Mwanzo 9 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 9:1-29

Mungu Aweka Agano Na Noa

19:1 Mwa 1:22Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia. 29:2 Mwa 1:26Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu. 39:3 Mwa 1:29; Kol 2:16; Mdo 10:15Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.

49:4 Law 3:17; 7:26; 17:10-14; 19:26; Kum 12:16, 23-25; 15:23; 1Sam 14:33; Eze 33:25; Mdo 15:20, 29“Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai. 59:5 Mwa 4:10; 42:22; 50:15; 1Fal 2:32; 2Nya 24:22; Za 9:12; Kut 21:28-32Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.

69:6 Mwa 1:26; 4:14; Amu 9:24; Mt 26:52“Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu,

damu yake itamwagwa na mwanadamu,

kwa kuwa katika mfano wa Mungu,

Mungu alimuumba mwanadamu.

79:7 Mwa 1:22; 9:19Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”

8Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye: 99:9 Mwa 6:18“Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu, 10pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani. 119:11 Isa 24:5; 33:8; 54:9; Hos 6:7; Mwa 8:21Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”

129:12 Mwa 17:11-12; Kut 12:14; Law 3:17; 6:18; 17:7; Hes 10:8Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo: 139:13 Eze 1:28; Ufu 4:3; 10:1Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia. 14Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni, 159:15 Mwa 8:1, 21; Kut 2:24; 6:5; 34:10; Law 26:42-45; Kum 7:9; Za 89:34; 103:18; 105:8; 106:45; Eze 16:60nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote. 169:16 Mwa 17:7-13, 19; 2Sam 7:13; 23:5; Za 105:9-10; Isa 9:7; 54:10; 55:3; 59:21; 61:8; Yer 31:34; 32:40; 33:21; Eze 16:60; 37:26; Ebr 13:20Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”

17Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”

Wana Wa Noa

189:18 Mwa 5:32; 10:6, 15; Lk 3:36Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.) 199:19 Mwa 5:32; 1:22; 10:32; 11:4-9Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.

20Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu. 219:21 Mwa 19:35Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake. 229:22 Hab 2:15Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 23Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.

24Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea, 259:25 Mwa 27:12, 29-40; 25:23; 37:10; 49:8; Kut 20:5; Za 79:8; Isa 14:21; Yer 31:29; 32:18; Hes 24:18; Yos 9:23akasema,

“Alaaniwe Kanaani!

Atakuwa mtumwa wa chini sana

kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”

269:26 Mwa 14:20; Kut 18:10; Za 7:17; 1Fal 9:21Pia akasema,

“Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu!

Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.

279:27 Mwa 10:2-5; Efe 2:13-14; 3:6Mungu na apanue mipaka ya Yafethi;

Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu,

na Kanaani na awe mtumwa wake.”

28Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350. 299:29 Mwa 2:17Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.

Slovo na cestu

1 Mojžíšova 9:1-29

1Tedy požehnal Bůh Noé i synům jeho a řekl jim: Ploďtež se a rozmnožujte se, a naplňte zemi. 2Strach váš a hrůza vaše buď na všeliký živočich země, a na všecko ptactvo nebeské. Všecko, což se hýbe na zemi, a všecky ryby mořské v ruce vaše dány jsou. 3Všecko, což se hýbe a jest živo, bude vám za pokrm; jako i bylinu zelenou, dal jsem vám to všecko. 4A však masa s duší jeho, kteráž jest krev jeho, nebudete jísti. 5A zajisté krve vaší, duší vašich vyhledávati budu; z rukou každého hovada vyhledávati jí budu, i z ruky člověka, ano i z ruky každého bratra jeho budu vyhledávati duše člověka. 6Kdo by koli vylil krev člověka, skrze člověka vylita bude krev jeho; nebo k obrazu svému učinil Bůh člověka. 7Vy pak ploďte a množte se; v hojnosti se rozploďte na zemi, a rozmnoženi buďte na ní. 8I mluvil Bůh k Noé a synům jeho s ním, řka: 9Já zajisté vcházím v smlouvu svou s vámi, i s semenem vaším po vás, 10A se všelikou duší živou, kteráž jest s vámi, z ptactva, z hovad a ze všech živočichů zemských, kteříž jsou s vámi, ode všech, kteříž vyšli z korábu, až do všelikého živočicha zemského. 11Protož utvrzuji smlouvu svou s vámi, že nebude vyhlazeno více všeliké tělo vodami potopy; aniž bude více potopa k zkažení země. 12I řekl Bůh: Totoť bude znamení smlouvy, kteréž já dávám, mezi mnou a mezi vámi, a mezi všelikou duší živou, kteráž jest s vámi, po všecky věky. 13Duhu svou postavil jsem na oblaku, a bude na znamení smlouvy mezi mnou a mezi zemí. 14A budeť, když uvedu mračný oblak nad zemí, a ukáže se duha na oblaku, 15Že se rozpomenu na smlouvu svou, kteráž jest mezi mnou a mezi vámi a mezi všelikou duší živou v každém těle; a nebudou více vody ku potopě, aby zahladily všeliké tělo. 16Nebo když bude duha ta na oblaku, popatřím na ni, abych se rozpomenul na smlouvu věčnou mezi Bohem a mezi všelikou duší živou v každém těle, kteréž jest na zemi. 17I řekl Bůh k Noé: Toť jest znamení smlouvy, kterouž jsem utvrdil mezi sebou a mezi všelikým tělem, kteréž jest na zemi. 18Byli pak synové Noé, kteříž vyšli z korábu: Sem, Cham a Jáfet; a Cham byl otec Kanánův. 19Ti tři jsou synové Noé, a ti se rozprostřeli po vší zemi. 20Noé pak obíraje se s zemí, začal dělati vinice. 21A pije víno, opil se, a obnažil se u prostřed stanu svého. 22Viděl pak Cham, otec Kanánův, hanbu otce svého, a pověděl oběma bratřím svým vně. 23Tedy vzali Sem a Jáfet oděv, kterýžto oba položili na ramena svá, a jdouce zpátkem, zakryli hanbu otce svého; tváři pak jich byly odvráceny, a hanby otce svého neviděli. 24Procítiv pak Noé po svém víně, zvěděl, co mu učinil syn jeho mladší. 25I řekl: Zlořečený Kanán, služebník služebníků bude bratřím svým. 26Řekl také: Požehnaný Hospodin, Bůh Semův, a buď Kanán služebníkem jejich. 27Rozšiřiž Bůh milostivě Jáfeta, aby bydlil v stáncích Semových, a buď Kanán služebníkem jejich. 28Živ pak byl Noé po potopě tři sta a padesáte let. 29A tak bylo všech dnů Noé devět set a padesáte let; i umřel jest.