Mwanzo 8 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 8:1-22

Mwisho Wa Gharika

18:1 Mwa 9:15; 19:29; 21:1; 30:22; Kut 2:23-24; Ay 12:15; 14:13; Rut 4:13; Nah 1:4; 1Sam 1:11, 19; 2Fal 20:3; 1Nya 16:15; Neh 1:8; 5:19; 13:11-31; Hes 10:9; Za 66:6; 105:42; 106:4; Lk 1:54, 72; Kut 14:21; Yos 2:10; 3:16; Isa 11:15; 44:27Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka. 28:2 Mwa 7:4, 11Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani. 38:3 Mwa 7:24Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua, 48:4 Mwa 7:11, 20; 2Fal 19:37; Yer 51:27katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati. 5Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.

6Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina 78:7 Amu 11:15; Kum 14:14; 1Fal 17:4-6; Ay 38:41; Za 147:9; Mit 30:17; Isa 34:11; Lk 12:24na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi. 88:8 Ay 30:31; Za 55:6; 74:19; Wim 2:12-14; Isa 38:14; 59:11; 60:8; Yer 48:28; Eze 7:16; Nah 2:7; Hos 7:11; 11:11; Mt 3:16; 10:16; Yn 1:32Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi. 9Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina. 10Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina. 11Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia. 12Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.

138:13 Mwa 5:32Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka. 148:14 Mwa 7:11Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.

15Ndipo Mungu akamwambia Noa, 168:16 Mwa 7:13“Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao. 178:17 Mwa 1:22Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”

188:18 1Pet 3:20; 2Pet 2:5Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao. 19Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.

Noa Atoa Dhabihu

208:20 Mwa 12:7-8; 13:18; 22:9; 26:25; 33:20; 35:7; 7:8; 22:2-13; Kut 17:15; 24:4; 10:25; 20:24; 40:29; Ay 42:8; Law 1:3; 4:29; 6:8-13; Hes 6:11; Amu 6:26; 11:31; 1Sam 20:29Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. 218:21 Kut 29:18, 25; Law 1:9, 13; 2:9; 4:31; Hes 15:3, 7; 2Kor 2:15; Mwa 3:17; 6:5; 9:11-15; Yer 17:9; Za 51:5; Mt 15:19; Rum 1:21; Yer 44:11; Isa 54:9Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.

228:22 Yos 3:15; Za 67:6; 74:17; Yer 5:24; Zek 14:8; Mwa 1:14“Kwa muda dunia idumupo,

wakati wa kupanda na wa kuvuna,

wakati wa baridi na wa joto,

wakati wa kiangazi na wa masika,

usiku na mchana

kamwe havitakoma.”

Japanese Contemporary Bible

創世記 8:1-22

8

1船の中のノアとすべての生き物を、神は心にかけていました。やがて神が風を吹きつけると、しだいに水は減り始めました。 2地下水も止まり、滝のように降っていた大雨も収まってきたようです。 3-4降り始めてから百五十日目に水は少しずつ引いていき、とうとう船はアララテ山の頂に止まりました。 5日に日に水位は下がり、三か月後にはほかの山々も姿を現し始めました。

6水が引き始めてから四十日目、ノアは天窓を開いて、 7からすを放しました。からすは、地面が乾くまであちこちを飛び回っていました。 8しばらくしてノアは、今度は鳩を放し、乾いた土地を捜させました。 9けれども鳩は下り立つ所が見つからず、ノアのもとへ帰って来ました。水がまだ全地を覆っていたからです。ノアは腕を伸ばし、鳩を船の中に入れました。

10それから七日後、ノアはまた鳩を飛ばしてみました。 11夕方ごろ戻った鳩を見ると、オリーブの若葉をくわえています。それで、水がかなり引いたことがわかりました。 12さらに一週間後にもう一度放してみると、鳩はそれきり戻りませんでした。

13そのあと、さらに三十日ほどたちました。ノアが船の屋根を取って外を見渡してみると、もう水は引いています。 14しんぼう強く、さらに八週間待つうちに、とうとう地面はすっかり乾きました。 15-16神はノアに言いました。「さあ、家族といっしょに外に出なさい。 17動物も鳥も地をはうものもみな出してやりなさい。それぞれ繁殖して、どんどん増えるようにするのだ。」 18-19それを待っていたように、ノアと妻と息子夫婦、それに動物たちはみな、その種類ごとに船から出ました。

20ノアはそこに主への祭壇を築き、神から指定された動物や鳥をささげ物としてささげました。 21神はそれを喜び、こう心に誓われました。「もう二度とこのようなことはしない。人間は子どもの時から悪い性質を持っていて、悪い考えを抱くものだ。わたしはもう、大地をのろって生き物を滅ぼすようなことは絶対にしない。 22大地がある限り、春の種まきと秋の収穫、暑さと寒さ、冬と夏、昼と夜とが、年ごとにくり返されるだろう。」