召集将领,

他们一路跌跌撞撞,

奔上城墙,架起防御盾牌。

6河闸大开,宫殿坍塌。

7王后赤身被掳;

宫女捶胸悲泣,

像鸽子一样哀鸣。

8尼尼微城自古以来就像聚水的池子,

如今居民却像泄漏的池水四散奔逃。

虽有人喊:“站住!站住!”

却无人回头。

9抢银子吧!抢金子吧!

城里有无尽的财富和数不清的宝物。

10尼尼微被洗劫一空!

沦为废墟!

一片荒凉!

人们胆战心惊,双膝哆嗦,

浑身发抖,面色苍白。

11如今那狮子的洞穴,

那喂养猛狮的地方在哪里呢?

从前,雄狮、母狮和幼狮曾在那里出入,

无人惊扰。

12雄狮为幼狮撕碎充足的食物,

为母狮绞杀猎物,

洞穴里堆满猎物,

堆满撕碎的肉。

13万军之耶和华说:

“我与你为敌,

我要烧毁你的战车,

使刀剑吞噬你的猛狮;

我要使你无法再掳掠他国,

你使者的声音将从此消逝。”