Mwanzo 8 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 8:1-22

Mwisho Wa Gharika

18:1 Mwa 9:15; 19:29; 21:1; 30:22; Kut 2:23-24; Ay 12:15; 14:13; Rut 4:13; Nah 1:4; 1Sam 1:11, 19; 2Fal 20:3; 1Nya 16:15; Neh 1:8; 5:19; 13:11-31; Hes 10:9; Za 66:6; 105:42; 106:4; Lk 1:54, 72; Kut 14:21; Yos 2:10; 3:16; Isa 11:15; 44:27Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka. 28:2 Mwa 7:4, 11Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani. 38:3 Mwa 7:24Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua, 48:4 Mwa 7:11, 20; 2Fal 19:37; Yer 51:27katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati. 5Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.

6Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina 78:7 Amu 11:15; Kum 14:14; 1Fal 17:4-6; Ay 38:41; Za 147:9; Mit 30:17; Isa 34:11; Lk 12:24na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi. 88:8 Ay 30:31; Za 55:6; 74:19; Wim 2:12-14; Isa 38:14; 59:11; 60:8; Yer 48:28; Eze 7:16; Nah 2:7; Hos 7:11; 11:11; Mt 3:16; 10:16; Yn 1:32Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi. 9Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina. 10Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina. 11Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia. 12Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.

138:13 Mwa 5:32Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka. 148:14 Mwa 7:11Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.

15Ndipo Mungu akamwambia Noa, 168:16 Mwa 7:13“Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao. 178:17 Mwa 1:22Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”

188:18 1Pet 3:20; 2Pet 2:5Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao. 19Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.

Noa Atoa Dhabihu

208:20 Mwa 12:7-8; 13:18; 22:9; 26:25; 33:20; 35:7; 7:8; 22:2-13; Kut 17:15; 24:4; 10:25; 20:24; 40:29; Ay 42:8; Law 1:3; 4:29; 6:8-13; Hes 6:11; Amu 6:26; 11:31; 1Sam 20:29Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. 218:21 Kut 29:18, 25; Law 1:9, 13; 2:9; 4:31; Hes 15:3, 7; 2Kor 2:15; Mwa 3:17; 6:5; 9:11-15; Yer 17:9; Za 51:5; Mt 15:19; Rum 1:21; Yer 44:11; Isa 54:9Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.

228:22 Yos 3:15; Za 67:6; 74:17; Yer 5:24; Zek 14:8; Mwa 1:14“Kwa muda dunia idumupo,

wakati wa kupanda na wa kuvuna,

wakati wa baridi na wa joto,

wakati wa kiangazi na wa masika,

usiku na mchana

kamwe havitakoma.”

Swedish Contemporary Bible

1 Moseboken 8:1-22

1Gud tänkte på Noa och alla vilda och tama djur i arken. Han lät en vind blåsa över jorden så att vattnet började sjunka undan. 2Djupets källor och himlens luckor stängdes, och skyfallen avtog. 3Vattnet fortsatte att sjunka undan. Efter 150 dagar minskade vattnet så mycket 4att arken stannade på Araratbergen på sjuttonde dagen i sjunde månaden. 5På första dagen i tionde månaden hade vattnet minskat så mycket att bergstoppar började bli synliga.

6Efter fyrtio dagar öppnade Noa fönstret som han hade gjort i arken 7och släppte ut en korp som flög fram och tillbaka tills jorden blivit torr. 8Sedan skickade Noa också ut en duva för att se om den kunde hitta torr mark, 9men duvan fann ingen plats att vila på utan återvände till Noa i arken. Vattnet stod fortfarande för högt på jorden. Då sträckte Noa ut sin hand och tog in duvan i arken igen.

10Sju dagar senare släppte Noa än en gång ut duvan ur arken, 11och nu återvände fågeln mot kvällen med ett friskt olivlöv i näbben. Då visste Noa att vattnet sjunkit undan. 12En vecka senare släppte han ut duvan igen och den gången kom den inte tillbaka.

13I Noas sexhundraförsta år, på första månadens första dag, hade vattnet torkat bort från jorden. Noa tog bort arkens tak och såg att marken hade torkat upp. 14På tjugosjunde dagen i andra månaden var jorden torr. 15Då sa Gud till Noa: 16”Gå ut ur arken, du och din hustru, dina söner och dina svärdöttrar. 17Ta med dig ut alla djur som är hos dig, fyrfotadjur, fåglar och markens kräldjur. Det ska bli ett myller av dem på jorden. De ska föröka sig och bli många på jorden.” 18Noa, hans söner, hans hustru och hans svärdöttrar gick ut. 19Fyrfotadjuren, kräldjuren och fåglarna, allt som rör sig på jorden lämnade arken, den ena sorten efter den andra.

20Sedan byggde Noa ett altare åt Herren. På det offrade han fyrfotadjur och fåglar av alla rena sorter som brännoffer. 21Herren kände den behagliga doften och sa för sig själv: ”Jag ska aldrig mer förbanna jorden för människans skull, för människans hjärtas tankar är onda redan från den tidigaste ungdomen. Jag ska aldrig mer förgöra allt levande som jag nu har gjort.

22Så länge som jorden finns kvar

kommer sådd och skörd,

köld och värme,

sommar och vinter,

dag och natt

aldrig att upphöra.”